CV ya Mwanasheria mkuu wa Serikali Jaji Stephen Werema

CV ya Mwanasheria mkuu wa Serikali Jaji Stephen Werema

ni jaji na pia ni mwanasheria mkuu wa serikali ila jana matumizi ya neno "shall" na "may" kwa mujibu wa sheria za nchi yamempga chini.

Hizo modal verbs husumbua (wanasheria) wengi na si yeye tu. Tushawahi kuwa na kamjadala kule kwenye jukwaa la sheria kuhusu hizo verbs hususan kwenye sheria za kazi.
 
Kiukweli; wataalam wengi walioko serikalini ni wasomi kama huyu bwana, wamepotea tu pale ambapo wameshindwa kuelewa nini ilikuwa kazi yao ya msingi na kujikuta wakishabikia na kutetea chama tawala. Hii imeonekana sana baada tu ya mfumo wa vyama vingi kuingia, na serikali kwa kutambua hilo imekuwa ikiwatumia watu kama hao kwa kutekeleza mambo yake.

wakijitambua hata serikali itawashukuru pia kwa kuishauri vema kuliko kuwa tu ndiyo mzee na baadaye wanajikuta wanahaha kubariki uovu uliotendeka ama unaoelekea kutendeka.

Wapi report ya pesa za uswiss na new jersey? Weerema huyohuyo alisema anaifanyia kazi ni hadi lini!!!!!
 
Mwaka 2011 nilishawahi kusema huyu mtu uwezo wake ni mdogo sana na nikasema kuna haja ya kupitia kwa kina hukumu alizotoa akiwa jaji.Ni lazima atakua alitoa hukumu kandamizi au zenye upendeleo

Tukileta CV yake ili ikamilike nadhani na nukuu zake alizowahi kutoa ziwekwe ili kuitendea haki CV hii nzito iliyosheheni usomi na experience!
Wewe uwezo wako mbona ndiyo wa ajabu kabisa hata haufiki wa ......
 
Ni kweli alifeli mtihani wa uwakili (bar exam)
Source ; kwa mujibu wa rafiki ake wa karibu LAU masha former Waziri wa mambo ya ndani
Ya kweli hayo au kwa vile tu hamumpendi na kwa vile mnadhani ni kilaza basi ndo mnaamua kumzushia?

Mtu aliyekuwa attorney general advocate (what hell is that even?) iweje afeli mtihani wa uwakili? Na kwani mtihani wa uwakili ni mgumu kuliko miaka 4 aliyosomea sheria hapo UDSM?
 
Last edited by a moderator:
Limesomeshwa na pesa za walipa kodi na sasa anatumikia mafisadi.
duh mkuu wewe ni noma? mbona hasira hivi? wazee wote waliosoma wa level hiyo au umri huo wamesomeshwa na serikali sio ajabu baba yako ni mmojawapo!
 
Ni kweli alifeli mtihani wa uwakili (bar exam)
Source ; kwa mujibu wa rafiki ake wa karibu LAU masha former Waziri wa mambo ya ndani

Lau Masha kajuaje? Yeye ndo alisahihisha mtihani wake? Na Masha alisema hivyo lini na wapi? Yupo on record akisema hivyo au alibwatuka akiwa keshakunywa pombe Rose Garden?
 
Mdau bar exam ilikuaga ni oral exam afu ilikua haina kificho maana mwisho wa siku watu walifaulu wanaapishwa in public
Lau Masha kajuaje? Yeye ndo alisahihisha mtihani wake? Na Masha alisema hivyo lini na wapi? Yupo on record akisema hivyo au alibwatuka akiwa keshakunywa pombe Rose Garden?
 
anaiaibisha shule yangu ya ENGINEERS bwiru boys tech. sec. school..
 
Mwaka 2011 nilishawahi kusema huyu mtu uwezo wake ni mdogo sana na nikasema kuna haja ya kupitia kwa kina hukumu alizotoa akiwa jaji.Ni lazima atakua alitoa hukumu kandamizi au zenye upendeleo

Tukileta CV yake ili ikamilike nadhani na nukuu zake alizowahi kutoa ziwekwe ili kuitendea haki CV hii nzito iliyosheheni usomi na experience!

mkuu umechemka, hujaiona hiyo LLM? Si ni ya chuo kile cha masters ya Lukuvi and the like!
 
Mdau bar exam ilikuaga ni oral exam afu ilikua haina kificho maana mwisho wa siku watu walifaulu wanaapishwa in public

Yeye AG alifanya hiyo exam mwaka gani? Na mtu kwa Tanzania anapewa attempts ngapi?

Bado haiingii akilini kwamba jamaa aliyefeli hicho ki-exam eti ndo aje kuwa judge na AG....haingii akilini kabisa.

Na bado siamini hadi nipate sources zingine zaidi ya watu tu humu (tena wenye chuki dhidi yake) kusema bila supporting evidence.

Kuna website moja hivi ina orodha ya mawakili wote wa Tanzania. Ngoja niitafute niangalie kama yupo...walau hapo nitakuwa nimepata pa kuanzia.
 
Tunataka na ya mnyampaa ANTFAS MGHWARY LISU ili tuingie kwenye mjadala
 
Yeye AG alifanya hiyo exam mwaka gani? Na mtu kwa Tanzania anapewa attempts ngapi?

Bado haiingii akilini kwamba jamaa aliyefeli hicho ki-exam eti ndo aje kuwa judge na AG....haingii akilini kabisa.

Na bado siamini hadi nipate sources zingine zaidi ya watu tu humu (wenye chuki dhidi yake) kusema bila supporting evidence.

Kuna website moja hivi ina orodha ya mawakili wote wa Tanzania. Ngoja niitafute niangalie kama yupo...walau hapo nitakuwa nimepata pa kuanzia.

Kweli watu ni wakeleketwa...website yako unayoiamini hujaitafuta bado unapinga..ukikuta ni kweli cv yake iko sahii utaikana comment yako.
 
Kweli watu ni wakeleketwa...website yako unayoiamini hujaitafuta bado unapinga..ukikuta ni kweli cv yake iko sahii utaikana comment yako.

Kinachonifanya nipinge ni mantiki. Wewe mtu keshakuwa jaji, na sasa ni mwanasheria mkuu. Halafu eti tunaambiwa alifeli kimtihani cha uwakili.

Hata kama Tanzania ni nchi ya hovyo hovyo lakini bado siamini kama kweli tunaweza kuwa hovyo kiasi hicho.

Leteni ushahidi kwamba kweli alifeli hicho kijimtihani.
 
Kinachonifanya nipingi ni mantiki. Wewe mtu keshakuwa jaji, na sasa ni mwanasheria mkuu. Halafu eti tunaambiwa alifeli kimtihani cha uwakili.

Hata kama Tanzania ni nchi ya hovyo hovyo lakini bado siamini kama kweli tunaweza kuwa hovyo kiasi hicho.

Leteni ushahidi kwamba kweli alifeli hicho kijimtihani.

Hakika hata mimi Nyani Ngabu naungana nawe ku doubt hili kabisa na nina uhakika halina ukweli.
 
Last edited by a moderator:
Sio tunajadili mambo ya wazee wetu tu! ambao kiukweli wanatukwamisha sana sana, hasa baada ya kuingia kwenye siasa na kusahau umuhimu wa elimu zao kwa maendeleo ya taifa. Sasa nasi vijana ambao wengine tayari mmeingia kwenye mkumbo huo huo kama wazee wetu walivyofanya, tujiulize, je? watoto wenu nao si watawapigia kelele hizo hizo? au ndio nyani haoni kundule? Ningependa sisi vijana tuikomboe hii nchi, tuwe tofauti na wazee wetu, mbona inawezekana tu!
 
mmmh Mungu tusaidie na Tanzania yetu manake without your intervention we shall all be perished with this CCM regime.
 
CV za kusoma ni mbwembwe hasa hasa kwenye mfumo Elimu ambao lengo lake ni kutoa msomi mwenye mawazo tegemezi. Refer kwenye objectives and aims of "Colonial Education", hata baada ya uhuru mfumo haukabadilishwa bali tulibadilishiwa content tu, mbaya zaidi tukakewekewa "Unyerere." So sishangai kwa CV hii bado Werema akawa hivyo alivyo ni mfumo, kuna watu wana uwezo wa "kufaulu" mitihani lakini IQ yao ni ndogo sana. Na viongozi waliotufikisha hapa wote wana CV zilizotukuka lakini wameboronga mwanzo mwisho.
So kwa Werema and etal tusishangae madudu ndivyo walivyo, mfumo uliwabeba na sasa na hizi Division 5 watafyatua Kina Werema, Mulugo wakutosha.

Mkuu Pukudu, Unyerere ndio unini ?
 
Last edited by a moderator:
mimi binafsi namfahamu Werema tangu akiwa wakili ofisi ya mwanasheria mkuu, tulikuwa wote wajumbe wa Bodi ya chuo Cha DIT yeye akiwakilisha ofisi ya mwanasheria mkuu na mimi nikiwakilisha wanachuo kwa maana ya rais wa chuo.. tulikuwa na mgogoro mkubwa sana wa kisheria pale chuoni kati ya mwaka 2003 hadi 2005 ambao mimi binafsi nilimlaumu kushindwa kuonyesha mchango wake kama mwanasheria kwa tatizo ambalo lilikuwa wazi la kukiukwa sheria iliyokianzisha chuo hicho kwa miaka mingi.

nilishangaa sana baada ya Werema kuchaguliwa kuwa mwanasheria mkuu wa serikali kwa kuwa naujua vizuri uwezo wake wa kushughulikia masuala ya kisheria hasa katika mazingira yenye mvutano wa pande kadhaa.

sijawahi kuwa na imani naye kutokana na ninavyomfahamu.
 
anaiaibisha shule yangu ya ENGINEERS bwiru boys tech. sec. school..

mkuu afadhali wewe anakuaibisha kwa shule tu! mie mkuu ni zaidi kwani mbali ya kusoma Bwiru boys tunatoka nalo mkoa mmoja na kabila moja kasoro wilaya tu. Kwa kweli kuna kipindi huwa naona aibu kusema huyu mkurya muoga na manafiki ni kabila yangu. lakini hivi huyu jamaa kweli ni Mura? nina mashaka na ukurya wake!
 
Back
Top Bottom