Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

Ndio ukweli unaojengewa hoja dhaifu kabisa. Hakuna sababu za nchi hii kuwa na kaimu kwa muda wote

Othaman alitoa notisi kwa muda mrefu, hakuamka asubuhi na kusema anastaafu
Vetting ilitakiwa ifanyike, Rais ana vyombo vyote ambavyo hata siku moja vingeweza kumpa habari zote anazotaka kupata Jaji mkuu

Kabudi kasema, Nyerere alitoa sababu na sote tunajua. Mwaka 1962 hatukuwa na Madaktari (MD) zaidi ya 10, wapi tungepata Jaji mkuu?

Hali si hiyo, sasa hivi wakurugenzi wengine wana PhD. Kuna majaji wenye uzoefu.
Tunaweza kuomba Kenya, Uganda n.k. Kwanini tuwe na kaimu muda wote huo?

Kinachofanyika ni kuondoa nguvu ya Jaji mkuu na kumweka kaimu katika level sawa na mkurugenzi wa TRA , Bandari au kwingine kwa kujua Jaji mkuu mchakato wa kumuondoa si rahisi na utazua maswali mengine ndani na nje ya nchi.

Sasa MM anaposema ni pres prerogative, nakubaliana naye, lakini tukubali prerogative hata pale inapotumika kinyume na inavyokusudiwa?

Turuhusu mambo yaende ende kwa kutumia neno prerogative?
precisely na huu ndio msingi wangu katika post #2
 
Hivi kaimu Jaji Mkuu akisafiri nje ya nchi watateuza kaimu mwingine kukaimu nafasi ya kaimu Jaji Mkuu?

Halafu kuna nyakati huwa tunasahahu kuwa hawa kina Lissu ni wawakilishi tu. Sitashangaa kusikia kuwa hoja ya Lissu kuhusu CJ na katiba inatokana na watu wazito tu huko kwenye judiciary! Sio rahisi kwa majaji au hata wabunge wa CCM kuraise concerns zao moja kwa moja hasa kama hizo ambazo zinamuhusu bosi wao na kwa hivyo the logical and easier route ni "kuwatumia" wapinzani.
 
Kuna mtu ka cooment kuwa kaimu jaji anaweza kuwa legevu kwa aliemteua kwa kuwa anakosa kinga za jai mkuu kamili!
Hapana tupige tu kelele, maana tukikaa kimya na yenyewe ni uoga au hofu.
 
una hoja zenye mashiko kuliko za mzee mwanakijiji. upo sahihi comrade tumezungukwa na wasaliti wengi na kuna uwezekano hata huyu mzee tuliempenda sana kwa tafakuri zake kipindi cha JK nae anasubiri kupewa kitengo aufyate kama akina kitila na polepole.

Shame on them
Sio hivyo tu,inapotungwa katiba hatuangalii mazingira ya sasa tu huwa inaangaliwa hata nini kinaweza kutokea baadae pia ili kuzuia watu kujifanyia mambo kwa utashi wao,fikiria sasa hivi kuna katiba na sheria lakini watu wanazikiuka waziwazi je ingekuwaje kungekuwa hakuna kabisa hizo sheria na katiba?
 
Sio hivyo tu,inapotungwa katiba hatuangalii mazingira ya sasa tu huwa inaangaliwa hata nini kinaweza kutokea baadae pia ili kuzuia watu kujifanyia mambo kwa utashi wao,fikiria sasa hivi kuna katiba na sheria lakini watu wanazikiuka waziwazi je ingekuwaje kungekuwa hakuna kabisa hizo sheria na katiba?
kabudi ni mchumia tumbo njaa yake ndio inampelekea atumie uzoefu wake wa kufundisha kutuhadaa na kutekeleza maagizo ya bosi wake
 
Practice ni mtu kuamua hajaamua amewaacha vidagaa vijimwaemwae ili vijulikane
Sio kweli,huo ni mwendelezo uleule ambao unakuta mwalimu aliyebobea kwenye biashara/ujasiliamali hajawahi hata kumiliki genge la nyanya.
 
Prof.. Kabudi, prof maji marefu and prof jay have the same level of thinking capacity. Kibajaji ndiyo level hiyo hiyo.
 
Mkuu sana mleta mada, kwa aina ya wabunge wetu tulionao darasa la prof kabudi lilikuwa ni lazima......tena na viboko juu!!.
Nna hakika hata akitoa quiz kulingana na darasa lile wafuatao watataga; msukuma, kibajaj, maji marefu, jah people, lema, sugu nk
Kubenea tu atafaulu lile somo.
 
