Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

mleta bandiko nimekuelewa sana na usemacho uko sahihi 100% (kwa maandiko ya katiba ila kiuhalisia hauko sawa100%)

unauliza kwamba kukaimu ujaji mkuu hakumfanyi aliyekaimishwa kutofanya kazi kwa kuhofia mamlaka iliyo mpa nafasi (huu ni uongo wafanyakazi karibu wote tanzania ni wanafiki hata huyu aliye kaimishwa hana nguvu/uwezo wa kuipinga mamlaka)

hakuna mtanzania ambaye anaweza simamia ukweli unao mkwanza mteule wake hili lipo wazi

kutoidhinishwa kwa jamaa ni kweli kuna athari za kiutendaji kutokana na tabia za mtanzania kumnyenyekea/kupindisha ukweli ili amfurahishe aliye mpa nafasi.
 
"Mzee Mwanakijiji, post: 20873879, member: 118"]Nimesikiliza kwa makini kile kinachoitwa "darasa" la Prof. Kabudi. Inasikitisha kuna watu wanasifia ametoa "darasa"
Ni kweli inasikitisha kwasababu darasa alilotoa halikujibu hoja mezani
Kuna hoja ya kuuliza swali; kwamba - kwanini Rais amemteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu kwa muda wote huu.
Swali ni kwamba, kwanini nafasi imekaimiwa kwa muda mrefu kiasi hicho? Jaji Othman alitoa notisi akijua uzito wa nafasi hiyo na vetting inayotakiwa. Hakuamka asubuhi na kufikisha 24hrs notice!!!Swali lina mantiki na lijibiwe kwa mantiki.
Swali ambalo halipaswi kuulizwa na tulilikataa wakati ule ni kuhusu mamlaka ya Rais kumteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu. Hili liko ndani ya mamlaka ya Rais (Presidential prerogative).
Sidhani kama kuna aliyehoji hili. Hapa tuwe wakweli
Wabunge kama wanaona Rais anatumia muda mrefu kjujaza nafasi ya Urais wana uwezo wa kubadilisha sharia na hata Katiba chini ya Ibara ya 100 ya Katiba yetu.
Mfumo mbaya umetufikisha hapa, hatuhitaji katiba viraka.Unaposema Wabunge na wa CCM ambao kila jambo ni sawa wapo katika kundi unaloongelea? Angalia 'odds' ya hoja yako kuwa ya kweli
Kama wanataka nafasi ya Jaji Mkuu isikaimiwe indefinitely (kama hoja ya Lissu ilivyoashiria) namna pekee ni kubadilisha Katiba au sheria ili kuweka kikomo kama ilivyo katika baadhi ya nafasi za utumishi wa umma
Hatuwezi kuweka viraka kila siku , kwanini tusikubali kuandika upya katiba ili mfumo uendane na wakati tukishirikisha mawazo kama ya hili. Hapa unaunga mkono hoja ya mfumo
Kama kwa mfano Rais angejaza cheo cha Ujaji siku moja tu baada ya Jaji Othman kustaafu wapo ambao labda wangeweza kuja na hoja ya kwanini amejaza nafasi haraka bila kuonesha tafakari sana au klutumia muda kufanya utafiti wa kutosha!
Hapana, angehoji mjinga tu. Urais ni taasisi, uteuzi una vetting, kulikuwa na notisi ya kustaafu ambayo kwa muda mrefu. Nani angehoji hilo? Mbona hawahoji teuzi za nafasi nyingine nyeti?
Jibu,Rais ana vyombo vya kazi si lazima public ijue. Asingehoji mtu timamu
Lakini pia kuna swali ambalo inabidi liulizwe kwa wale wanaolalamikia - kwa Rais kuweka Kaimu Jaji Mkuu ni shughuli gani ya Mahakama Kuu ambayo haiwezi kufanyika sasa hivi kwa vile kuna kaimu Jaji Mkuu au ni kitu gani hakifanyiki katika mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ambacho kinapaswa kufanywa na jaji mkuu peke yake. Hili ndilo linaweza kuwa hoja ya kwanini inahitajika Jaji Mkuu na siyo Kaimu Jaji Mkuu?
Hapa unafanya 'adulteration' ya nafasi ya Jaji mkuu

Prof Kabudi kasema hakuna hata dakika nchi inaweza kukaa bila Jaji mkuu. Hakumaanisha anafanya kazi za mhakama zote, alimaniisha ni sehemu muhimu ya maamuzi ya mahakama

Pili, unajichanganya kihoja. Kama hakuna kinachosimama, wapo wanaouliza kwanini Rais asimteue tu mtu bila kukaimu ikiwa hana impact unayosema?

