Dar Lux kapotezwa?

Dar Lux kapotezwa?

Utafika mbali wanaoendelea ni wasio na mikopo unakuwa na real capital

Mawazo ya kimaskini. Hufiki mbali bila mikopo au some external investment be it investors, syndication, shareholders etc. Whatever you call it bado ni hela za watu na utawajibika kwao. Organizations kubwa kama Manchester United hadi banks zenyewe zina madeni ndo sembuse wewe? Madeni sio mabaya, kibaya ni matumizi. Wewe utadunduliza hadi lini kupata capital ya 10M USD?
 
Umesahau kutaja rangi ya Ngozi ya wamiliki wa basi tajwa. Na wote wapo mjengoni wakiteta na wafanya maamuzi katika Chama. Unategemea nn?
Hawa jamaa kwenye sekta ya usafirishaji wako na biz strategies nzuri sana.

Hata ukiangalia kwenye malori akina Kanji Lalji akina F.M Abri ni miaka na miaka wanakimbiza tu
 
Nimesema kwenye uzi mwingine, I'll c&p here:

Biashara ya mabasi ni biashara pasua kichwa kuliko zote.

Scandinavia iliyofanya Mapinduzi kwenye hii sekta ilikufa kifo Cha mende.

Hood imekufa.

Sumry chali.

Sauli yupo hoi siku zake zinahesabika, Achimwene got him in the headlock.

Dar express, Dar Lux, Rungwe waliokuwa powerhouse kwenye hii sekta wote wapo hoi. Etc etc

Turnover kwenye hii sekta ni kubwa mno. Kila miaka miwili wanakuja wengine na kupotea kama upepo household names.

Utasema usimamizi na sababu zote ila sio rahisi kusema hao wote hawajui wanachokifanya. Fanya hii biashara kama unataka kufukia pesa zako.
Shabiby,Abood, super feo na New force wamejitahidi kudumu
 
Biashara za mabasi faida utaanza kuiona kwa wastani wa muda miaka kuanzia miwili.
Kuna biashara ambazo zitakusaidia tu kutengeneza flow nzuri ya pesa , kuweka pesa kwenye mzunguko na kutengeneza discipline nzuri ya pesa lakini si biashara zitakazo kutoa au kukupa utajiri maradufu.

Naweza sema ni kama ile unaona kuliko kukaa na milioni 300 bank, kwa nini usiiweke kwenye mzunguko izae taratibu kuliko kukaa na pesa mwisho utaiharibu kwa matumizi ya ajabu au kutumia hovyo ikaisha.

Ni kama utumie milioni 50 kujenga nyumba utakayoipangisha kwa mwaka upate mil 4, itachukua miaka 12 kuanza kupata faida, lakini ni biashara ambayo unaweza kusomesha watoto wako hadi chuo kikuu wakitegemea kodi ya nyumba, lakini hio mil 50 ungekaa nayo ndani, isingetoboa mwaka.

Biashara ya mabasi ni nzuri kama huna pesa za tia maji tia maji, inapaswa uwe na mfuko wa kueleweka, mapato unaweka bank unakuja kuchungulia account baada hata ya mwaka au zaidi.

Si kila biashara ni kwa ajili ya faida kubwa. Ni baadhi, na unapoanzisha business unakuwa na malengo.
Hatuwezi sema amefilisika, ni maamuzi tu.
Una akili za kivivu.
 
Dar Lux alimzurumu Mama mmoja nyumba yake hapo Mbezi beach walikua wanakopesha hela za Riba na weka dhamana baadae riba ikawa kubwa wakachukua nyumba na yeye Lux aliweka dhamana Bank na kukopea hela zilizofanya aweze kununua na kukopa baadhi ya magari enzi za Magu yule Mama alipolalamika hilo swala likafatiliwa mpaka mahakamani ikaonekana palikua na janja janja tu toka hapo wakaanza kupiga mnada bus zake moja baada ya ingine kuna muda mengine unakuta bus jipya lipo chini ya madarali wakilitangaza kuliuza bus ziliuzwa zikiwa safarini...
Nadhani kwa bus zilizouzwa kwa bei ndogo hizo ni mojawapo aisee..
Sasa matatizo kama haya watu wengine wakisikia fulani kashindwa biashara utasikia biashara ya Bus sio kabisa kumbe kuna vitu vipo chini ya carpet wazee...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom