Dar: Maandamano makubwa katikati ya Jiji

Dar: Maandamano makubwa katikati ya Jiji

Status
Not open for further replies.
Hakuna Muislaam wa siasa kali wala baridi. Uislaam ni Uislaam tu. Mafunzo yake basically yanatokana na Qur'an na Qur'an ni moja tu.

Hayo ni maneno yanayojengwa na wasio waislaam ili kuwatenganisha waislaam na kuyatamk akwako na kuyakubali ina maana wewe umemeza, chambo, ndoano, chubwi na mshipi. Tafadhali badilika na uelewe Uislaam ni mmoja tu na usidanganyile wala usidanganywe kuwa kuna Uislaam wa siasa baridi au siasa kali.

Waislaam tunaelewa kuwa wapo wanaojiita Wakristo lakini Uislaam hautambui kama kuna Dini ya Mwenyeezi Mungu inayoitwa Ukristo.

Ingekuwa kweli umesameh hii post yako isingebeba jazba namna hii.

Uislaam unatiwa aibu na wale wanaokuwa na mashtani wenzao husema kuwa sisi tu pamoja nanyi wale tulikuwa tunawadhihaki tu. Uislaa hauingii aibu kwa kuusemea kwa wema japo neno moja tu la mafundisho yake. Kama unayeelewa vizuri mafundisho ya Kiislaam hutakiwi kuona haya kwa Uislaam wako. Kipi kibaya katika Uislaam hata kikufanye uone haya?
Hapana,Alkaeda siyo uislam,I stand to be corrected.
 
na kwambia kwa serikali ya CCM haiwezi kuwakamata haina ubavu huo mkuu wanawaogopa kama nini wakidhubutu waislamu watalianzisha mpaka magogoni na mkulu atang'oka mkuu,subutu yao hawawezi nakwambia.
Wale wa mwembechai waliokung'utwa walilianzisha mpaka wapi? Ukibebwa kama mayai ndiyo unapata kichwa na hiyo?
 
njiwa, kuna watu wanataka kuhusisha masuala ya uislam na hoja zao za kisiasa, eti kwa nini cdm wanazuiwa, na hoja nyingine dhaifu, wanashindwa kuelewa hayo masuala ya waislam hayafungamani na chama chochote cha siasa.
Uislam hautegemei nguvu au uwepo wa chama chochote cha siasa ili usimame, unajitegemea na unajitosheleza, hauhitaji collabo na ccm, cdm wala cuf.
 
hivi kati ya walioandamana na wasomi wapo.!?
 
Hakuna Muislaam wa siasa kali wala baridi. Uislaam ni Uislaam tu. Mafunzo yake basically yanatokana na Qur'an na Qur'an ni moja tu.

Hayo ni maneno yanayojengwa na wasio waislaam ili kuwatenganisha waislaam na kuyatamk akwako na kuyakubali ina maana wewe umemeza, chambo, ndoano, chubwi na mshipi. Tafadhali badilika na uelewe Uislaam ni mmoja tu na usidanganyile wala usidanganywe kuwa kuna Uislaam wa siasa baridi au siasa kali.

Waislaam tunaelewa kuwa wapo wanaojiita Wakristo lakini Uislaam hautambui kama kuna Dini ya Mwenyeezi Mungu inayoitwa Ukristo.

Ingekuwa kweli umesameh hii post yako isingebeba jazba namna hii.

Uislaam unatiwa aibu na wale wanaokuwa na mashtani wenzao husema kuwa sisi tu pamoja nanyi wale tulikuwa tunawadhihaki tu. Uislaa hauingii aibu kwa kuusemea kwa wema japo neno moja tu la mafundisho yake. Kama unayeelewa vizuri mafundisho ya Kiislaam hutakiwi kuona haya kwa Uislaam wako. Kipi kibaya katika Uislaam hata kikufanye uone haya?

huwezi changanya siasa na dini hata siku 1 gamba wewe uliyejivika uislamu bandia na wakati nyie ndio mnaoiba fedha za kodi zetu na kuzipeleka kanisani pamoja na wakina lowasa na sitta.
 
Polisi wa IGP mwema wako wapi kuzuia maandamano hayo ambayo yanafanyika kabla ya sensa kwisha?. Polisi hao wapo kwa ajili ya M4C tu na wanachama wa chadema?. Je vyombo vya usalama vilikuwa havina taarifa kwamba waislam watafanya maandamano hayo leo?. Nina wasiwasi mkubwa na jinsi nchi inavyoendeshwa, kwani inaonekana wazi kwamba vyombo vyote vya usalama viko kuwadhibiti Chadema tu na wala si kitu kingine.
Sensa ilifanyika wapi na wapi?.Mi najua pale magogoni nilimuona hajat akimuhesabu JK na wajukuu zake.Huku kwetu hakuna.
 
Kama wana Kibali FFU wa nini? Maana hawachelewi kumlipua mtu na bomu halafu waseme aliangukiwa na kitu kizito!!
 
