Dar Lux kapotezwa?

Dar Lux kapotezwa?

Biashara za mabasi faida utaanza kuiona kwa wastani wa muda miaka kuanzia miwili.
Kuna biashara ambazo zitakusaidia tu kutengeneza flow nzuri ya pesa , kuweka pesa kwenye mzunguko na kutengeneza discipline nzuri ya pesa lakini si biashara zitakazo kutoa au kukupa utajiri maradufu.

Naweza sema ni kama ile unaona kuliko kukaa na milioni 300 bank, kwa nini usiiweke kwenye mzunguko izae taratibu kuliko kukaa na pesa mwisho utaiharibu kwa matumizi ya ajabu au kutumia hovyo ikaisha.

Ni kama utumie milioni 50 kujenga nyumba utakayoipangisha kwa mwaka upate mil 4, itachukua miaka 12 kuanza kupata faida, lakini ni biashara ambayo unaweza kusomesha watoto wako hadi chuo kikuu wakitegemea kodi ya nyumba, lakini hio mil 50 ungekaa nayo ndani, isingetoboa mwaka.

Biashara ya mabasi ni nzuri kama huna pesa za tia maji tia maji, inapaswa uwe na mfuko wa kueleweka, mapato unaweka bank unakuja kuchungulia account baada hata ya mwaka au zaidi.

Si kila biashara ni kwa ajili ya faida kubwa. Ni baadhi, na unapoanzisha business unakuwa na malengo.
Hatuwezi sema amefilisika, ni maamuzi tu.
Pesa ya basi katika laki kula elfu tano tu....nyingine tia bank...au uvunguni🙂
 
Biashara ya mabus sio biashara ya mwekezaji mzuri.
Ni biashara ya kuuzia sura kwa wapenda sifa.wapiga wa kodi zetu na watoa makafara kwao rahisi kupata damu.Au wakurupukaji baada ya kupiga madini au site.
Anaeiba Kodi zetu haoni uchungu kununua mabus au kuendesha bus Kwa Hela ya ofisi.
Ni kama zilivyo daladala nyingi ni za watumishi thus wakistaafu nazo zinapaki.
Hii ni biashara kichaa ya wabongo kuigana
 
Bus za kisasa,anaenda na mda ikiondoka kama imekodiwa na sio daladala,gari nyingi ikizingua dk sifuri nyingi ishakuja ingine kuwafaulisha,uzoefu wa biashara na sio umeuza madini huyo mbio mbio unamwaga mabus.

Waendelee kujifunza kwake maana sio vibaya kujifunza Kwa MTU mwenye uzoefu. Ila Mimi naona Abood yupo Update Kama usemavyo anajua wateja wake wanahitaji nini hana ajali za hovyo n.k
 
Biashara ya mabus sio biashara ya mwekezaji mzuri.
Ni biashara ya kuuzia sura kwa wapenda sifa.wapiga wa kodi zetu na watoa makafara kwao rahisi kupata damu.Au wakurupukaji baada ya kupiga madini au site.
Anaeiba Kodi zetu haoni uchungu kununua mabus au kuendesha bus Kwa Hela ya ofisi.
Ni kama zilivyo daladala nyingi ni za watumishi thus wakistaafu nazo zinapaki.
Hii ni biashara kichaa ya wabongo kuigana
Kweli Kama Abood yupo ccm kimkakati ili Ku-stabilize biashara Zane the same MO alivyokuwa Ccm na wengineo
 
Jamaa alikuwa na convoy sio poa yenye Higer, Yutong, Zhongtong na Scania Polo na ofisi za kisasa

Wachina na Scania walimblacklist, changamoto ilikuwa marejesho

Ukiscroll up message #2 imefafanua vizuri sana
Ndo ya kupiga madini haya umepiga jiwe bilioni kadhaa bank statement ukienda kwa mchina na scania wanakupa business plan ya mabus ya kwenye makaratasi ukiingia field hali ni tofauti
 
Nimesema kwenye uzi mwingine, I'll c&p here:

Biashara ya mabasi ni biashara pasua kichwa kuliko zote.

Scandinavia iliyofanya Mapinduzi kwenye hii sekta ilikufa kifo Cha mende.

Hood imekufa.

Sumry chali.

Sauli yupo hoi siku zake zinahesabika, Achimwene got him in the headlock.

Dar express, Dar Lux, Rungwe waliokuwa powerhouse kwenye hii sekta wote wapo hoi. Etc etc

Turnover kwenye hii sekta ni kubwa mno. Kila miaka miwili wanakuja wengine na kupotea kama upepo household names.

Utasema usimamizi na sababu zote ila sio rahisi kusema hao wote hawajui wanachokifanya. Fanya hii biashara kama unataka kufukia pesa zako.
Daah.... Shabiby kidume sana. Tangu nazaliwa yupo tu.

Naona Zuberi na Najmunisa nao washakufa.
 
Boss umelala nyumbani kwako unasubiri pesa toka kwa anjeti Pana dereva,konda,fundi, traffic, vehicle,mizani,stand,sumatra nk wote nao wanataka kujenga,kula,kunywa,kuhonga kwa pesa Toka Kwa gari yako hawakukusaidia mtaji,mtihani kweli kweli
 
Abood na Shabiby ndio wakongwe pekee waliobaki, zaidi ya miaka 25 kwenye game. Na wanazidi kushusha vyuma vipya. Wakongwe wengine wote walishatupa vitaulo
Umesahau kutaja rangi ya Ngozi ya wamiliki wa basi tajwa. Na wote wapo mjengoni wakiteta na wafanya maamuzi katika Chama. Unategemea nn?
 
Waendelee kujifunza kwake maana sio vibaya kujifunza Kwa MTU mwenye uzoefu. Ila Mimi naona Abood yupo Update Kama usemavyo anajua wateja wake wanahitaji nini hana ajali za hovyo n.k
Hana mpinzani Moro wa kumtoa hayupo,ana Dua la wazee wa kiluguru.
Islam alikuja kapotea kama atakavyopotea BM.
Abood yupo pale pale
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom