Jitihada zinaendelea kuhakikisha mawasiliano yanakuwepo kabla wajenzi wa barabara hawajaanza kazi ili tuwajulishe maeneo yenye miundombinu yetu kuepusha usumbufu usio wa lazimaInakuaje wajenzi wa barabara wanakata miundo mbinu yenu hamuwachukulii hatua kurejesha mapema iwezekanavyo na bado mnawapelekea madai ya malipo wateja wenu?
Pole sana za bingwa..tupatie maelezo yako binafsi yaan kituo ulichoomba,fomu namba pamoja na namba yako ya simu kwenye mesage nasi tutaufanyia kaziDawasa mnakera
Nimepeleka maombi ya kufungiwa maji
Mwezi wa pili huu
Kuja kufanyiwa tathimini tu nishakuja ofisini kwenu tabata mara 3
Ofisi za serikali urasimu mwingi...kila siku saundi tu...hapo ni utathimini tu....daah
Tumelipokea na tunaahidi kuwaelimisha zaidi ili tatizo lisijitokeze tenaWasoma meter na wakata maji wa DAWASA hivi wana kiwango gani cha elimu. Maana ni wabishi na wasiotaka kuelewa. Mfano wamekata maji na kutoa notification ambapo bill ya notification ilishalipwa. Sasa waje kurudisha maji, wamekuja wamerudisha maji sasa pale walipofunga kwa kukunja panavuja, wanakuambia funga na mpira wewe mteja wakati wao ndio wameharibu. Naomba kujua kiwango cha elimu cha watu hawa.
Tusaidie account namba yakoHabari, naona upo online. Mie ni mnifaika wa maji ya mkopo Kibamba. Toka nimefungiwa yale maji sijapewa invoice yoyote ya kuomyesha ni kiasi gani nadaiwa. Mmeanza kunitumia bili mwezi wa pili mwaka huu. Nahitaji kulipa ila niko nje ya mkoa, naomba muongozo
NILILIPA SHS.462,000 KWA AJILI YA KUUNGANISHIWA MAJI KIMARA BARUTI BAADA YA SURVEYOR KUFANYA SURVEY. IMEFUNGWA METER KWENYE LILE ENEO LAKINI TANGU ILIPOFUNGWA HALIJATOKA HATA TONE MOJA LA MAJI. MAJIRANI WOTE WANAPATA MAJI LAKINI KWANGU HAKUNA. NIMEAMBIWA ILE METER ILIFUNGWA KWENYE BOMBA LA MAJI LA ZAMANI AMBALO HALINA MAJI. NIMETUMA MALALAMIKO DAWASA NA HADI WIZARANI LAKINI HAKUNA ANAECHUKUA HATUA.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni Dawasa...Dawasco haipo tenaHivi hii kampuni jina lake hasa ni lipi kati ya haya; DAWASA au DAWASCO? which is which?
Mradi bado haujakamilika..tukimaliza tutaanza kuwafungia huduma ya majiNaomba kujua ni lini mtaanza kuwaunganishia maji wakazi wa Saranga Mwisho? Kwani tokea mmeweka mabomba na kuwajazisha form wananchi hakuna kinanchoiendelea mpaka sasa.
Utaratibu unaotakiwa kufuatwa ni mmiliki wa nyumba kuomba extra meter ambayo itajumuishwa kwenye mita kuu yake na ndio atakuwa anapokea bili zote extra alizoomba kupitia bili kuu yakeHIVI DAWASCO MTATUTATULIA LINI TATIZO LA MITA.TUNAKUWA WA WAPANGAJI WENGI NA TUNAHITAJI METER KWENYE ENEO MOJA.MFANO UNA JENGO LINA APARTMENT 3 KILA MTU ALIPE KADRI YA MATUMIZI YAKE
Nadhan mgeacha DAWASCO Mkuu mana wao kidogo walikuwa na unafuu kuliko nyinyi.....Nimelipa bill ya kufungiwa maji mwezi Wa NNE sasa sjaona cha suvyer wala kishoka..Nini hili mnatufanyia wateja wenu?Ni Dawasa...Dawasco haipo tena
Sawa, asante. Sasa fanyeni utaratibu wa kubadilisha nyaraka zenu zisome DAWASA badala ya DAWASCO.Ni Dawasa...Dawasco haipo tena
Mkuu hata mimi nikienda kudai naambiwa bado hawajafungulia account ya bomba langu sasa sielewiJambo kubwa nina ugomvi na nyie hasa kwenye malipo ya bill zangu hamjaingiza kwenye mfumo mpaka mnaniletea madeni niliyolipa tayari ila mmekataa kukubali kuwa nililipa ingawa receipt zote zipo.
Afrika bado naamini mabeberu yanapaswa kurudi kutupa despline ili tuendane nao.Mkuu hata mimi nikienda kudai naambiwa bado hawajafungulia account ya bomba langu sasa sielewi
DAWASA shida ni nini mbona MAJI hatupati karibia wiki la pili hili,maeneo ya KIMARA.Hakuna TAARIFA yoyote ya kupasuka kwa BOMBA wala MATENGENEZO kwa umma.
Je? mnataka wakazi wa DAR tuanze kutumia maji ya mitaroni na hali ya KIPINDUPINDU ndo hii,je mkilaumiwa kwa kuchochoea matumizi ya maji yasiyo salama ilihali bili zinalipwa mtakuwa na cha kujitetea???.