Dar: Rais Samia akabidhi magari 123 kwa Mamlaka za Maeneo ya Utekelezaji kwa Shughuli za TASAF

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,982
FUJRHz0WQAIYtDh.jpg

AMOS MAKALLA, MKUU WA MKOA WA DAR

Kwanza niseme hali ya mkoa ipo salama, hali nishwari tunaendelea na shughuli zetu. Kwahiyo, hata ile operesheni ya panya buku na panya road imefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Kimya kabisa! Lakini, nikuahidi kuwa ni operesheni endelevu.

…juzi tulipata matukio ya moto lakini sisi uliotupa majukumu tukuhakikishie kwamba jambo lile tumeweza kulidhibiti na wananchi wale wafanyabiashara watarudi katika nafasi zao na kuendelea na biashara zao.

LADISLAUS MWAMANGA, MKURUGENZI MTENDAJI – TASAF

Tanzania inashika nafasi ya kwanza kwa Afrika na nafasi ya pili duniani kwa kujenga uchumi junmuishi. Hili limewezekana kutokana na ushirikiano katika ngazi zote za utekelezaji.

Ahsante Rais Samia kwa kuidhinisha kuandikisha kaya mpya 498,091 kwenye mpango wa TASAF ili ziweze kushiriki katika shughuli za kukuza uchumi wa kaya na pia kutoa fedha za UVIKO-19 Shilingi bilioni 5.5 ili ziweze kuwafikia walengwa wa TASAF katika maeneo hatarishi kwa ugonjwa wa UVIKO-19.

Mh. Rais, Awamu ya Tatu ya TASAF ndiyo inatekelezwa sasa. Utekelezaji wake ulianza Februari 2020 na unatarajiwa kukamilika 2025. Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu kimetengewa shilingi trilioni 2.

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

Tumeendelea kuhakikisha wananchi wanaoishi katika mazingira duni (mjini na vijijini) wanaendelea kupata mahitaji yao ya msingi kwa kupata fursa ya kujiimarisha kiuchumi kupitia programu mbalimbali, ikiwemo: kutoa mikopo isiyo na riba na kutoa ruzuku kwa kaya zinazoishi katika mazingira duni.

- Mpango unazaa matunda
Lengo la serikali kuanzisha TASAF ilikuwa ni kupunguza uasikini. Kwahivyo, tunafarijika sana kusikia na kuona kuwa lengo hilo linaendelea kufikiwa.

Taarifa zinasema kwamba hadi kufikia mwaka huu, TASAF inaonesha kuwa mpango huu unachangia kupunguza umasikini wa mahitaji ya msingi ya kaya kwa zaidi ya 10% na umasikini uliokithiri kwa zaidi ya 110%

Kutokana na mafanikio ya mpango huu, sasa ni azma ya Serikali kuendelea na utekelezaji wake ili kuwafikia wahitaji wote katika vijiji, mitaa na shehia

- Viongozi wa kisiasa wasitengwe
Niseme, katika uandiishaji wa kaya masikini, niombe Ndugu Mwamanga, kuna viongozi wa vyama vya siasa, ambao wamepewa vueo vya vyama vya siasa kule chini,… lakini ukimwangalia hali anaishi katika umasikini kwani kuwa mtu wa kuaminiwa na kuwa na busara hakuhitaji pesa. Unaweza kuwa na mazingira duni nab ado ukaaminiwa na jamii.

Kwahiyo, kama watu wamemchagua kuwahudumia katika eneo lile, kusimzuie kufaidika na mapango huu wa TASAF. Isimzuie!

Kama vigezo vinaonesha anaishi kwenye mazingira duni, basi isimzuie kunufaika na mpango huu. Viongozi wote wa vyama vya siasa.

- Elimu ya matumizi ya rasilimali
TASAF mmefanya vizuri kutoa fedha, kusomesha na kuwapa huduma za kiafya. Lakini kuna mwananchi ana uwezo mkubwa sana, anaishi kwenye mazingira yasiyoridhisha, ana ng’ombe 200, 300 lakini anaishi katika mazingira yasiyoridhisha.

Anaishi kwenye nyumba ambayo haiwezi kumkinga dhidi ya maradhi ya TB. Kinyumba hakieleweki. Watoto hawaendi shule, mambo ya bima hana. Naombeni mfanye pia kazi ya kutoa elimu kuwatoa watu kwenye umasikini wa fikira nan a waishi maisha ambayo yanaeleweka.

Lengo ni kuwatoa watu kwenye maisha duni wanayoishi.

- Wasaidiwe kibiashara
Ingawa mradi huu umeiletea sifa Tanzania, bado tukipimwa katika viwango vya umasikini bado tupo chini.

Kupitia TASAF tunakwenda kuinua watu wenye maisha duni wanyanyuke, waungane na wengine katika biashara lakini pia katika maisha. Tukifanya hivyo tutatimiza malengo endelevu SDG’s bila kumuacha mtu nyuma.

Nilipopita kwenye maonyesho, nimeona vikundi vimetengeneza vitu vizuri sana. Wanahitaji misaada midogomidogo, kwa mfano kwenye vifungashio ya vitu wanavyovizalisha. Vifungashio vitawapa soko.

Wote wamelilia masoko. Lakini masoko kwakuwa bidhaa zao hazijafikia viwango, na moja kati ya viwango ni vifungashio.

Naomba sana wasaidiwe.

- Fedha zitumiwe ipasavyo
Ndugu zangu, wanangu mnaofanya kazi TASAF, TASAF kama ilovyosemwa ina Tshs trilioni 2 ambazo fedha hizi si msaada. Fedha hizi ni mkopo. Tunachukuwa mikopo nafuu kuinua watu wetu wa chini.

Naomba mkazitumie fedha hizi ipasavyo. Nina taarifa, nina habari kwamba kwenye baadhi ya maeneo bado kuna walafi. Kuna watu wapo midomo wazi na wanafanya kila wanaloweza wale fedha hii.

Na inapotokea kuna mmoja mgumu, huyo ndiyo adui yao na huyo ndiye anapigwa vita.

Kuweni na imani. Fedha hii tunakwenda kuilipa Watanzania wote. Chukuwa kile unachopaswa kuchukuwa kutokana na kazi yako.

- Kamati ziwe Jumuishi
TASAF inalazimisha mchanganyiko wa wajumbe katika kamati zake – wanawake na wanaume. Maeneo mengine kwa idadi sawa na maeneo mengine kwa idadi ya kutosha ya Wanawake.

Sisemi mpango huu hauna mapungufu – yapo. Lakini kwa uchache sana.

Tulifanya makossa kwenye awamu ya kwanza ambapo kamati zile hazikuwa na uwiano wa uwakilishi. Kuna maeneo unaambiwa, au unakuta, tatizo la mahali hapo unaambiwa ni soko. Soko linajenngwa lakini ukienda ukitembea soko halitumiki kwasababu siyo shida ya sehemu hiyo.

Na kwenye kamati waliokuwa wakipendekeza soko walikuwa wanajitazama wao kuliko mahitaji ya jamii ile. Lakini kwenye yale maeneo ambapo jamii imeshirikishwa kweli kumejengwa mahitaji ya jamii.

- Maangalizo kuhusu magari

1. Ili kufuatilia nyendo za magari haya, magari yatafungwa mifumo ya car-tracking

2. Magari hay ani kwaajili ya shughuli zaTASAF mijini na vijijini. Yatumike kwenye shughuli za TASAF kama ilivyoainishwa katika mkataba na makubaliano baina ya TASAF na Halmashauri.

3. Utunzaji wa magari haya ni jukumu la Halmashauri. Yamenunuliwa kwa fedha nyingi hivyo ni vema yakatunzwa ili yafanye kazi kwa miaka mingi. Magari haya yasiende kuharibiwa kwa makusudi, yakapangiwa mawe ili Wakurugenzi waje kuomba kuyanunua.

Likiharibika mapema, Mkurugenzi utatuambia kwanini limeharibika mapema.

4. Service ya magari haya ifanywe na wazoefu, kutoka kampuni ya Toyota ambao ndiyo wasambazaji. Najua mtasema Toyota watawafanyia service kwa gharama, lakini kama wameweza kutuuzia kwa nusu bei, inawezekana kuzungumza nao. Zungumzeni na Toyota.

Magari ya zamani ambayo yalikabidiwa kwaajili ya utekelezaji wa TASAF na ambayo yalitolewa taarifa kuwa ni mabovu, yote yarudishwe ofisi za TASAF tawi la Dar es Salaam yakiwa na vifaa vyote muhimu. Mwamanga, usipokee magari yaliyotolewa vifaa.
 
Alhad badala ya maombi yeye amejikita kwenye Kitubio (Toba), hii maana yake ni nini?
 
Naamini ni magari ambayo bei ya manunuzi na gharama za uendeshaji si kama Ma - VX...!
 
Yule mwehu wenu aliyekuwa akizindua mpaka vyerehani ili tu awe live kwenye TV zote mbona hukuuliza kuwa amekosa kazi?
Leta ushaidi wa Magufuri kuzindia kiwanda cha vyereani, harafu kipimo cha utendaji wa Samia sio Magufuri, Magufuri alifanya yakwa
Kukabidhi magari nayo ni kazi ya rais siku hizi?

Hii nchi viongozi wanakula maisha tu hakuna kazi ya kufanya.
Njoo na data, wapi na lini?
 
Yule mwehu wenu aliyekuwa akizindua mpaka vyerehani ili tu awe live kwenye TV zote mbona hukuuliza kuwa amekosa kazi?
Leta ushaidi wa Magufuri kuzindia kiwanda cha vyereani, harafu kipimo cha utendaji wa Samia sio Magufuri, Magufuri alifanya yakwakwe na Samia afanye ya kwakwe, sio kila kitu mbona Magufuri alifanya hivo, wambie wasaidizi wa Samia wawe wabunifu sio kutembea kwenye nyota ya magufuri
 
Mheshimiwa Rais, pamoja na nia yako hiyo njema ya kukabidhi hayo magari kwa taasisi za serikali, najua kwa sehemu kubwa hayo magari yatatumika na viongozi wa taasisi hizo.

Naomba uangalie kwa jicho la pekee kwa upande wa UONGOZI wa Taasisi hizi za Serikali na Mashirika ya Umma. Taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma kuna OMBWE KUBWA la UONGOZI. Ni watu wasio na utu, wala weledi wa uongozi. Kwa Mfano, Taasisi ya Serikali kubwa kama UDSM haina VC kwa takribani miaka 4 sasa.

Tujuavyo sisi watanzania VC wa UDSM kwa mfano huwa ni mtu mwenye hadhi ya Kidiplomasia, Mwerevu, Msomi mzuri aliyeelimika, Mtu wa watu, mwenye UTU, Mwenye Ushawishi, Mbeba Maono na Nembo ya Taasisi husika, Mwalimu wa wengine, anayependa kuwalea na kuwainua wengine, anayemfundisha na kumwelekeza kwa upendo asiyejua na siyo "KUUA".

Kubwa Zaidi VC wa UDSM kwa mfano tangu kuzaliwa kwa taasisi hii HULEA VIPAJI na KUVIPA NAFASI ya kuchanua. Mheshimiwa Rais na WAZIRI wa ELIMU na VIONGOZI wa Wizara inayohusika na UTUMISHI wa UMMA fuatilieni kwa karibu kinachofanywa na Mamlaka za UDSM na Matawi yake.

Hata Utendaji kazi wa Mabaraza ya Ushauri na Usimamizi wa Taasisi hii ni dhaifu sana. Wanapitisha na Kuamua kadiri Uongozi wa Taasisi unavyotaka. Ukweli kinachoendelea ndani ya UDSM na Matawi yake ni visasi, kukomoana, kuumizana na kuonyeshana ubabe tu.

Utadhani siyo taasisi ya wasomi wanaoweza kutumia nadharia, vyeo vya kitaaluma na maarifa wanayodai kuwa nayo kuendesha Taasisi hii.
 
Mheshimiwa Rais, pamoja na nia yako hiyo njema ya kukabidhi hayo magari kwa taasisi za serikali, najua kwa sehemu kubwa hayo magari yatatumika na viongozi wa taasisi hizo.

Naomba uangalie kwa jicho la pekee kwa upande wa UONGOZI wa Taasisi hizi za Serikali na Mashirika ya Umma. Taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma kuna OMBWE KUBWA la UONGOZI. Ni watu wasio na utu, wala weledi wa uongozi. Kwa Mfano, Taasisi ya Serikali kubwa kama UDSM haina VC kwa takribani miaka 4 sasa.

Tujuavyo sisi watanzania VC wa UDSM kwa mfano huwa ni mtu mwenye hadhi ya Kidiplomasia, Mwerevu, Msomi mzuri aliyeelimika, Mtu wa watu, mwenye UTU, Mwenye Ushawishi, Mbeba Maono na Nembo ya Taasisi husika, Mwalimu wa wengine, anayependa kuwalea na kuwainua wengine, anayemfundisha na kumwelekeza kwa upendo asiyejua na siyo "KUUA".

Kubwa Zaidi VC wa UDSM kwa mfano tangu kuzaliwa kwa taasisi hii HULEA VIPAJI na KUVIPA NAFASI ya kuchanua. Mheshimiwa Rais na WAZIRI wa ELIMU na VIONGOZI wa Wizara inayohusika na UTUMISHI wa UMMA fuatilieni kwa karibu kinachofanywa na Mamlaka za UDSM na Matawi yake.

Hata Utendaji kazi wa Mabaraza ya Ushauri na Usimamizi wa Taasisi hii ni dhaifu sana. Wanapitisha na Kuamua kadiri Uongozi wa Taasisi unavyotaka. Ukweli kinachoendelea ndani ya UDSM na Matawi yake ni visasi, kukomoana, kuumizana na kuonyeshana ubabe tu.

Utadhani siyo taasisi ya wasomi wanaoweza kutumia nadharia, vyeo vya kitaaluma na maarifa wanayodai kuwa nayo kuendesha Taasisi hii.
Naomba kuuliza kwani Anangisye hayupo?

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Piga kazi mama tumecheleweshwa mnooo kama taifa. Kanyaga twende
 
Back
Top Bottom