Kama lissu ndio alichoongea na kabudi alichojibu lissu yupo makini na kabudi ni mweupe kabisa au anajitoa akili zile story hazina maana yeyote alizotoa kinachotakiwa ni uteuzi Wa jaji mkuu tu ni aibu Sana kukaa na kaimu asiye na nguvu na anadhalilisha Waislam

kudos!
 
kabudi anadhani bado yupo theatre 1 au yombo 4 au nkrumah hall bado ana tongotongo za mjengoni,mle hakuna CW
 
Kwa nini?
Kuingia kwao madarakani hakufanani.
Jaji mkuu huweza kufanya maamuzi ili amfurahishe mteuzi wake, lkn kaimu jaji mkuu anaweza kujipendekeza zaidi kwa mteuzi ili ikiwezekana awe jaji mkuu. Hii ni hulka ya kibinadamu.

Kuhusu Makamu, sioni shida ya kujipendekeza kwa Rais. Makamu hateuliwi na Rais. Rais hayupo ofisini lkn anafahamika kuwa ni nani. Makamu anajua kuwa hata afanyaje, bila uchaguzi na kupata kura za kutosha hawezi kupandishwa na kuwa Rais.

Ndo maana sioni usambamba wa mfano huu wa Rais na Makamu wa Rais na Utendaji wa kaimu jaji mkuu na jaji mkuu (wateule wa Rais) Ingelikuwa Jaji mkuu alishateuliwa ila hayupo ofisini kwa sababu fulani ingeeleweka, lkn hii ya kuwa na kaimu jaji mkuu ambaye anaweza kuwa na matumaini ya kupandishwa ngazi na kuwa jaji mkuu, inaweza kuathiri utendaji wake hata bila kunong'onezwa na mteuzi wake.
 
Tundu lisu amekutana na gwiji. Hata mmutee vipi anapwaya alikuwa anapewa kiki na wasiojua sheria. Sasa kaja mwenyewe. Ila nilikuwa nasikia siku nyingi sana kuwa tundu lieu hajui sheria Bali ni mwanaharakati tu Wa sheria na mpayukaji pasipo kujua lolote ndo mana kabudi kasema mwanasheria yeyote anapaswa kuwa na busara siyo kila kitu kinatatuliwa na sheria bali jamii nabethics sake.
Lisu anacheza na uzuzu wa watz kwamba hatujui sheria na haki zetu ila kimsingi huwezi kumwita mwanasheria bingwa kwakuwa hata sio mwepesi wa kusite vifungu wala katiba .. anatumia personal instincts to justify mambo.. plus anafanya siasa/mwanaharakati zaidi kuliko sheria.
Najua kuna wanasheria kibao TZ Lisu hawafikii ila sio watu wa kiki/media na sio politicians.. kuna vipanga wa Havard hapo TZ kibao.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Hili si jambo sahihi; wabunge kama wanaona Rais anatumia muda mrefu kujaza nafasi ya jaji mkuu wana uwezo wa kubadilisha sharia na hata Katiba chini ya Ibara ya 100 ya Katiba yetu.
Unadhani hoja hii ikipelekwa Bungeni na Tundu Lissu ama mbunge mwingine wa upinzani wabunge wa CCM wataiunga mkono?
 
Lisu anacheza na uzuzu wa watz kwamba hatujui sheria na haki zetu ila kimsingi huwezi kumwita mwanasheria bingwa kwakuwa hata sio mwepesi wa kusite vifungu wala katiba .. anatumia personal instincts to justify mambo.. plus anafanya siasa/mwanaharakati zaidi kuliko sheria.
Najua kuna wanasheria kibao TZ Lisu hawafikii ila sio watu wa kiki/media na sio politicians.. kuna vipanga wa Havard hapo TZ kibao.
Halafu hao hao "vipanga" bado wakamchagua awe Rais wao (TLS)?
 
Hivi kaimu Jaji Mkuu akisafiri nje ya nchi watateuza kaimu mwingine kukaimu nafasi ya kaimu Jaji Mkuu?

Halafu kuna nyakati huwa tunasahahu kuwa hawa kina Lissu ni wawakilishi tu. Sitashangaa kusikia kuwa hoja ya Lissu kuhusu CJ na katiba inatokana na watu wazito tu huko kwenye judiciary! Sio rahisi kwa majaji au hata wabunge wa CCM kuraise concerns zao moja kwa moja hasa kama hizo ambazo zinamuhusu bosi wao na kwa hivyo the logical and easier route ni "kuwatumia" wapinzani.
hoja za lissu huwa hawawezi kuzijibu..huwa wanaishia kushambulia personality yake
 
Halafu hao hao "vipanga" bado wakamchagua awe Rais wao (TLS)?
Mkuu sio wote wako busy na uongozi.. kuna wengine sisi majiniaz tunapenda siti za nyuma "chilling"...joking. sio kila kipanga anataka kuwa kiongozi.. plus vipanga wako busy na mambo makubwa sana hawana hata muda wa kupoteza kuwa kiongozi..
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Back
Top Bottom