Jaji mkuu anahitajika kwasababu alizosema Kabudi
Kumbuka huu ni mhimili mkubwa, hauwezi kuendeshwa kama TRA au Bandari
Lakini kung'ang'ania kitu ambacho wote wanajua hakipo - kwamba Rais hajavunja sheria wala Katiba, na kuwa hakuna kikomo cha muda kilichowekwa kwa hoja ya kuwa ni mazoea mapya haitoshi kuwa hoja.
Sawa kabisa, hakuna sheria iliyovunjwa.

Kimaadili hilo linatia shaka sana. Rais ana public trust, anaweza kuamuru nchi iingie vitani kisha kulitaarifu Bunge, anaweza kuvunja idara, mamlaka za umma n.k. bila kuhojiwa.

Ana nguvu za kisheria 'Exec order' na inakuwa sheria wakati huo.

Katika kufanya hivyo haipaswi kufanya kitu kinachoweza kuleta hisia za ' abuse of power''
Abuse of power si lazima iwe kuvunja sheria, ni misconduct kwa kutumia nafasi hiyo

Kabudi alieleza kwanini Nyerere alichukua muda kupata Jaji mkuu.
Tungeelewa Kabudi angeeleza kwanini Rais anachukua muda kupata Jaji mkuu.

Hakuna anayehoji kwanini hajamthibitisha, wanahoji sababu.

Hizi zipo katika uwezo wao kwasababu katiba inasema 'mamlaka yanatoka kwa wananchi'

Wananchi wanasababu za kuhoji ili kumnusuru Rais na 'abuse of Power' Si lazima Rais afanye wanavyotaka, ni muhimu kwake kuhakikisha anachokifanya kina public trust
Lakini wapo ambao wanasema kuwa kwa kutomthibitisha Kaimu Jaji basi Kaimu Jaji anaweza asifanye anayotakiwa kufanya kwa kuhofia kuiudhi mamlaka ya uteuzi. hilo si wazo sahihi katika utawala. Unapokaimu nafasi unakuwa na madara yote ambayo unayo kwa mujibu wa kukaimu kwako.
Je, hii si genuine concern! Hili linaonyesha tayari kuwana mistrust, kazi ya Kabudi ilikuwa kuondoa mistrust inayojengekea si kutueleza ukubwa wa mamlaka yake.

Yes tunajua anayo, lakini je, yanatumika bila kuwa na shaka za 'abuse'.

Mkuu, kama hakuna sababu za kwanini Jaji mkuu awe kaimu, hoja ya kwamba amewekwa 'njia panda' haiwezi kupingika kwa hoja. Umejaribu lakini hukufanikiwa kunishawishi.
Mfano uliotoa haulingani na hali ilivyo.

Kumpa ukaimu ni kumuondolea kinga ya 'kutoondelewa' kiholela.

Kwa maana kuwa ameshikizwa na si kishikizo halisi.
Hili ndilo Kabudi alipaswa kulitolea ufafanuzi. Hakufanya kama ambavyo hujafanya.
Presidential prerogatives..
Hili litumike kiholela. Prerogative ina misingi yake na sababu za kueleweka. Nyerere hakuwa na wasomi, tunasababu gani wakati huu?
 
Tuanzie hapa: Kazi za Kaimu Jaji ni zipi na za Jaji Mkuu ni zipi ambazo zinaingilia utendaji wa aliemteua?

..Mchakato wa KUMTUMBUA Kaimu Jaji Mkuu ni sawa na ule uliotumika kumtumbua Mwele Malecela.

..Jaji Mkuu kamili huwezi kumuondoa bila kushirikisha jopo la majaji wa jumuiya ya madola.

..hapo ni wazi kabisa dikteta uchwara atapendelea mhimili wa mahakama uongozwe na mtu anayeweza kumtumbua wakati wowote ule.
 
Mimi niliona pumba,baada ya kusema uteuzi wa rais unaimarisha independence ya utendaji na objectivity.Yani mtu akiteuliwa na Rais anakuwa independent na objective.Baada ya hoja hiyo nikamuona naye ni PROPESA tu.
 
mkuu umemsoma Lissu au umeandika tu?

YA KAIMU JAJI MKUU

Mheshimiwa Spika,
Mahakama ya Tanzania haina kiongozi wake kamili, yaani Jaji Mkuu. Hii ni kwa sababu, tangu Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman astaafu tarehe Mosi Januari ya mwaka huu, Rais John Pombe Magufuli hajateua Jaji Mkuu mpya kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mkuu Chande Othman. Badala yake, Rais Magufuli amemteua Jaji wa Rufaa Prof. Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu.

Mheshimiwa Spika,
Ibara ya 118(4) ya Katiba yetu, Rais anaruhusiwa kuteua Kaimu JAji Mkuu iwapo itatokea kiti cha Jaji Mkuu kitakuwa wazi; au Jaji Mkuu hayupo Tanzania; na au Jaji Mkuu atashindwa kutekeleza kazi yake kwa sababu yoyote, na Rais ataona kuwa kwa muda wa tukio lolote kati ya hayo matatu inafaa kumteua Kaimu Jaji Mkuu. Kaimu Jaji Mkuu aliyeteuliwa kwa utaratibu huu “... atatekeleza kazi za Jaji Mkuu mpaka atakapoteuliwa Jaji Mkuu mwingine....”

Mheshimiwa Spika,
Pamoja na kuwapo kwa ibara ya 118(4), Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu inaamini kwamba Rais Magufuli anavunja Katiba ya nchi yetu kwa kushindwa kuteua Jaji Mkuu kamili takriban miezi mitano tangu kustaafu kwa Jaji Mkuu Chande Othman. Hii ni kwa sababu, ibara ya 118(4) haikutungwa kwa lengo la kumwezesha Rais kuteua Kaimu Jaji Mkuu bila kikomo cha muda.

Kama ilivyo kwa sheria zote, ibara ya 118(4) ina sababu yake maalum. Ibara hiyo imewekwa kwa makusudi ya kuhakikisha kwamba kwa muda wote kunakuwa na kiongozi wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania pamoja na kiongozi wa Mahakama ya Tanzania, wakati Jaji Mkuu kamili anasubiriwa kuteuliwa. Kaimu Jaji Mkuu ni sawa ni kile kinachoitwa na wanasheria ‘interlocutory position.’ Kaimu Jaji Mkuu ni nafasi ya muda inayoshikiliwa na mtu mwenye sifa za kuwa Jaji Mkuu kabla nafasi hiyo haijajazwa na Jaji Mkuu kamili.

Swali halali linahitaji majibu ni, je, Kaimu Jaji Mkuu anastahili kuwapo madarakani kwa muda gani? Hili ni suala la tafsiri ya Katiba linalohitaji kujibiwa na Mahakama. Kwa maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, miezi mitano ni muda mrefu mno wa kuwa na Kaimu Jaji Mkuu.

Mheshimiwa Spika,
Bunge lako tukufu, kama mmojawapo wa mihimili mikuu ya dola ya Tanzania, lina kiongozi wake mkuu muda wote: Spika au Naibu Spika. Serikali, kama mhimili mwingine mkuu, ina kiongozi wake mkuu muda wote: Rais au Makamu wa Rais. Kwa Mahakama ya Tanzania, mhimili mkuu wa tatu wa dola ya Tanzania, kutokuwa na kiongozi wake kamili miezi mitano baada ya kustaafu kwa Jaji Mkuu Chande Othman, kunatoa taswira potofu kwamba Mahakama ina hadhi hafifu au ya chini ikilinganishwa na mihimili mingine mikuu ya dola ya Tanzania.

