Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,895
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Kutokana na umri wangu sio rafiki tena. Acha nifupishe. Unapoingia kwenye mahusiano ya mapenzi ambayo unataka yawe serious na au unaingia kwenye ndoa na unataka utulivu. Kuna mambo lazima uyajue na kuyaelewa.
Mambo hayo ni kama ifuatavyo;
1. Hisia hubadilika kulingana na umri, hali, nyakati na mazingira
Kuna hisia za balehe, hisia za ujana, hisia za utu uzima na hisia za uzee. Kinachopelekea hisia kubadilika kutokana na umri ni uzoefu mpya, kubadilika kwa mtazamo na interest. Mkiwa hamna mtoto hisia zenu zinakuwa tofauti na mkiwa na mtoto au watoto.
Sio ajabu ukiwa unabalehe ulikuwa unapenda mabinti wenye sifa fulani lakini sasa hivi haupendi. Halikadhalika na wanawake, katika umri fulani huweza kupenda wanaume wenye sifa fulani lakini wakivuka umri huo hisia hubadilika.
Nyakati zinavyosonga na kubadilika huweza kuzigeuza hisia za mwenza wako au wewe mwenyewe.
Ni vizuri unapochagua mke au mume mtafutane mnaofanana kwa angalau asilimia 75% kama lengo lenu ni kuzikana.
2. Pesa humpa Mwanamke nguvu kubwa kama hatakuwa na hekima ndoa kuvunjika ni 90% uhakika
Mwanamke kama anakupenda hata awe na pesa atakuwa mtiifu kwako. Lakini hoja ya kwanza inaeleza kuwa hisia hubadilika. Vipi kama hisia zake zikibadilika katika umri, hali, nyakati au mazingira fulani.
Taikon kama Mastermind, Multiplayer na kionambali. Ninakuambia Ogopa Mwanamke abadilike hisia zake akiwa na nguvu, naam namaanisha Pesa. Ni hatari. Kuna namna nyingi za kudili na jambo hili. Hii ni mada ya siku nyingine.
Kwa upande wa mwanaume kinachompa nguvu zaidi ni afya yake hasa nguvu za kiume. Mwanaume hata awe bilionea au tajiri namba moja kama hana nguvu za kiume hawezi kumwongoza Mwanamke, hana hiyo Mamlaka.
Utagundua kuwa kila mmoja hutafuta ulinzi utakaomfanya kuwa na nguvu. Mwanamke hutaka pesa. Wakati mwanaume hutaka abaki na nguvu zake za kiume ili azidi kuheshimiwa.
3. Mtu anauwezo wa kupenda zaidi ya mara Moja ingawaje hatakuja kupenda kama pendo la kwanza
Huyo unayemtesa na kumringia anauwezo wa kukuacha na kumpenda mtu mwingine kabisa na akakusahau kabisa. Moyo wa binadamu umeumbwa ku-renew hisia za upendo zaidi ya mara moja.
4. Mwanamke anapotoa pesa nyumbani ni ishara ya kukupenda kuliko, lakini pia hiyo ni kumbukumbu ambayo ataitumia huko baadaye.
5. Mwanamke hupenda surprise ya vitu vizuri kuliko ahadi. Ingawaje ahadi humpa faraja. Elewa pia Mwanamke faraja ni moja ya kile akiitacho maneno Mazuri.
6. Elewa, Mwanaume hapendi Surprise. Hii ní Kwa sababu mwanaume kiasili hujiona ni mtawala, na watawala hupenda taarifa mapema na sio mambo ya kushtukiza.
Ni rahisi kumfurahisha Mwanamke kwa kum-surprise kwa zawadi ya Gari au kiatu. Lakini ukifanya hivyo kwa mwanaume ni nadra sana kufurahia.
7. Mwanamke anapenda kusifiwa wakati mwanaume anapenda kutukuzwa
Usipompa Mwanamke sifa yeye hawezi kukutukuza. Kama mjuavyo utukufu ni wa Mungu. Lakini mwanaume kwenye hii dunia ndiye mungu mdogo. Mkeo akutukuze itakupasa umsifie na uhakikishe anapewa sifa huko nje. Hapo itahusisha huduma na kumtunza.
Elewa kuwa, Mwanamke akikupenda na ukamhudumia na kumtunza anakuona mungu wake. Atakutii kwa kila kitu kuliko hata Mungu wake. Ndio maana ikasemwa kuwa Mwanaume atamtawala Mwanamke. Lakini sio jambo la bure isipokuwa kuna gharama lazima mwanaume ulipie ili upate kumtawala Mwanamke.
8. Mwanamke atachepuka kwa sababu mbili tuu;
Moja, Kisasi. Hapa uwe umemuumiza vya kutosha na huonyeshi kujali na unamdharau.
Haishauriwi uki-cheat Mwanamke akukamate red-handed.
Pili, Hisia zake kuhama, hisia za Mwanamke zinajengeka polepole. Mwanamke hawezi kukupenda kwa siku moja. Halikadhalika kama alikuwa anakupenda hisia hupotea polepole. Mwanamke hana huo uwezo wa kukuondoa moyoni mwake kwa siku moja.
Mwanamke aliyeachwa kwa ghafla na Ex wake kabla hisia zake hazijahama alafu wewe ukaja ukawa naye ni rahisi sana kurudiana na Ex wake. Tofauti na Mwanamke waliyekuwa wanasumbuana kwa muda mrefu na Ex wake.
Ili Mwanamke aku-cheat atahitaji sababu, na sababu ni hizo mbili. Pesa ni Geresha tuu.
Sababu za mtu ku-cheat nyingi na kuu ni internal factors na sio external factors.
Acha nipumzike sasa.
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es salaam.