TAIFA LETU TULIPENDALO SAAANA LA TANZANIA HIVI SASA LIKO NJIANI KUANGAMIA SHAURI YA KUKOSA UONGOZI SIKIVU, ADILIFU NA WENYE HEKIMA

"Taifaa la Tanzania linaumwa tena linaugua ugonjwa wa hatari sana tangu uchaguzi wa Oktoba 2010, kufanyike juhudi za haraka kulitibu taifaa," alisikika miezi michahe akitoa hii kauli yenye hekima tele yule Mhe Mbuye wa Arusha alie likizoni Godless Lema.

Hata hivyo, ni wangapi ndani ya nchi hii walau waliweza kumuazima sikio na kutafakari ki-undani zaidi hii kauli???????????

Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete na maswahiba wake wanaoendelea kufilisi nchi hii kupitia Dowans, EPA na rundo la fedha za ki-shetani kwenye Benki Uswisi, wataendeleaa kuishi kwa matumaini ya ulinzi wa FFU mpaka lini?????????

Ama kweli Tanzania taifa langu linaangamia kwa kukosa uongozi wenye hekima na uadilifu.

Kaskazini, mashariki na kusini kuzunguka nje ya uzio wa Ikulu kuna idadi kubwa ya Askari FFU na vifaa vya kazi. Ni idadi kubwa kuliko siku zingine.

Upande wa baharini mahali ambapo ni eneo la kuegesha magari kukiwa na sherehe kubwa ikulu, kuna gari ya maji ya washawasha, defender nne na FFU wamebeba bunduki na mabomu ya machozi.
 
ingependeza tuone na chadema nao wanaandamana kuelekea walipo waislamu kuwaunga mkono

sijui waislamu ndio wangeanza attack au polisi

maana haya matumizi ya nguvu hata hayaeleweki
 
huwezi changanya siasa na dini hata siku 1 gamba wewe uliyejivika uislamu bandia na wakati nyie ndio mnaoiba fedha za kodi zetu na kuzipeleka kanisani pamoja na wakina lowasa na sitta.

Uislaam unahusisha kila kitu ukijuwacho na usichikijuwa, siasa ikiwemo.
 


MOU,KUCHOMA MAKANISA NDO MADA ZENU.,

Viletavyo Maendeleo kwa Uislam ni Kugomea Sensa,na Kutofanya Kazi,na kusoma Madrassa??

Na Mtatumiwa Sana na CCM. Kwa sababu sasa hvi hamjitambui


nani kachoma kanisa huku bara..? hebu taja! ...

zanzbar uamsho walishakataa kwamba wanahusika mbona unalazimisha

huwezi kujua vinavyotuletea maendeleo sababu weye sio muislam

ahsante acha tutumike!
 
Heshima kwenu wakuu,

Napata taabu sana wanajamvi wenzangu mnaaowakejeli waIslam kwa kuandamana.WaIslamu wana haki ya kuandamana mradi hawavunji sheria za nchi,iwapo kuna sheria,kanuni au taratibu zimekiukwa ni wajibu wa vyombo vya dola kuhakikisha wavunjifu wa sheria wanachukuliwa hatua stahiki [si kuwapiga risasi].

Naomba wanajamvi wote tuache mara moja kukejeli imani za watu wengine,unapokashfu Imani usiyoiamni upo uwezekano mkubwa Imani yako nayo ikadharauli.

Nawatakia maandamano ya amani waIslamu wote walioandamana bila vurugu.Mungu Ibariki Tanzania,Mungu Ibariki Afrika.
 
naomba kujua tofauti ya wale wanaovaa surwali ndefu na wale wanaovaa fupi

Ha ha ha!Mkuu sijawahi katika maisha yangu kuwa na shida na waislam,ila maybe labda walikuwa wanaficha ama sijui ni kitu gani?maana mtu anakulazimisha kabisa eti umchukie!Hiyo si amani hata kidogo!Ndo maana ninaamini mafisadi ndo wanaendeleza haya ili wasahaulike.Na hilo la kufanya kila kitu just kwa kutumia hiyo slogan ya "muislam mwenzetu"siyo mbaya hata kidogo endapo kama hayo hayageuki kuchukia wenzao kiasi hiki.It doesn't make any sense kufanya na kusema haya huku ukirun around na kusema "Islam is a religion of Peace",unless peace inayozungumziwa ni tofauti na tunayoijuwa universally.
 
Japo mimi mpagani, lakini nimependa ushirikiano huu. Ila usiishie kwenye mambo ya dini tu. Nendeni hadi kwenye ilimu. Mkifanya maandamano ya mchango, mtajenga shule nyingi sana.
 


sipo DAR mkuu!... ila nafurahi kuona waislam walivyo kuwa na umoja

Wangeonesha umoja wao katika kutatua matatizo katika jamii hasa elimu, afya, uzembe, ufisadi, rushwa nk.nk. serikali ingebadilika na kuwajibika zaidi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom