Bila ushahidi kwamba kweli alifeli itabaki kuwa ni maneno yako tu hadi hapo utakapotoa ushahidi kwamba kweli alifeli hicho kimtihani.
Unamzungumzia Palamagamba Kabudi? Yule genius wa sheria aliyepata festi klasi (ya sheria) ambayo huwa tunaambiwa na
Pasco humu kuwa ndo ngumu kupatikana katika kozi/fani zote zinazofundishwa hapo UDSM....yaani unasema kwamba huyo bwana licha ya kupata festi klasi hapo UDSM baadaye alikuja akakacha kufanya hicho kimtihani cha uwakili kwa sababu ni kigumu sana?
Yaani huyo genius akaogope hako kamtihani? Hiyo habari wewe umeitoa wapi? Manake huyo bwana ni mjumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba na kwenye tovuti ya hiyo tume kuna kiji-profile cha wajumbe kinachoelezea elimu pamoja na tajiriba zao na ya huyo bwana Kabudi inasomeka hivi:
Sasa bwana Mbeky naomba unieleze hapo nilipopakoleza na maandishi mazito yenye rangi nyekundu panamaanisha nini. Kuwa advocate of the high court of appeal of Tanzania huhitaji kufanya hako kamtihani?
Halafu naomba unieleze ni imekuwakuwaje hadi jina lake huyo bwana Kabudi kutokea kwenye roll of advocates na yeye akiwa roll namba 1169 na tarehe yake ya admission ni 15.12.2009.
Kwa chanzo bofya
hapa. Hii roll inaishia 2009 tu.
Ukiboko wake ni nini?