Dar: RC Chalamila amevunja Uongozi wa Soko la Mabibo na kukabidhi kwa Manispaa ya Ubungo

Kindeena

JF-Expert Member
Sep 27, 2017
9,062
15,805
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila leo August 17, 2023 amevunja uongozi wa Soko la Mabibo na kukabidhi soko hilo kwa Manispaa ya Ubungo.

Soko hilo lililokuwa likimilikiwa na kikundi cha watu wachache nakupelekea kuwepo kwa changamoto mbalimbali ambazo Mkuu wa Wilaya Mhe. Hashim Komba alizibaini kama, miundombinu mibovu iliyo pelekea kuwepo kwa tope wakati wa mvua, chemba kuziba, mazingira machafu sokoni hapo, kutokuwepo kwa taarifa sahihi za mapato na matumizi, kutokuwepo kwa maboresho yoyote sokoni hapo huku kikundi cha watu wachache wakinufaika.

Katika mkutano huo, Mhe. Chalamila alianza kwa kuukemea vikali uongozi huo kwa mambo yaliyokuwa yanaendelea sokoni hapo ikiwemo kuwafukuza watumishi wa Serikali na hata kufikia hatua ya kutaka kuchoma moto gari la kubeba taka linalomilikiwa na Serikali.

"Hawawezi kutupanda kichwani, nimechukizwa na vitendo hivyo," alisisitiza Chalamila.

Aidha, Chalamila aliviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha hakuna mtu yeyote atakaye kuja kusumbuliwa wakati serikali ikifanya shughuli zake katika soko hilo kama ukusanyaji wa ushuru na uendeshaji wa soko hilo kiujumla.

Soko litakuwa chini ya Manispaa na kuhakikisha hakuna mfanyabiashara atakaye sumbuliwa na mtu yeyote, taratibu zote zitaendelea kama kawaida, aliwaagiza wafanyabiashara sokoni hapo kulipa ushuru kwa Manispaa.

Baadhi ya wananchi na wafanyabiashara sokoni hapo wamepongeza hatua hiyo ya serikali ya kuchukuwa soko wakiamini soko hilo ninakwenda kuwa bora zaidi kama masoko mengine.

Halikadhalika, Soko hilo limetengewa kiasi cha shilingi milioni 600 kwaajili ya kuliboresha na katika uboreshwaji huo hakuna mfanyabiashara yeyote atakaye ondolewa wakati uboreshaji unaendelea

Pia soma - Hali ya soko la Mabibo wakati wa mvua ni mbaya sana

 
🎵Masudii amekuwa jambazii
Ukikutana naye usikuu pitilia mbalii
Amaa siivyo atakudhuru mama
Amaa siivyo atakudhuru baba......🎵

Serikali imekuwa kwapu kwapu.
Anatoka kiongozi ameshautwika huko anapandisha mzuka na kufanya yake.

Stories za kutunga kibao.
Matumizi mabaya ya dola

Kule Mwenge, serikali imekwapua ardhi ya ushirika kibabe imejenga shopping centre na stand...

CCM imejimilikisha Tanzania isivyo halali
 
Lilianzajeanzaje? Ndio kusema limetaifishwa KWA mujibu wa habari hii?
Hili swali lijibiwe na huyu anayesapoti uhuni wa RC. Soko liliwmzishwa na wafanyabiashara wenyewe na lilikuwa linamilikiwa na wao 100% isipokuwa ushuru wa Halmashauri ulikuwa unatozwa kama kawaida. Sasa RC kijanja anakabidhi soko Kwa Halmashauri na soon tutaona watu wanaanza kulipa Kodi za vibanda Kwa hicho kisingizio cha m600 hewa zitakazowekezwa.
 
Wabongo wamezoea kuishi kiujanja ujanja sana,serikali ifanye kazi yake soko liboreshwe hao wahuni wakiliharibu sana hilo soko hela wanachukua halafu miundombinu wanataka manispaa itengeneze.
 
Mbona hii ni Mara ya pili serikali inalichukua ? Enzi za Makonda hivo hivo wakati urafiki wanataka kuwatimua wafanya biashara wahamie Mburahati serikali iliiendesha na kuanza kuchukua ushuru na mapato ya vyoo vyakulipia ambavyo kwa ujumla Wastani sio chini ya Million tatu kwa siku ? Nini kilikuaja kutokea tena likarudi mikononi mwa madalali wa viazi ?
 
Alipanick tu lkn haikua serious kiasi hicho, watu wapo bize na shughul zao we ukawasumbue na vikao vyako watakuelewa? Wengn sisi makuli tunashusha ndizi na parachichi tusiposhusha tunakufa njaaa, yy analipwa Kwa kuja kikaoni
 
Alipanick tu lkn haikua serious kiasi hicho, watu wapo bize na shughul zao we ukawasumbue na vikao vyako watakuelewa? Wengn sisi makuli tunashusha ndizi na parachichi tusiposhusha tunakufa njaaa, yy analipwa Kwa kuja kikaoni
Kwahiyo kama wewe ni kuli hiyo inazuiaje mambo mengine kuendelea? Alichongea Chalamila huenda kisiwe kizuri, ila sio kwa point zako hizi.
 
Mkuu wa mkoa wa DSM alitembelea Soko la Ndizi Mabibo na kuvunja Uongozi wa Soko hilo kwa madai walimfukuza DC wa Kinondoni alipokwenda kukutana nao

Chalamila akiwa na hasira kali aliwaambia Wafanyabiashara hao kuwa anaweza kuwafyatua na wakapotea kabisa kama wataendelea na mambo yao ya kipumbavu

RC amesisitiza kuwa hakuna Mpumbavu yoyote anayeweza kumpanda kichwani tena Wakome kama Walivyokoma kunyonya Maziwa ya mama zao

Amemalizia kwa kusema Wakiendeleza kumzingua atalifungilia Mbali na Soko lenyewe Ili warudi kwa hao wanaowahonga fedha ili walete fujo

Source: Ayo TV
 
Mkuu wa mkoa wa DSM alitembelea Soko la Ndizi Mabibo na kuvunja Uongozi wa Soko hilo kwa madai walimfukuza DC wa Kinondoni alipokwenda kukutana nao

Chalamila akiwa na hasira kali aliwaambia Wafanyabiashara hao kuwa anaweza kuwafyatua na wakapotea kabisa kama wataendelea na mambo yao ya kipumbavu

RC amesisitiza kuwa hakuna Mpumbavu yoyote anayeweza kumpanda kichwani tena Wakome kama Walivyokoma kunyonya Maziwa ya mama zao

Amemalizia kwa kusema Wakiendeleza kumzingua atalifungilia Mbali na Soko lenyewe Ili warudi kwa hao wanaowahonga fedha ili walete fujo

Source: Ayo TV
Hii ndio Tanzania yetu!
 
Mkuu wa mkoa wa DSM alitembelea Soko la Ndizi Mabibo na kuvunja Uongozi wa Soko hilo kwa madai walimfukuza DC wa Kinondoni alipokwenda kukutana nao

Chalamila akiwa na hasira kali aliwaambia Wafanyabiashara hao kuwa anaweza kuwafyatua na wakapotea kabisa kama wataendelea na mambo yao ya kipumbavu

RC amesisitiza kuwa hakuna Mpumbavu yoyote anayeweza kumpanda kichwani tena Wakome kama Walivyokoma kunyonya Maziwa ya mama zao

Amemalizia kwa kusema Wakiendeleza kumzingua atalifungilia Mbali na Soko lenyewe Ili warudi kwa hao wanaowahonga fedha ili walete fujo

Source: Ayo TV

Soko lipo Wilaya na Manispaa ya Ubungo.

Iweje Dc wa Kinondoni afukuzwe wakati siyo eneo lake kiutawala?

Aliyefukuzwa ni DC wa Ubungo
 
Hili swali lijibiwe na huyu anayesapoti uhuni wa RC. Soko liliwmzishwa na wafanyabiashara wenyewe na lilikuwa linamilikiwa na wao 100% isipokuwa ushuru wa Halmashauri ulikuwa unatozwa kama kawaida. Sasa RC kijanja anakabidhi soko Kwa Halmashauri na soon tutaona watu wanaanza kulipa Kodi za vibanda Kwa hicho kisingizio cha m600 hewa zitakazowekezwa.
Wewe utakuwa Swadaka au Kimwayeya
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila leo August 17, 2023 amevunja uongozi wa Soko la Mabibo na kukabidhi soko hilo kwa Manispaa ya Ubungo.

Soko hilo lililokuwa likimilikiwa na kikundi cha watu wachache nakupelekea kuwepo kwa changamoto mbalimbali ambazo Mkuu wa Wilaya Mhe. Hashim Komba alizibaini kama, miundombinu mibovu iliyo pelekea kuwepo kwa tope wakati wa mvua, chemba kuziba, mazingira machafu sokoni hapo, kutokuwepo kwa taarifa sahihi za mapato na matumizi, kutokuwepo kwa maboresho yoyote sokoni hapo huku kikundi cha watu wachache wakinufaika.

Katika mkutano huo, Mhe. Chalamila alianza kwa kuukemea vikali uongozi huo kwa mambo yaliyokuwa yanaendelea sokoni hapo ikiwemo kuwafukuza watumishi wa Serikali na hata kufikia hatua ya kutaka kuchoma moto gari la kubeba taka linalomilikiwa na Serikali.

"Hawawezi kutupanda kichwani, nimechukizwa na vitendo hivyo," alisisitiza Chalamila.

Aidha, Chalamila aliviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha hakuna mtu yeyote atakaye kuja kusumbuliwa wakati serikali ikifanya shughuli zake katika soko hilo kama ukusanyaji wa ushuru na uendeshaji wa soko hilo kiujumla.

Soko litakuwa chini ya Manispaa na kuhakikisha hakuna mfanyabiashara atakaye sumbuliwa na mtu yeyote, taratibu zote zitaendelea kama kawaida, aliwaagiza wafanyabiashara sokoni hapo kulipa ushuru kwa Manispaa.

Baadhi ya wananchi na wafanyabiashara sokoni hapo wamepongeza hatua hiyo ya serikali ya kuchukuwa soko wakiamini soko hilo ninakwenda kuwa bora zaidi kama masoko mengine.

Halikadhalika, Soko hilo limetengewa kiasi cha shilingi milioni 600 kwaajili ya kuliboresha na katika uboreshwaji huo hakuna mfanyabiashara yeyote atakaye ondolewa wakati uboreshaji unaendelea

Pia soma - Hali ya soko la Mabibo wakati wa mvua ni mbaya sana

Haijui mabibo huyo.Mwacheni
 
Back
Top Bottom