CV ya Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu (Mr II)

CV ya Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu (Mr II)

Elimu mliyonayo mnajua iliandaliwa na watu gani? Hapo Mwanzo hakukuwa na darasa wala chuo na si miaka mingi sana, na hao waliobuni mambo haya na kuweka mifumo na taratibu hizi walikuwa kama Sugu tnea labda chini ya hapo kwa kipimo mnachotaka. Ni hivi, ufahamu wa mtu, hekima zake, busara zake, uwezo wa kuwasilisha kile anacho jua na kukiamini na kuwashawishi wingine kuwa ni kweli na kinawezekana, na kuweza kushiriki katika kuona kuwa kinatekelezeka ni elimu zaidi ya Profesa anaehubiri darasani na ukimpa Idara ya maendleo au shirika au wizara unashindwa kujua tofauti.

Tutapia uwezo wako kwa kile unachoonyesha kwenye jamii si kwa elimu uliyosoma darasani halafu unaishia kulalamika kunungúnika kila kitu unataka uwe umeandaliwa wewe ukija unakula tu, ikiwemu kuilaumu serikali, wazazi na jamii. Hiyo ni dalili ya kuwa umesoma lakini huna upeo yaani huna uwezo wa kuona opportunities au kucreate opportunitites. Kwa nyinyi mnaokaaa mjini nendeni kule vijijini makone vijana wanavyotengeneza pesa na wanaishi maisha so natural. Nyinyi mnaita maisha duni kwasababu ya televission ya mzungu, ila ikifika wakati mnaambiwa na Daktari unatakiwa ule hivi au utembee sana au usilale kwenye kitanda hiki ndo unashtuka alah kumbe wale jamaa wanaishi maisha mazuri zaidi kuliko sisi?

Mtizamo ni kitu muhimu sana katika kumjudge mtu, na kukurupuka bila kumpima ni udhaifu mbaya sana. amini usiamini mimi naweza kuwa nimesoma sana, lakini nikienda kijijini kuongea na wenyeji huwa kila siku najifunza mambo mapya kabisa mbayo sikuwa nayafahamu, na wenig wao hawajaenda shule kama mimi au kwenda ulaya na kwingineko.

Tutatumia vigezo vyako vya performance shuleni kama tunataka uwee mwalimu, na hilo halina ubishi, ila mara nyingi tumekuwa tukiwaalika watu kutoa mada na lecrure kwa wanafunzi si kwasababu ni ma-profesa au wana degree, la ila kwasababu ya ujuzi walioupata katika maisha na wakiongea uzoefu na ujuzi wao, mnaweza kuona kabisa jambo linalofaa kuimarisha katika elimu yenu.
 
CV Dhaifu sana hii kwa mtu kuongoza jiji la Mbeya. Hapa tusitegemee maendeleo yoyote.
Tafadhali nifafanulieni hiyo Self Employed = Celebrity ndo kazi gani? Kwa English yangu ya Form II nakumbuka Celebrity ni MTU MASHUHURI/ MAARUFU.
 
CV Dhaifu sana hii kwa mtu kuongoza jiji la Mbeya. Hapa tusitegemee maendeleo yoyote.
Tafadhali nifafanulieni hiyo Self Employed = Celebrity ndo kazi gani? Kwa English yangu ya Form II nakumbuka Celebrity ni MTU MASHUHURI/ MAARUFU.

Unajua mambo anyowafanyia watu wa Mbeya!!? Je Unafahamu chochote kuhusiana na uwezo wake wa kujenga hoja na kushawishi!? (soma vizuri Autobiography yake utabaini uwezo wa huyu jamaa ni zaidi ya Phd holder kwa hustling alizopitia) Mbeya inapiga hatua sasa na mchango wa huyu jamaa unaonekana dhahiri...Karibu Mbeya.
 
CV Dhaifu sana hii kwa mtu kuongoza jiji la Mbeya. Hapa tusitegemee maendeleo yoyote.
Tafadhali nifafanulieni hiyo Self Employed = Celebrity ndo kazi gani? Kwa English yangu ya Form II nakumbuka Celebrity ni MTU MASHUHURI/ MAARUFU.

...Ndugu yangu hivi kuwa mwanasiasa unatakiwa uwe na elimu ya kiwango gani? Kwani nchi ye2 tatizo siyo kiwango elimu bali uwepo wa watendaji na wasimamizi wabovu, wenye kujawa na tabia ya wizi, choyo uwongo, chuki, unafiki na tamaa. Ebu! tumrejee Mh. Karamagi, Idi Simba, Pr. S. Mbilinyi, Rais Mstaafu Mkapa, Mangula, Lowassa, na wengineo. Hawa ni miongoni mwa wale wenye elimu ya juu tena rasmi lakini ndiyo walio saini MIKATABA MIBOVU inayoitesa nchi na watu wake. Hapa cha msingi tuzingatie elimu kwa watendaji na siyo wanasiasa, wao tuzingatie uwezo wa kutoa hoja na kuisimamia kwani wapo wenye elimu unayoibeza na wana hoja nzuri za kujenga kuliko hao wasomi wetu wanaokesha kukariri Kiingereza ambacho uambulia patupu kama Mh. Mulugo, badala kujiimarisha kimaarifa.
 
Uadilifu haupimwi kwa ukubwa wa elimu tu. Ukiwa muadilifu hata ukiwa huna elimu utabakia na uwezo wa kuongoza kwa haki na heshima kwa wananchi. Wapo waliosoma na wakawa mafisadi wa mali za umma kwa ufannisi mkubwa, wapo walioongoza nchi wakiwa hawana elimu lakini wakawacha legacy kubwa ya uadilifu.

Criteria ya uongozi ni UADILIFU, elimu ni nyenzo tu ya kukupa uwezo wa kukabili changamoto kwa urahisi.
 
Mimi Nashauri wale ambao wana wasiwasi na Elimu ya Sugu wananunue kitabu chake kinachoeleza historia ya maisha yake, halafu hata sisi tunaochangia humu jamvini tujilinganishe na Sugu tuone ni wangapi ambao tuna uwezo kama wa Sugu kimatendo achana na vyeti ambavyo tumejaza kwenye makabati.
Fikiria huyu jamaa hadi ameweza kutoa kitabu japo cha maisha yake wangapi humu ndani tuna uwezo huo, Mh. Karume (marehemu) kule Zanzibar aliweza kujenga majengo ambayo hadi leo ni historia na hakuwa Mhandisi na yeyey mwenyewe ndiyo alisimamia ujenzi. Suala la Elimu hapa si vyeti ni nanmna mhusika anavyoweza kujipambambanua katika kutatua matatizo yake na jamii inayomzunguka
 
Your very very right!! Kwani sifa kubwa ya kiongozi lazima afanane na wapiga kura wake!!! hasa ukizingatia mh Sugu (Kama walivyo wabunge wengine) kwa mbeya yeye ndiye 1st citizen wengine wote wanafuata nyuma yake, na kwa msingi huo yeye ndiye mwenye nafuu hakukuwa na mbadala wake

Kiingereza chako tu kimekuvua nguo na kukuonyesha hadharani kuwa ni mtu unaefanana na mawazo yako. Ahsante kwa mtazamo wako juu ya watu wa Mbeya
 
Amesoma O-level miaka miwili (2), na amewahi fanya kazi kama 'celebrity'!

O level muhula wa kwanza uanzia January na wa pili uishia November

Form 1 - 1988
Form 2 - 1989
Form 3 - 1990
Form 4 - 1991

Sasa hiyo miaka miwili unayoiongelea sijui ni ipi!?
 
O level muhula wa kwanza uanzia January na wa pili uishia November

Form 1 - 1988
Form 2 - 1989
Form 3 - 1990
Form 4 - 1991

Sasa hiyo miaka miwili unayoiongelea sijui ni ipi!?
Mkuu upo sàhihi kabisa wa TZ wengine wanakurupuka,iko hivi
1988-1990 form 1 mpaka form 3 muhula wa kwanza MBEYA SEC
1990-1991 form 3 muhula wa pili mpaka form 4 SABASABA SEC sasa cha ajabu nini hapo!!
 
93 Niko Boarder naitafuta South africa leo hii najichanganya tu america ndivyo maisha yanachange leo ndani ya terrano kesho vx au range,nafika mpaka barmaco sio tu san fransisco huko kote nafika ktk kutafuta mshiko wanga huko na kule nawapa dole la kati ni nani?? Suguuuuu na nani? Ni weweeeeee tuuuu talanlanlalalaaaaaaa ni moto chini.

"Waweruu" (ndio inavyoitikiwa baada ya kuuliza hapo kwenye red) huyo jamaa alikuwa naye UK kipindi hicho anafanya kazi na "Social Misfit ya Waweru"

Mzazi ulikuwepo Diamond wakati inazinduliwa hii kitu "Mziki na Maisha"??
 
Huo utakua ni unyanyapaa ni wabunge wengi na watendaji wengi wa serikali tena sehamu zingine ni sekta nyeti utawakuta darasa la saba kigezo ni weledi na umakini katika utendaji wa kazi mi nafikiri tungepata hansard za bunge tuone ni wabunge wangapi tangu wameingia bungeni mpaka sasa hawajachangia chochote harafu tunawaita wasomi. Kuwa na elimu kubwa sio kigezo cha kuleta maendeleo ila ni ile hari ya uthubutu na kujiamini. Kwa kua kwetu Dodoma mjini ningepanda tumjadili na huyu mbunge wa Dodoma mjini. Sijawahi kumsikia hata siku moja wagogo wanadhulimiwa viwanja na mashamba yao na CDA hata siku moja sijasikia akiwatetea. Binafsi Sugu ni Jembe ambalo linawakilisha watoto wa maskini ambao hata kupata Elimu kwny maisha yao likua shida. nakumbuka nyimbo yake ya zamani sana inaitwa Hali halisi. Je mafanikio ya Bakheressa yanawiana na Elimu yake?
 
Huyu hana shida amesema ukeli wake hata katika kitabu chake cha Sugu ameeleza yote. Vipi wenye elimu bandia za Proffesor, Dr nk!
La Saba tunaweza.
 
Raisi wa Mbeya, BIG up Sugu!!

JK mwenyewe kaachwa mbaali sana kwa upeo na sugu.
 
Back
Top Bottom