Kitendo hiki vile vile kinatoa taswira potofu kwamba pengine Kaimu Jaji Mkuu wa sasa hatoshelezi nafasi hiyo; au kwamba miongoni mwa Majaji wote wa Rufaa au wa Mahakama Kuu ya Tanzania au mawakili na wanasheria wengine wa nchi hii pamoja na wale wa nchi za Jumuia ya Madola hakuna hata mmoja wao mwenye uwezo au sifa za kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu inamtaka Mheshimiwa Waziri amshauri Rais Magufuli, kwa heshima zote anazostahili, amthibitishe Kaimu Jaji Mkuu Prof. Juma katika nafasi hiyo au, vinginevyo, ateue mwanasheria mwingine anayemwona ana sifa za kuwa Jaji Mkuu kamili wa Tanzania. Hali ilivyo hivi sasa inawatia aibu wanasheria wote wa Tanzania na inaitia aibu nchi yetu katika jumuia ya kimataifa.
Kama lissu ndio alichoongea na kabudi alichojibu lissu yupo makini na kabudi ni mweupe kabisa au anajitoa akili zile story hazina maana yeyote alizotoa kinachotakiwa ni uteuzi Wa jaji mkuu tu ni aibu Sana kukaa na kaimu asiye na nguvu na anadhalilisha Waislam
 
How? litakuwa na madhara gani? Na kama sheria au Katiba haijaweka kikomo hilo ni tatizo la nani hasa? Kwanini LIssu asije na hoja ya dharura ya kutaka mabadiliko ya sheria au kushawishi wabunge angalau 2/3 yao wafanye mabadiliko ya Katiba?
Mwanakijiji wewe ni mzoefu wa maswala ya bunge unajua hilo unalosema akilifanya Lissu halitafanikiwa kama alishindwa January Makamba wa CCM hoja yake ya kubadili sheria ili kudhibiti wenye nyumba kujipangia kodi za nyumba kiholela unadhani Lissu atakubaliwa hiyo hoja? Na hapa siyo move ya kubadili sheria bali ni katiba maana Acting chief justice amewekwa kikatiba ibara ya 118 ya URT constitution, unajua mziki wa nchi hii kubadili katiba tena kwa hoja binafsi ya mpinzani kama Lissu tena jambo lenye manufaa kwa CCM? Anyway ni wazo zuri kulijaribu ukizingatia yeye ni Rais wa TLS japo matokeo yake tunajua kabla mechi haijaanza
 
Inategemea, kwangu mimi lilikuwa ni muhimu kwani nimejifunza mengi ambayo sikuyafahamu, siyo tu kuhusu mambo ya uteuzi wa Jaji bali kwa mfano sikujua kwamba Raisi wa AK hachaguliwi na Wananchi kama wetu bali huchaguliwa na Bunge, na kwamba Chama kiko juu ya raisi wa AK na kinaweza kumuondoa madarakani kama Mbeki alivyoondolewa, hivyo nimejua tofauti ya Raisi wa AK na wetu na zipi limitations za mifumo yote miwili n.k.

Hivyo leo hii siwezi kuanza kumlinganisha Raisi wa JMTZ na Raisi wa AK kwa mfano kwani najua ni vyeo viwili vinavyofanana lkn ni tofauti!
AK unamaanisha nn mkuu?
 
..Mchakato wa KUMTUMBUA Kaimu Jaji Mkuu ni sawa na ule uliotumika kumtumbua Mwele Malecela.

..Jaji Mkuu kamili huwezi kumuondoa bila kushirikisha jopo la majaji wa jumuiya ya madola.

..hapo ni wazi kabisa dikteta uchwara atapendelea mhimili wa mahakama uongozwe na mtu anayeweza kumtumbua wakati wowote ule.
Ndio ukweli unaojengewa hoja dhaifu kabisa. Hakuna sababu za nchi hii kuwa na kaimu kwa muda wote

Othman alitoa notisi kwa muda mrefu, hakuamka asubuhi na kusema anastaafu

Vetting ilitakiwa ifanyike, Rais ana vyombo vyote ambavyo hata kwa siku moja vingeweza kumpa habari zote anazotaka ili kupata Jaji mkuu

Kabudi kasema, Nyerere alitoa sababu na sote tunajua.
Mwaka 1962 hatukuwa na Madaktari (MD) zaidi ya 10, wapi tungepata Jaji mkuu?

Hali si hiyo, sasa hivi wakurugenzi wengine wana PhD. Kuna majaji wenye uzoefu.
Tunaweza kuomba Kenya, Uganda n.k. Kwanini tuwe na kaimu muda wote huo?

Kinachofanyika ni kuondoa nguvu ya Jaji mkuu na kumweka kaimu katika level sawa na mkurugenzi wa TRA , Bandari au kwingine kwa kujua Jaji mkuu mchakato wa kumuondoa si rahisi na utazua maswali mengine ndani na nje ya nchi.

Sasa MM anaposema ni pres prerogative, nakubaliana naye, lakini tukubali prerogative hata pale inapotumika kinyume na inavyokusudiwa?

Turuhusu mambo yaende ende kwa kutumia neno prerogative?
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji, kwenye issue ya kukaimu, sorry you've missed the point.

Sheria yoyote inapotungwa na Bunge inanakuwa na madhumuni fulani. Lengo la kifungu cha mamlaka ya rais kuteua Kaimu Jaji kilidhamiria Kaimu Jaji Mkuu atateuliwa pale tuu Jaji Mkuu yupo lakini yuko nje ya nchi, ama ana maradhi yaliyopelekea kushindwa kutimiza majukumu yake, hivyo anateuliwa Kaimu as a temporary measures, Jaji Mkuu akirudi au akipona anaendelea na majukumu yake.

Lakini Jaji Mkuu anapomaliza muda wake wa utumishi wa umma, 6 months before notification hutumwa na rais kupelekewa majina matatu to choose from.

Huu Uteuzi wa Prof. Juma kama Kaimu Jaji Mkuu wakati nafasi ya Jaji Mkuu iko wazi permanently is not right!. It is as if Dr.Juma is not trusted hivyo yuko under probation kama atafiti ndipo ateuliwe na asipofiti anateuliwa mtu mwingine!. Hii ni very demoralising na Dr.Juma hawezi kuwa na confidence ya ku exercise all his powers kwa sababu kuna vitu Kaimu Jaji hawezi kufanya ikiwemo kukaimu nafasi ya Urais!.

Ukaimu huu sio sawa na ule Ukaimu wa mtu kukaimu nafasi fulani temporary mwenyewe akirudi unapisha. Huku ni kukaimu wakati nafasi haina mwenyewe!.

Kingine ambacho Mwanakijiji hakijui, hajui kuwa kaimu hata kaimu rais, hawezi kusaini amri yeyote ambaye inapaswa kusainiwa na rais ikiwemo kusaini sheria, kutangaza hali ya hatari, kuteua wala Kaimu rais haruhusiwi kusaini Presidential Preventative Detention Order!.

Enzi za Nyerere kuna siku Ali Hassan Mwinyi alikaimu na akasaini hati ya kizuizini, aliyetiwa kizuizini alishitaki Mahakama Kuu, amri ile ikapigwa chini kwa sababu Kaimu rais ni kaimu na sio rais, ukaimu unaishia kwenye kutoa maagizo na sio kusaini jambo lolote linalohitaji saini ya rais!.

Mfano Bunge likitaka kufanya impeachment process Kaimu Jaji Mkuu hawezi kwa sababu aliielezwa kwenye sheria ni Jaji Mkuu.

Taratibu ni kama sheria. Kama hutajawahi kuwa na Kaimu Jaji Mkuu muda wote huu, why now?!.

Paskali
Mkuu Paskali nieleweshe kidogo. Kwenye maelezo yako umesema vitu ambavyo kaimu jaji mkuu hawezi kufanya ni kukaimu nafasi ya urais kama ni hivyo je kaimu jaji mkuu anaweza kumwapisha Rais?
 
Mh.Paramagamba "he is above sixty" aliomba aheshimiwe kwa utu uzima wake.Acha niendelee kumuheshimu kama alivyoomba ila kimsingi sijaona kile kinachoitwa "darasa", aliongea vitu vya kawaida sana na hakuna hoja yoyote ya TL aliyoijibu.

Tundu Lissu alitoa ushauri tu badala yake Mh.Kabudi badala ya kujadili hoja za Lissu,akaamua " kuhawilisha maarifa yake ya ualimu"na kuyaleta bungeni.Msome tena Mh.Lissu kisha niambie kama aliyoyasema kabudi yalikuwa yanajibu hoja aliyoiuliza Lissu.

****************************************

YA KAIMU JAJI MKUU

Mheshimiwa Spika,
Mahakama ya Tanzania haina kiongozi wake kamili, yaani Jaji Mkuu. Hii ni kwasababu, tangu Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman astaafu tarehe Mosi Januari yamwaka huu, Rais John Pombe Magufulihajateua Jaji Mkuu mpya kuchukua nafasiiliyoachwa wazi na Jaji Mkuu ChandeOthman. Badala yake, Rais Magufuli amemteua Jaji wa Rufaa Prof. Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu.

Mheshimiwa Spika,
Ibara ya 118(4) ya Katiba yetu, Raisanaruhusiwa kuteua Kaimu JAji Mkuuiwapo itatokea kiti cha Jaji Mkuu kitakuwawazi; au Jaji Mkuu hayupo Tanzania; na auJaji Mkuu atashindwa kutekeleza kaziyake kwa sababu yoyote, na Rais ataonakuwa kwa muda wa tukio lolote kati ya hayo matatu inafaa kumteua Kaimu Jaji Mkuu. Kaimu Jaji Mkuu aliyeteuliwa kwa utaratibu huu “... atatekeleza kazi za Jaji Mkuu mpaka atakapoteuliwa Jaji Mkuu mwingine....”

Mheshimiwa Spika,
Pamoja na kuwapo kwa ibara ya 118(4),Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lakotukufu inaamini kwamba Rais Magufulianavunja Katiba ya nchi yetu kwakushindwa kuteua Jaji Mkuu kamili takriban miezi mitano tangu kustaafu kwa Jaji Mkuu Chande Othman. Hii ni kwa sababu, ibara ya 118(4) haikutungwa kwa lengo la kumwezesha Rais kuteua Kaimu Jaji Mkuu bila kikomo cha muda.

Kama ilivyo kwa sheria zote, ibara ya 118(4) ina sababu yake maalum. Ibara hiyo imewekwa kwa makusudi ya kuhakikisha kwamba kwa muda wote kunakuwa nakiongozi wa Mahakama ya Rufani yaTanzania pamoja na kiongozi waMahakama ya Tanzania, wakati Jaji Mkuu kamili anasubiriwa kuteuliwa. Kaimu Jaji Mkuu ni sawa ni kile kinachoitwa na wanasheria ‘interlocutory position.’ Kaimu Jaji Mkuu ni nafasi ya muda inayoshikiliwa na mtu mwenye sifa za kuwa Jaji Mkuu kabla nafasi hiyo haijajazwa na Jaji Mkuu kamili.

Swali halali linahitaji majibu ni, je, Kaimu Jaji Mkuu anastahili kuwapo madarakani kwa muda gani? Hili ni suala la tafsiri ya Katiba linalohitaji kujibiwa na Mahakama. Kwa maoni ya Kambi Rasmi ya UpinzaniBungeni, miezi mitano ni muda mrefu mnowa kuwa na Kaimu Jaji Mkuu.

Mheshimiwa Spika,
Bunge lako tukufu, kama mmojawapo wa mihimili mikuu ya dola ya Tanzania, lina kiongozi wake mkuu muda wote: Spika au Naibu Spika. Serikali, kama mhimili mwingine mkuu, ina kiongozi wake mkuu muda wote: Rais au Makamu wa Rais. Kwa Mahakama ya Tanzania, mhimili mkuu wa tatu wa dola ya Tanzania, kutokuwa nakiongozi wake kamili miezi mitano baadaya kustaafu kwa Jaji Mkuu ChandeOthman, kunatoa taswira potofu kwamba Mahakama ina hadhi hafifu au ya chini ikilinganishwa na mihimili mingine mikuu ya dola ya Tanzania.

Kitendo hiki vile vile kinatoa taswira potofu kwamba pengine Kaimu Jaji Mkuu wa sasa hatoshelezi nafasi hiyo; au kwamba miongoni mwa Majaji wote wa Rufaa au wa Mahakama Kuu ya Tanzania au mawakili na wanasheria wengine wa nchi hii pamoja na wale wa nchi za Jumuia ya Madola hakuna hata mmoja wao mwenye uwezo au sifa za kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu inamtaka Mheshimiwa Waziri amshauri Rais Magufuli, kwa heshima zote anazostahili, amthibitishe Kaimu Jaji Mkuu Prof. Juma katika nafasi hiyo au, vinginevyo, ateue mwanasheria mwingine anayemwona ana sifa za kuwa Jaji Mkuu kamili wa Tanzania. Hali ilivyo hivi sasa inawatia aibu wanasheria wote wa Tanzania na inaitia aibu nchi yetu katika jumuia ya kimataifa.
Kabudi anajulikana kwa majigambo kiukweli anatakiwa aache kulichukulia bunge kama darasa la sheria tena darasa la first year maana alichokifanya ni kutoa history ya constitutional dvt of Tanzania ambayo vyuoni hufundishwa semester ya kwanza ya mwaka wa kwanza kwenye constitutional and legal system of East Africa Law, sasa sijui kesho atakuja na somo gani au gentile constitution?
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji, kwenye issue ya kukaimu, sorry you've missed the point.

Sheria yoyote inapotungwa na Bunge inanakuwa na madhumuni fulani. Lengo la kifungu cha mamlaka ya rais kuteua Kaimu Jaji kilidhamiria Kaimu Jaji Mkuu atateuliwa pale tuu Jaji Mkuu yupo lakini yuko nje ya nchi, ama ana maradhi yaliyopelekea kushindwa kutimiza majukumu yake, hivyo anateuliwa Kaimu as a temporary measures, Jaji Mkuu akirudi au akipona anaendelea na majukumu yake.

Lakini Jaji Mkuu anapomaliza muda wake wa utumishi wa umma, 6 months before notification hutumwa na rais kupelekewa majina matatu to choose from.

Huu Uteuzi wa Prof. Juma kama Kaimu Jaji Mkuu wakati nafasi ya Jaji Mkuu iko wazi permanently is not right!. It is as if Dr.Juma is not trusted hivyo yuko under probation kama atafiti ndipo ateuliwe na asipofiti anateuliwa mtu mwingine!. Hii ni very demoralising na Dr.Juma hawezi kuwa na confidence ya ku exercise all his powers kwa sababu kuna vitu Kaimu Jaji hawezi kufanya ikiwemo kukaimu nafasi ya Urais!.

Ukaimu huu sio sawa na ule Ukaimu wa mtu kukaimu nafasi fulani temporary mwenyewe akirudi unapisha. Huku ni kukaimu wakati nafasi haina mwenyewe!.

Kingine ambacho Mwanakijiji hakijui, hajui kuwa kaimu hata kaimu rais, hawezi kusaini amri yeyote ambaye inapaswa kusainiwa na rais ikiwemo kusaini sheria, kutangaza hali ya hatari, kuteua wala Kaimu rais haruhusiwi kusaini Presidential Preventative Detention Order!.

Enzi za Nyerere kuna siku Ali Hassan Mwinyi alikaimu na akasaini hati ya kizuizini, aliyetiwa kizuizini alishitaki Mahakama Kuu, amri ile ikapigwa chini kwa sababu Kaimu rais ni kaimu na sio rais, ukaimu unaishia kwenye kutoa maagizo na sio kusaini jambo lolote linalohitaji saini ya rais!.

