daviey69
JF-Expert Member
- Aug 12, 2013
- 2,234
- 866
very nice Dream, Slowly Mungu pamoja nasi na tutafika.Sasa Tanzania imejifunza vitu vingi.
Siasa ni mfumo wa kiuchumi ambso utawainua wananchi husika.
Siasa ya Tanzania kwa nchi za nje kwa miska mingi imekuwa ya ukombozi, ukombozi wa mwafrika toka tawala za kikandamizi za kikoloni.
Hivi karibuni Tanzania imejikuta katika sakata la kuitetea Kongo na wananchi wake walioko mashariki mwa Kongo.
Wananchi hawa kwa miaka mingi wamekuwa katika mlolongo wa matatizo ya kukosa amani na ustawi wa jamii.
Umoja wa mataifa umejaribu kwa miongo mingi tu kuleta amani bila mafanikio.
Lakini ni katika jaribio la mwisho hili la kutumia nguvu kwa kuwashirikisha majirani wa Kongo wenye nia ya dhati kuisaidia, sasa tunaona amani yaweza kurejea mashariki ya Kongo.
Ni wazi kuwaTanzania haina chake ndani ya Afrika Masharikikutokana na hatua za wazi za kutengwa na majirani zetu wa kaskazini.
Lakini akufungiaye njia anakuonyesha mlango mzuri zaidi , hata ni kama wa kuufanyia kazi zaidi.
Ni vema sasa watanzania tukaweka mguu ndani ya Kongo, mguu wa kibiashara, mguu ambao hautaondolewa na tsifa lolote..
Ni muhimu sasa wananchi wa Kongo na Tanzania tukawa wamojs na kuendeleza spirit ya Goma, spirit yz ushirikiani kibiashara sasa.
Kilichobaki ni kuendeleza reli ya kati hadi Kigoma. Na kuanzisha rail ferries hadi mashariki mwa Kongo na kushinikiza wenzetu wa Kongo ku ifungua nchi yso kwa kujenga reli hadi Kinshasa.
Utajiri mkubwa wa Kongo na Tanzania utakuwa kichocheo kikubwa sana katika kujenga reli hii.
I have a dream!!!