zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,938
Hapana,Alkaeda siyo uislam,I stand to be corrected.
Hata Ku KLux Klan sio Ukristo.
Hapana,Alkaeda siyo uislam,I stand to be corrected.
nani kachoma kanisa huku bara..? hebu taja! ...
zanzbar uamsho walishakataa kwamba wanahusika mbona unalazimisha
huwezi kujua vinavyotuletea maendeleo sababu weye sio muislam
ahsante acha tutumike!
Kaskazini, mashariki na kusini kuzunguka nje ya uzio wa Ikulu kuna idadi kubwa ya Askari FFU na vifaa vya kazi. Ni idadi kubwa kuliko siku zingine.
Upande wa baharini mahali ambapo ni eneo la kuegesha magari kukiwa na sherehe kubwa ikulu, kuna gari ya maji ya washawasha, defender nne na FFU wamebeba bunduki na mabomu ya machozi.
Wamewakamata wamewahesabu sasa wawa achie...mbona majizi ya Rasmali hayakamatwi..
Hata Ku KLux Klan sio Ukristo.
Hivi intellijensia ya Polisi haikujua maandamano haya ili kuyazuia? Mbona hii intellijensia inafanya kazi one side tuu
Lingine ni kuwaombea ndugu zetu hao brain washed wasije wakapigwa risasi na hawa askari wa ccm.
Na nikwambie kitu mkuu? Nisiowapenda mimi ni hawa waislamu 'extremists' ambao kila kukicha wanajambisha watu kwa vitisho. Na isitoshe, hawa wanadhalilisha uislamu sana kwani watu wengine wanafikiri kuwa uislamu ni dini ya vurugu na ukitaka kuwa muislamu mzuri lazima uwe mtukutu kwa saaana, lakini dini ya kiislamu haipo hivyo, basi tu hao, ambao katika percentage ya waislamu ni wengi, wanapenda shari muda wote. Sometimes huwa najiuliza, hivi kwa miaka 100 ijayo, uislamu utakuwepo kweli? Maana kama mambo yanakwenda hivi, mh, hivi vizazi vipya na vijavyo..., lol, kabila tu ndo mtu hawezi kubadili.Siyo waislam wote ni watu wa amani.Kuna mujahedeen ama Alkaeda nk.Sasa hao utawakuta wanapata baraka za misikiti.Nguvu za maextremist wenye msimamo mkali imewashinda moderates.Na consenquences ni for all regardless.And that's the sad part of it.
MUNGU awabariki... Miaka 50 Malalamiko yenu hatukuwahi kuyaona kwenye Maandamano... Sasa hivi yanatisha... YANA UBABE,
NGUVU... hatujawahi kuona tunayaona kwenye TV kwenye nchi za watu wengine; kwanini tusiulize? tulidhani kudai haki ilikuwa
kuna njia tofauti na pale kweni nyinyi RAIS ni MWISLAMU; MAKAMU MWISLAMU na WAZIRI WA ULINZI MWISLAMU; JAJI
MKUU MWISLAMU; JAJI KIONGOZI MWISLAMU nilidhani kuna njia za kiusalama kufuata... SIO KUTISHIA JIJI ZIMA...
Mkuu mvumbuzi wewe ndio umevumbua hili,wenzako serikalini wanakula bata wanajua wamesolve issue kilainiiiii,kama kumsukuma mlevi.... kumbe!!!Kama maandamano yaliyofanywa na Waislam kuelekea ofisi ya Mchimbi yamepelekea Waislamu waliogomea sensa kuachiwa ni dhahiri hawakuwa na kosa . Kwa sababu hiyo Dr. mchimbi anatakiwa ajiuzulu kwa kushindwa kazi la sivyo awaeleze Watanzania kama walikamatwa kimakosa au amewaogopa waislam. Katika historia ya nchi yetu na kwa kumbukumbu za karibuni sijawahi kuona maandamano kufanywa hadi makao makuu ya Jeshi la polisi huku polis wakisindikiza.
Huu ni udhaifu mkubwa wa serikali kwani kitu chochote kingeweza kutokea eti kisa waislam. Maandamana ya waislam yalikuwa violent kuliko ya CHADEMA huku wakitoa matamko ya kutishia amani ya dini na nchi kwa ujumla lakini wameachwa hadi kufika Makao makuu ya Polisi. Tunabaki na maswali mengi mno kuhusu implication na mesage behind ambayo JK anataka wawasio waislam tuipate.
Kama kweli hawa waislam waliogomea sensa walitenda kosa haikuwepo sababu ya kuwaachia kwa shinikizo la maandamano kwani next time wataandamana tena kutaka Malasusa au Kadinali Pengo aachie ngazi na serikali ika comply. Lazima serikali iangalie implication kwani hili nahesabu ni mmojawapo ya makosa yasiyo ya lazima na ya kizembe kabisa kuwahi fanywa na serikali ya JK. Naomba kama hawa Waislam walikamatwa kimakosa Waziri Mchimbi ajiuzulu kwa kusababisha uvunjivu wa amani kwa uwezo wake mdogo wa kutoweza kutofautisha lipi ni kosa na lipi siyo kwani nchi itayumba hii.
miminataka waunguze hiyo wizara hapo .. Wanangoja nini? Piga moto wizara hiyo
Mkuu umenifurahisha na majibu yako murua.Mkuu mimi sihitaji kuwa na nyimbo maana sio mwana kwaya wala muimba bongo flavor! Ninacho kisimamia na ambacho nitakisimamia hata kutofautiana na wewe muislamu mwenzangu ni hizi kauli za kuchukia na kuleta uhamasa wa dhihiri kwa watu wa dini nyingine wakati uislamu hautufundishi hivyo. Kama mtu mmoja akileta dharau kaleta yeye kama yeye na nita deal naye yeye na sio watu wa dini yake, dhehebu lake. Huyualiye tukana anahitaji kuelemishwa ili ayaone makosa yake ndio maana hata waislamu wenzetu huwa tunawalingania kwenye dini yetu, sio?
Mkuu. Mimi siamini uislamu wenye kujengeana chuki na uhasama kama baadhi ya waislamu wenzangu wanavyotaka/kuonyesha tuwachukie na kuwajengea uhasama wakristo wote! Najua hawa wanao onyesha chuki za wazi wanazionyesha hapa kwenye bodi lakini chuki hizo haziendi moja kwa moja mpaka kwa masheikh wetu au viongozi wetu wanao tufundisha kuwa uislamu ni dini ya amani na upendo, chuki zao/zenu zipo hapa kwa vile tu ziko.
Naamini kwa haya ninayo yafanya kwa kuheshimu imani za wengine, dini za wengine, utu wa watu wengine na kuwaelimisha pale inapo bidi uzuri wa dini yangu, basi mwenyezi Mungu aliye mwingi wa rehma hata nichukia na kuniadhibu eti kwa kuwa naishabikia Chadema.
Salaam alykum.
Sent from BlackBerry 8520 authorized by JamiiForums.