Mtibeli.
Kutokana na umri wangu sio rafiki tena. Acha nifupishe. Unapoingia kwenye mahusiano ya mapenzi ambayo unataka yawe serious na au unaingia kwenye ndoa na unataka utulivu. Kuna mambo lazima uyajue na kuyaelewa.
Mambo hayo ni kama ifuatavyo;
1. Hisia hubadilika kulingana na umri, hali, nyakati na mazingira
Kuna hisia za balehe, hisia za ujana, hisia za utu uzima na hisia za uzee. Kinachopelekea hisia kubadilika kutokana na umri ni uzoefu mpya, kubadilika kwa mtazamo na interest. Mkiwa hamna mtoto hisia zenu zinakuwa tofauti na mkiwa na mtoto au watoto.
Sio ajabu ukiwa unabalehe ulikuwa unapenda mabinti wenye sifa fulani lakini sasa hivi haupendi. Halikadhalika na wanawake, katika umri fulani huweza kupenda wanaume wenye sifa fulani lakini wakivuka umri huo hisia hubadilika.
Nyakati zinavyosonga na kubadilika huweza kuzigeuza hisia za mwenza wako au wewe mwenyewe.
Ni vizuri unapochagua mke au mume mtafutane mnaofanana kwa angalau asilimia 75% kama lengo lenu ni kuzikana.
2. Pesa humpa Mwanamke nguvu kubwa kama hatakuwa na hekima ndoa kuvunjika ni 90% uhakika
Mwanamke kama anakupenda hata awe na pesa atakuwa mtiifu kwako. Lakini hoja ya kwanza inaeleza kuwa hisia hubadilika. Vipi kama hisia zake zikibadilika katika umri, hali, nyakati au mazingira fulani.
Taikon kama Mastermind, Multiplayer na kionambali. Ninakuambia Ogopa Mwanamke abadilike hisia zake akiwa na nguvu, naam namaanisha Pesa. Ni hatari. Kuna namna nyingi za kudili na jambo hili. Hii ni mada ya siku nyingine.
Kwa upande wa mwanaume kinachompa nguvu zaidi ni afya yake hasa nguvu za kiume. Mwanaume hata awe bilionea au tajiri namba moja kama hana nguvu za kiume hawezi kumwongoza Mwanamke, hana hiyo Mamlaka.
Utagundua kuwa kila mmoja hutafuta ulinzi utakaomfanya kuwa na nguvu. Mwanamke hutaka pesa. Wakati mwanaume hutaka abaki na nguvu zake za kiume ili azidi kuheshimiwa.
3. Mtu anauwezo wa kupenda zaidi ya mara Moja ingawaje hatakuja kupenda kama pendo la kwanza
Huyo unayemtesa na kumringia anauwezo wa kukuacha na kumpenda mtu mwingine kabisa na akakusahau kabisa. Moyo wa binadamu umeumbwa ku-renew hisia za upendo zaidi ya mara moja.
4. Mwanamke anapotoa pesa nyumbani ni ishara ya kukupenda kuliko, lakini pia hiyo ni kumbukumbu ambayo ataitumia huko baadaye.
5. Mwanamke hupenda surprise ya vitu vizuri kuliko ahadi. Ingawaje ahadi humpa faraja. Elewa pia Mwanamke faraja ni moja ya kile akiitacho maneno Mazuri.
6. Elewa, Mwanaume hapendi Surprise. Hii ní Kwa sababu mwanaume kiasili hujiona ni mtawala, na watawala hupenda taarifa mapema na sio mambo ya kushtukiza.
Ni rahisi kumfurahisha Mwanamke kwa kum-surprise kwa zawadi ya Gari au kiatu. Lakini ukifanya hivyo kwa mwanaume ni nadra sana kufurahia.
7. Mwanamke anapenda kusifiwa wakati mwanaume anapenda kutukuzwa
Usipompa Mwanamke sifa yeye hawezi kukutukuza. Kama mjuavyo utukufu ni wa Mungu. Lakini mwanaume kwenye hii dunia ndiye mungu mdogo. Mkeo akutukuze itakupasa umsifie na uhakikishe anapewa sifa huko nje. Hapo itahusisha huduma na kumtunza.
Elewa kuwa, Mwanamke akikupenda na ukamhudumia na kumtunza anakuona mungu wake. Atakutii kwa kila kitu kuliko hata Mungu wake. Ndio maana ikasemwa kuwa Mwanaume atamtawala Mwanamke. Lakini sio jambo la bure isipokuwa kuna gharama lazima mwanaume ulipie ili upate kumtawala Mwanamke.
8. Mwanamke atachepuka kwa sababu mbili tuu;
Moja, Kisasi. Hapa uwe umemuumiza vya kutosha na huonyeshi kujali na unamdharau.
Haishauriwi uki-cheat Mwanamke akukamate red-handed.
Pili, Hisia zake kuhama, hisia za Mwanamke zinajengeka polepole. Mwanamke hawezi kukupenda kwa siku moja. Halikadhalika kama alikuwa anakupenda hisia hupotea polepole. Mwanamke hana huo uwezo wa kukuondoa moyoni mwake kwa siku moja.
Mwanamke aliyeachwa kwa ghafla na Ex wake kabla hisia zake hazijahama alafu wewe ukaja ukawa naye ni rahisi sana kurudiana na Ex wake. Tofauti na Mwanamke waliyekuwa wanasumbuana kwa muda mrefu na Ex wake.
Ili Mwanamke aku-cheat atahitaji sababu, na sababu ni hizo mbili. Pesa ni Geresha tuu.
Sababu za mtu ku-cheat nyingi na kuu ni internal factors na sio external factors.
Acha nipumzike sasa.
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es salaam.