Mr George Francis
Senior Member
- Jun 27, 2022
- 186
- 212
Dada Yangu,
Ni kweli wewe ni mzuri sana wa sura, tumekubali.
Ni kweli mwonekano wako na shepu lako linaweza kumvutia kila mwanaume rijali, hili pia tumekubali.
Ni kweli umesoma sana, elimu nzuri na sasa kimtindo kama umejipata hivi!! Aisee!! tumekubali.
Ni kweli umetoka kwenye familia bora, yani baba, mama na ndugu zako wapo vizuri. Hatuna ubishi mwali wangu, tumekubali.
Ni kweli Mungu amekujalia, una kazi nzuri na biashara zako zimekuwa kubwa sana mjini, tumekubali.
Ni kweli umekuwa mcha Mungu na mfuasi mzuri wa dini, hukauki kanisani au msikitini. Hii ni sifa njema sana, tumekubali.
Ni kweli hivi vyote, vinaweza kuwavuta wanaume kutaka kuwa nawe kimapenzi na hata ndoa. Hakuna ubishi, lazima tukubali.
LAKINI, ili kudumu katika ndoa, ni lazima utambue maisha ya ndoa ni zaidi ya hivi vyote. Hapa sasa na wewe itabidi ukubali tu.
Mwanaume anapenda uzuri wako, lakini uzuri huo usiulete ndani mwako.
Mwanaume anapenda mwonekano wako, lakini mwonekano huo usiulete ndani mwako.
Mwanaume anapenda elimu yako, lakini elimu hiyo usiilete ndani mwako.
Mwanaume anapenda sana vile umetoka kwenye familia bora, lakini utajiri wao usiulete ndani mwako.
Mwanaume anapenda sana vile una kazi nzuri na biashara zako zinaenda, lakini zisikufanye ukaleta dharau nyumbani kwako.
Mwanaume anapenda sana vile umekuwa mcha Mungu, lakini kanisa au msikiti visikufanye ukashinda na kukesha huko ukasahau majukumu ya nyumbani kwako.
Neno la Mungu linasema,
"Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana."
Wakolosai 3:18
"Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno."
1 Petro 3:1
Pamoja na sifa na neema zote ulizojaliwa lakini kumbuka kuwa siku zote mwanaume anapenda kuwa mume ndani ya nyumba.
Mwanaume kuwa mume ni yeye kuwa na nguvu, ni yeye kuwa na madaraka na ni yeye kuwa na mamlaka ndani ya nyumba.
Ndio maana neno la Mungu linasisitiza wake kuwa na utii kwa waume zao.
Sifa ulizo nazo zitakufanya upendwe na hata kuolewa lakini sifa hizohizo ndizo zitakazokufanya uachike na kila mwanaume kama utakosa kuwa na utii.
#No_Learning_No_Earning
So we have to Learn.
Prepared By
Mr George Francis
Contact: 0713736006
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Ni kweli wewe ni mzuri sana wa sura, tumekubali.
Ni kweli mwonekano wako na shepu lako linaweza kumvutia kila mwanaume rijali, hili pia tumekubali.
Ni kweli umesoma sana, elimu nzuri na sasa kimtindo kama umejipata hivi!! Aisee!! tumekubali.
Ni kweli umetoka kwenye familia bora, yani baba, mama na ndugu zako wapo vizuri. Hatuna ubishi mwali wangu, tumekubali.
Ni kweli Mungu amekujalia, una kazi nzuri na biashara zako zimekuwa kubwa sana mjini, tumekubali.
Ni kweli umekuwa mcha Mungu na mfuasi mzuri wa dini, hukauki kanisani au msikitini. Hii ni sifa njema sana, tumekubali.
Ni kweli hivi vyote, vinaweza kuwavuta wanaume kutaka kuwa nawe kimapenzi na hata ndoa. Hakuna ubishi, lazima tukubali.
LAKINI, ili kudumu katika ndoa, ni lazima utambue maisha ya ndoa ni zaidi ya hivi vyote. Hapa sasa na wewe itabidi ukubali tu.
Mwanaume anapenda uzuri wako, lakini uzuri huo usiulete ndani mwako.
Mwanaume anapenda mwonekano wako, lakini mwonekano huo usiulete ndani mwako.
Mwanaume anapenda elimu yako, lakini elimu hiyo usiilete ndani mwako.
Mwanaume anapenda sana vile umetoka kwenye familia bora, lakini utajiri wao usiulete ndani mwako.
Mwanaume anapenda sana vile una kazi nzuri na biashara zako zinaenda, lakini zisikufanye ukaleta dharau nyumbani kwako.
Mwanaume anapenda sana vile umekuwa mcha Mungu, lakini kanisa au msikiti visikufanye ukashinda na kukesha huko ukasahau majukumu ya nyumbani kwako.
Neno la Mungu linasema,
"Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana."
Wakolosai 3:18
"Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno."
1 Petro 3:1
Pamoja na sifa na neema zote ulizojaliwa lakini kumbuka kuwa siku zote mwanaume anapenda kuwa mume ndani ya nyumba.
Mwanaume kuwa mume ni yeye kuwa na nguvu, ni yeye kuwa na madaraka na ni yeye kuwa na mamlaka ndani ya nyumba.
Ndio maana neno la Mungu linasisitiza wake kuwa na utii kwa waume zao.
Sifa ulizo nazo zitakufanya upendwe na hata kuolewa lakini sifa hizohizo ndizo zitakazokufanya uachike na kila mwanaume kama utakosa kuwa na utii.
#No_Learning_No_Earning
So we have to Learn.
Prepared By
Mr George Francis
Contact: 0713736006
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com