Mkuu mchambuzi ingekuwa vizuri kama ungeeleza zaidi kuhusu habari hii. Ukiangalia kwa undani unaweza kuona kuwa hizo kauli mbili ni kama hazijatolewa na DCI, ya kwanza inasema hakuna ushahidi kuwa amelishwa sumu, ya pili inasema jeshi halikuchunguza maradhi. Tuhuma ni kuwa Mwakyembe kalishwa sumu, so implied meaning ni kuwa anasema hajalishwa ila amejilisha, au anasema kuwa Mwakyembe hana tatizo la sumu. So Wizara ya afya inachunguza vipi shutuma? Ukiangalia hizi kauli unaona wazi kabisa mtu anayezisema hawezi kuwa DCI wa Tanzania.
Jeshi letu la Polisi au CID ina maabara na wanasayansi wanaoweza kuchunguza sumu za radiation? hapa Tanzania sumu ya panya yenyewe kuchunguza ni vigumu. Kuna Toxologists wangapi wanaoweza kufanya kazi na tukaamini kuwa wanafanya kazi kweli na tukapewa majibu kweli? au ndio yale yale ya kesi ya nyani kwa ngedere.
Kwa mtazamo wangu ambao unaweza kuwa finyu, ili kubaini kauli ya Manumba ina background gani, ni vizuri tukaangalia sequence of events pamoja na kauli mbalimbali kama ifuatavyo:
· Rais Kikwete katikati ya mwaka 2011 alitamka kwa masikitiko kwenye TV kwamba – "hali ndani ya CCM imefikia hatua mbaya kiasi kwamba watu hawa aminiani tena,
na hauwezi kuacha glasi yako ya maji ovyo ovyo…."
· Baada muda mrefu kufuatia kauli hii ya Rais, Mwakyembe akabainika anasumbuliwa na ugonjwa wa ajabu wa ngozi. Mwakyembe akaenda India lakini bila ya kutoa tamko lolote kuhusu kunyweshwa sumu.
· Wakati Mwakyembe akiwa India, miezi kadhaa, Sitta katika kipindi cha Dakika 45 kwenye ITV akatamka kwamba amemuona Dr. Mwakyembe kabla hajaenda India kuchunguzwa afya yake, na dhahiri Dr. Mwakyembe "
amelishwa sumu", kwani mwili wake umebadilika ghafla, unaota magamba, nywele mwilini zina momonyoka, na ngozi inapukutika kama unga….; Hili likawa tamko la kwanza la kiongozi wa serikali kwamba
Dr. Mwakyembe amelishwa sumu. Lakini bado mwathirika mwenyewe (mwakyembea) alikuwa hajatoa tamko lake la kuhusisha maradhi yake na sumu.
· Mwakyembe akarudi kutoka India, na kusema kwamba anamshukuru Mungu amepona, na kwamba taarifa juu ya ugonjwa wake zimepelekwa serikalini. Lakini bado hakutamka lolote kuhusu sumu.
· Wiki kadhaa zilizopita, wakiwa pamoja katika ibada moja Viwanja vya Tanganyika Packers, Sitta akatangaza mbele ya umati kwamba
Mwakyembe amelishwa sumu, na
kwamba madaktari india wamesema ni bahati sumu haikwenda kwenye moyo, figo wala maini, bali ilitoka nje, ndio maana ngozi yake ikapata madhara husika. Sitta akasema pia kwamba Serikali ina taarifa zote juu ya hili na kama inataka kupingana nae, basi ielezee umma nini kimemsibu Dr. Mwakyembe. Kwa upande wake, Dr. Mwakyembe katika ibada ile, hakusema lolote kuhusu
kulishwa sumu, zaidi ya kushukuru kwamba sasa amepona, Mungu atalipa, na kuomba wahumini wamwombee pia Professor Mwandosya na yeye apone.
· Baada ya tamko la Sitta kuhusu Mwakyembe
kulishwa sumu, na kwamba serikali ina taarifa, Waziri Nahodha akakanusha madai ya Sitta – kwamba Wizara yake haina taarifa hizo. Nadhani Nahodha alikuwa sahihi kwa sababu maneno ya Sitta ni kwamba Serikali ina taarifa kwamba "
Mwakyembe amelishwa sumu."; hii ni tofauti na kusema "serikali ina taarifa kwamba ugonjwa/maradhi yanayomsumbua Dr. Mwakyembe yanatokana na kuwa in contact na sumu kwa namna moja au nyingine. Binafsi, sidhani ripoti kutoka India inasema
‘Mwakyembe amelishwa sumu", ingawa lazima inasema
ugonjwa wake umetokana na sumu.
· Lakini Sitta akapingana na Nahodha na kusema kwamba taarifa kuhusu
kulishwa sumu kwa Dr. Mwakyembe tayari zipo mikononi mwa polisi siku nyingi. Mpaka hapo, bado Dr. Mwakyembe alikuwa hajatoa tamko lake kuhusu
kulishwa kwake sumu.
· Pia ni muhimu kusema hapa kwamba – Waziri Mkuu Pinda na Katibu Mkuu Afya Blandina Nyoni, katika nyakati tofauti waliweka bayana kwamba serikali haiwezi kutoa maelezo kuhusu ugonjwa wa Dr. Mwakyembe kwani ni ‘unethical', hivyo ni wajibu wa mgonjwa mwenyewe. Bado Dr. Mwakyembe hakakaa kimya.
· Leo, DCI Manumba akatoa taarifa ambazo sote sasa tunazifahamu. Kwa kauli ya Manumba, upelelezi wa kipolisi ulilenga kuchunguza maneno kwamba
"amelishwa sumu", sio vinginevyo. Kama taarifa za uchunguzi wa madaktari wa India hazijatumia maneno
"Mwakyembe amelishwa sumu", Maelezo ya DCI Manumba yanasimama kuwa sahihi kwani kwa maana hii basi, walichofanya DCI ni kuchanganya taarifa walizopokea kutoka vyanzo tofauti juu ya tuhuma kwamba mwakyembe
"amelishwa sumu", pamoja na taarifa zilizopo Wizara ya Afya, kutoka India. Na huu ndio msingi wa Manumba kutamka kwamba, kazi ya Polisi ni kuchunguza tuhuma, sio maradhi, na yupo sahihi katika hilo.
My assumption:
DCI alikuwa na taarifa kutoka chanzo kingine zinazosema
"Mwakyembe amelishwa sumu", hivyo DCI alifanya uchunguzi kuhusu "kulishwa sumu", na sio vinginevyo. Na baada ya DCI kufanya uchunguzi uliotokana na ushirikiano wa karibu na Wizara ya Afya, DCI amebaini kwamba taarifa za
"kulishwa sumu", hazilingani na maneno yaliyopo kwenye faili lililopo Wizara ya Afya. Inawezekana kabisa Madaktari India wameweka wazi kwamba tatizo ni
uwepo wa sumu mwilini, lakini hawajatumia neno
"amelishwa sumu", na ndio maana alichokichunguza Manumba ni "TUHUMA" kwamba
"Mwakyembe amelishwa sumu", SIO taarifa au tuhuma kwamba
"Mwakyembe amenusishwa sumu, amepuliziwa sumu, kanawia maji au sabuni yenye sumu, amepata contact na sumu kutokana na mkono wa mtu n.k. Ni hali hii ndio inanipelekea kuamini kwamba Manumba amefanya kazi yake kwa usahihi kabisa, hivyo tusipoteze muda kuhoji kauli yake.
Ni dhahiri kwamba Dr. Mwakyembe ana tatizo lisilo la kawaida, na uwezekano mkubwa ni kwamba maradhi yale yanatokana na sumu. Natumia neno ‘uwezekano mkubwa', kwani bado Mwakyembe hajatueleza. Kwa mtazamo wangu, Sitta ni dhahiri hajazungumza bila ya ruksa ya Mwakyembe, lakini kama walitaka kufikisha ujumbe waliokusudia, basi Sitta angejaribu kuwa na busara kidogo na kukwepa kutoa tafsiri yake juu taarifa za madktari wa india, mfano kuepuka kutumia maneno
"amelishwa sumu", na badala yake kutumia maneno kama vile, Dr. Mwakyembe
"anasumbuliwa na maradhi yatokanayo na sumu kuingia mwilini"; au Maradhi ya Dr. Mwakyembe
"yanatokana na sumu na kuna mkono wa mtu katika hilo " au,
Dr. Mwakyembe alishatoa taarifa nyingi kwa polisi kwamba anatishiwa maisha yake lakini hakuna lililofanyika, na sasa imefikia hatua ya kuugua kutokana na sumu kumwingia mwilini…., hivyo ni wasaa sasa wa Serikali kutoa tamko lake kwa kufuatana na taarifa iliyo ipokea kutoka kwa madaktari wa India.
Maswali muhimu ya kujiuliza ni je:
1. Je, taarifa za uchunguzi wa madaktari kutoka India, ambazo zipo Wizara ya Afya, zimetumia neno
"amelishwa sumu" au zimetamka tu kwamba
"alipata contact na sumu?"
2. Je, alichokana Waziri Nahodha ni maneno ya Sitta kwamba
"Mwakyembe amelishwa sumu", kwa maana ya kwamba taarifa kutoka india hazijatumia maneno hayo ingawa zinaelezea maradhi yatokanayo na sumu kuingia mwilini?
3. Je, taarifa zilizopo Wizara ya Afya ni zile zile ambazo
Sitta anasema kwamba Polisi tayari wanazo? au Sitta na Mwakyembe walipeleka Polisi taarifa za ziada?
4. Je, katika uchunguzi wao, DCI (Polisi) wametumia taarifa zilizopo Wizara ya Afya ambazo hadi sasa hatujui kama zimetumia maneno
‘Mwakyembe amelishwa sumu? au Polisi (DCI) wametumia taarifa nyingine walizopokea zenye maneno
"Mwakyembe amelishwa sumu, na kisha kutumia tuhuma hizi kwenda Wizara ya Afya kuangalia faili kutoka India lina maelezo ya namna gani"?
5. Na je, kutokana na Wizara ya Afya kutoa ushirikiano na DCI, hivyo kupelekea taarifa ya DCI kwamba hakuna ushahidi Mwakyembe
"amelishwa sumu", je ni sahihi kutafsiri kwamba, matokeo ya uchunguzi wa DCI ambayo yamefanikiwa kutokana na ushirikiano wa Wizara ya Afya ambayo moja kwa moja ni Serikali Kuu, je ina maana kwamba sasa huu pia ndio msimamo/majibu/maelezo rasmi ya serikali kuhusu ugonjwa wa Dr. Mwakyembe? Tusisahau Waziri Mkuu alishasema serikali haitatoa maelezo kuhusu nini kinamsibu Dr. Mwakyembe kwani ni unethical, hiyo kazi ni ya mgonjwa mwenyewe.
Mwisho, Mwakyembe ni mwanasheria, hivyo kukaa kwake kimya ni sawa na ‘ukimuona kobe kainama, ujue anatunga sheria'. Hivyo tuwe na subira, akiwa tayari ameshazingatia legal implications, lazima atatamka tu sasa rasmi kama ‘mwathirika wa sumu'.
Vinginevyo, iwapo sasahivi Serikali inashindwa kutoa
taarifa kuhusu ugonjwa wa Dr. Mwakyembe, ikitokea bahati mbaya (mungu pishilia mbali) kwamba Dr. Mwakyembe anafariki, je, serikali itatoa
taarifa juu ya kufariki kwa kiongozi wake? Itasema marehemu alikuwa anaugua nini?