Mfano Bunge likitaka kufanya impeachment process Kaimu Jaji Mkuu hawezi kwa sababu aliielezwa kwenye sheria ni Jaji Mkuu.

Taratibu ni kama sheria. Kama hutajawahi kuwa na Kaimu Jaji Mkuu muda wote huu, why now?!.

Paskali
Excellent!
 
Mkuu Paskali nieleweshe kidogo. Kwenye maelezo yako umesema vitu ambavyo kaimu jaji mkuu hawezi kufanya ni kukaimu nafasi ya urais kama ni hivyo je kaimu jaji mkuu anaweza kumwapisha Rais?
Vitu ambavyo kaimu hawezi kuvifanya ni vile vinavyoelekezwa kwenye katiba kuwa vitafanywa na Jaji Mkuu kama Jaji Mkuu. Hivyo Kaimu Jaji Mkuu anaweza kufanya kila kinachofanywa na Jaji Mkuu isipokuwa kwenye kukaimu urais kwa sababu kukaimu ni delegated powers hivyo kwenye status ya delegated powers hawezi ku delegete wakati yeye sio mwenyewe kama ilivyo kwa kaimu rais anaweza kufanya kila kinachofanywa na rais ila hawezi kutia saini pale green inapotakiwa saini ya rais.

Paskali
 
How? litakuwa na madhara gani? Na kama sheria au Katiba haijaweka kikomo hilo ni tatizo la nani hasa? Kwanini LIssu asije na hoja ya dharura ya kutaka mabadiliko ya sheria au kushawishi wabunge angalau 2/3 yao wafanye mabadiliko ya Katiba?
Umetoa hoja ambayo unajua kabisa wabunge wa CCM hawawezi kukubali jambo hilo hata kama lina faida,Wabunge wa CCM wapo kulinda chama sio maslahi ya nchi.
 
Mkuu Paskali nieleweshe kidogo. Kwenye maelezo yako umesema vitu ambavyo kaimu jaji mkuu hawezi kufanya ni kukaimu nafasi ya urais kama ni hivyo je kaimu jaji mkuu anaweza kumwapisha Rais?
Rais anaapishwa na Jaji Mkuu siyo Acting CJ, soma ibara ya 42 ya katiba. Na Jaji Mkuu anaapishwa na kuteuliwa na Rais
 
Hoja ya lissu mbona iko wazi kabisa...hajasema kuwa rais amekosea..anachosema lissu ni kuwa sheria zetu/katiba hazijaweka limit ya kuwa na acting chief Justice

Kitu ambacho kinaweza kuwa na madhara...hivi hebu chukulia kwa mfano rais aendelee kuwa na kaimu jaji hadi mwaka 2020.....hili jambo lin athari katika utendaji wa jaji

Kwa bahati mbaya Watu wengi huwa hamumuelewi Lisu kwa kipindi hicho anaongea...mnakuja kumuelewa baada ya miezi kadhaa au miaka kadhaa kupita
Mia mia
 
mleta bandiko nimekuelewa sana na usemacho uko sahihi 100% (kwa maandiko ya katiba ila kiuhalisia hauko sawa100%)

unauliza kwamba kukaimu ujaji mkuu hakumfanyi aliyekaimishwa kutofanya kazi kwa kuhofia mamlaka iliyo mpa nafasi (huu ni uongo wafanyakazi karibu wote tanzania ni wanafiki hata huyu aliye kaimishwa hana nguvu/uwezo wa kuipinga mamlaka)

hakuna mtanzania ambaye anaweza simamia ukweli unao mkwanza mteule wake hili lipo wazi

kutoidhinishwa kwa jamaa ni kweli kuna athari za kiutendaji kutokana na tabia za mtanzania kumnyenyekea/kupindisha ukweli ili amfurahishe aliye mpa nafasi.
Sasa kama hili ni kweli kutakiwa na tofauti gani kama akithibitishwa kuwa Jaji Mkuu?
 
Back
Top Bottom