Waislam mchana huu wanakusanyika maeneo ya kariakoo kwa ajili ya kwenda Wizara ya mambo ya ndani kwa njia ya maandamano.
Lengo kuu la maandamano hayo ni kwa ajili ya kuishinikiza serikali kuwaachia huru na kuwafutia kesi watu ambao wamekamatwa kutokana na kususia zoezi la SENSA, TAYARI waislam waliosali msikiti wa Mtambani (kitovu cha harakati) wanaelekea huko.
================================UPDATE=================================
Waandamanaji wakiwa karibu na geti la Wizara ya Mambo ya ndani
Wanaswali!
Lengo kuu la maandamano hayo ni kwa ajili ya kuishinikiza serikali kuwaachia huru na kuwafutia kesi watu ambao wamekamatwa kutokana na kususia zoezi la SENSA, TAYARI waislam waliosali msikiti wa Mtambani (kitovu cha harakati) wanaelekea huko.
================================UPDATE=================================
Waandamanaji wakiwa karibu na geti la Wizara ya Mambo ya ndani
Wanaswali!
Wamekuja kutaka wenzao waliokamatwa kwa kgomea sensa waachiwe huru walizuiwa lakini wamekuja kutoka kila kona na saa hizi barabara ya posta kutoka maeneo mengine moja imefungwa kwa muda na tention ni kubwa saa hiz wanamalizia kuseali salz la alasiri
Wamemaliza kuswali tunasubiri njia ya kuingia polisi makao makuu nayo imefungwa
Picha za Maandamano ya DSM leo 07/09/2012 kwa hisani ya KUMKICHWA: Breaking News: Picha za Maandamano Ya waislamu Wizara Ya mambo ya ndani
![]()
Mpaka muda huu Saa 10:21 Waislamu bado wako Wizara ya Mambo ya ndani, Barabara zimefungwa, Baadhi ya Shughuli za Muhimu za Kiuchumi zimesimama, Baadhi ya Maofisi yamefungwa.
Hivi ni Serikali au CCM inashindwa kuwaondoa au kuongea nao Waislamu waliondamana na shughuli za Uchumi na Kazi kurejea katika hali ya Kawaida maeneo ya Posta?
Naohofia Vurugu na Mali za watu zisije kuharibiwa tu.
It's very unfortunate that asilimia kubwa wanaokashifu maandamano haya tena kwa lugha za kejeli ni wale wale wanaofahamika kwamba ni wafuasi wa CHADEMA!! Hapa ndipo watu kama akina Mkandara wanapopata taabu kwani pamoja na Uislamu wao bado ni wapenzi wakubwa wa CHADEMA!!
Hivi sasa akiingia, atalazimika kujibishana na wale wale ambao wana itikadi moja katika kuiondoa CCM madarakani! Kama kweli CHADEMA wana lengo la kweli la kutafuta haki basi nilitarajia wawaunge mkono watu mbalimbali na makundi yao ikiwa kuna wanachokipigania! Na kama si lazima kuwaunga mkono, basi busara ingekushauri kukaa kimya kuliko kuwadhihaki kwa maneno ya kejeli! Hali kama hii ndiyo inayowafanya baadhi ya Waislamu waamini kwamba CHADEMA ni kwa ajili ya watu fulani tu......inakuwa ngumu kuyapinga madai kama hayo hasa ukizingatia maoni ya Pro-CHADEMA.
Mie nilikimbilia eneo la tukio muda mrefu tu uliopita; pale hamna cha CHADEMA wala CCM na bango mojawapo linasomeka "POLISI ACHENI DHULUMA, SENSA IMEFELI MAUAJI YA NINI?" Sasa mnataka kusema watu kama hao hawana madai ama hojaya msingi?! BInafsi, nimehesabiwa sensa na sikuona sababu ya kususia zoezi hilo. Hata hivyo, siwezi kuwa mkosefu wa busara ikiwa nitadhihaki wale waliogomea na kuwaita wajinga kwani nafahamu, kila mtu ana jambo lenye maslahi kwake. Lenye maslahi kwako si lazima liwe na maslahi kwa mwingine.
Ukifahamu hivyo, basi utagundua ni ujuha kumdhihaki mwingine kwa kumtaka aamini kama unavyoamini wewe! Anyway, kama unataka aamini kama unavyoamini wewe; ya nini basi kumtaka afanye hivyo huku ukimkejeli?!
Baada ya maandamano Hatimaye waislamu waliokua wamishikiliwa waachiwa huru souce ITV BREAKING NEWS
Clouds FM Imeripoti muda si mrefu kuwa muafaka umefikiwa kuwa wale wote waliokamatwa kwa ajili ya sensa waachiwe mara moja.
Wanahamia msikiti wa kichangani kupanga ufuatiaji wa agizo hilo