CV ya Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu (Mr II)

CV ya Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu (Mr II)

Siyo kila mawazo ya kuanzishia thread bhana,fanya upembuzi yakinifu au ujifunze kwa wengine,no research no right to speak
 
Huo utata uko wapi sasa? kuna siku amekwambia kua ana elimu zaidi ya hiyo unayoijua? muache Sugu wa watu apumuwe!
 
Last edited by a moderator:
nimefuatilia sana michango ya sugu akiwa bungeni na katika jamii kwa ujumla nimeona kuwa michango mingi ya mbilinyi huwa siyo ya kiwered sana bali huwa ni michango iliyokaa kimzaha na kuchekesha,niliwaza sana lakini nikabaini kuwa kunatatizo la elmu alilonalo ikumbukwe kuwa sugu alifukuzwa mbeya sec kwa utovu wa nidhamu na historia haioneshi kama alisoma shule yoyote hapa nchini baada ya kufukuzwa mbeya sec
mulugo with fake ID
 
shida kubwa ni hizi sifa za watu kuwa wanasiasa. panahitajika mjadala mkubwa ili wabunge wawe na viwango maalum vya elimu. haitoshi kwa mtu kujua kusoma na kuandika tu. matokeo yake tunapata watu wa design ya akina sugu. hata wanapotoa michango yao bungeni inakosa mvuto na inakposa kuwa na tija

Mbona hamuwachafui wa CCM ambao wako wengi sana waliomaliza darasa la saba na wengine wameforge vyeti vyao?Tuanze na Lusinde,Prof.Maji Marefu.Tusitafute undani wa mtu bali anachokizungumza bungeni kina faida kwa taifa letu.Kwa nini tuongee kuhusu maisha ya mtu binafsi sababu tu ni mpinzani?Angalia elimu uliyonayo imeisaidiaje taifa lako,kama haijaisaidia basi hauna tofauti na huyo aliyemaliza darasa la saba.
 
Hauwezi kuona utata huo kwa vile CHADEMA nzima wako hivyo kuanzia Mwenyekiti, Katibu mkuu, Mkurugenzi wa uenezi na wengine wengi, kwa hiyo huwezi kuona utata kwa sugu kwa vile ni mtu mdogo sana.

Hauwezi kutoa hoja mpaka uwataje viongozi wa CHADEMA.Toa hoja kulingana na kinachosemwa.Pili watanzania tuna mambo mengi ya kujadiliana kuhusu mustakabali wa maisha yetu na siyo kuhusu maisha ya watu.Angalizo,ukiongelea sana ya watu nyuma yako kuna watu wanaongea vibaya zaidi kuhusu wewe.Tuache kushabikia mambo ya watu.
 
Huna data za kutosha unakimbilia kuanzisha thread, sugu alishaweka wazi elimu yake na historia nzima ya maisha yake kwenye kitabu kiitwacho MUZIKI NA MAISHA - SUGU the autobiography! Namfahamu SUGU ni real, hana haja ya kufoji vyeti. Na wanambeya wanamkubali kuliko hata kikwete!

View attachment 88079
 
Sugu kapata ubunge kwa jina lake na tukumbuke nyimbo zake zilikaa kiharakati zaidi kwa mtu wa kawaida hivyo michango yake bungeni mlengwa ni mtu wa kawaida sio ninyi ambao mna weredi na elimu za juu.
Hapa ndipo wasomi watanzania wanapokosea, kama ni waandishi wanashindana kwa weredi kuandika bila kujua kwamba mtu wa kawaida itamchukua mda mrefu kuelewa maudhui. Nnamdi Azikiwe alikuwa msomi toka marekani lakini alipoingia nigeria ili aeleweke kwa mtu wa kawaida alianzisha gazeti lenye kuandika kwa lugha nyepesi kuhamasisha uhuru wa nchi nyingi tu za afrika magharibi. Watu walilipenda kuzidi yaliyokuwepo tayari wakati huo
 
nimefuatilia sana michango ya sugu akiwa bungeni na katika jamii kwa ujumla nimeona kuwa michango mingi ya mbilinyi huwa siyo ya kiwered sana bali huwa ni michango iliyokaa kimzaha na kuchekesha,niliwaza sana lakini nikabaini kuwa kunatatizo la elmu alilonalo ikumbukwe kuwa sugu alifukuzwa mbeya sec kwa utovu wa nidhamu na historia haioneshi kama alisoma shule yoyote hapa nchini baada ya kufukuzwa mbeya sec

Toka nimeanza kusikiliza bunge sijaona kibaya alichosema Sugu.Hebu tupe na upande wa pili ambao hutoa matusi huko bungeni badala ya ku-argue kwa kutumia hoja,unawaweka wapi?Kama hauwezi kuwaponda mawe wabunge na viongozi ambao wamesoma lakini elimu yao haijaifaidisha taifa basi usirushe mawe upande wa pili.

Kuna viongozi wamesomeshwa bure kuanzia chekechea mpaka vyuo vikuu na walichokifanya ni kufilisi taifa letu kwa kujilimbikizia mali na kuuza maliasili zetu.Mara elfu huyo sugu ambaye anatoa michango bungeni inayowakilisha watu wa jamii fulani.
 
Hebu tuambie michango ya Chenge Bungeni aliye soma Harvad, Wabongo tumekalia ana ishu za Vyeti, Nchi kama USA walio ifikisha hapo ilipo hawakuwahi kwenda shule watu kama Thomas Edson, Mchael Dell, wakina BILL hawajaenda shule ila ndo walio ibadili USA, huku tunakomaa na vyeti,

Tanzania tutakuja kubadilika tukiachana na elimu za vyeti

Kutoenda shule ukiwa unamaanisha nini? Unataka kutuambia hao uliowataja hawajakanyaga shule kabisa? Hivyo vitu wanavyovifanya wameoteshwa?
 
Tume ya uchaguzi ilifanya kazi yake,wananchi wa Mbeya pia walifanya kazi yao.Sheria zipo wazi,kama kulikuwa na kasoro yoyote nafasi ya pingamizi ilikuwapo.Tujadili ni jinsi gani tutaweza kujinasua kwenye lindi la umasikini,tuache maneno mepesi yaliyopitwa na wakati.
 
Kutoenda shule ukiwa unamaanisha nini? Unataka kutuambia hao uliowataja hawajakanyaga shule kabisa? Hivyo vitu wanavyovifanya wameoteshwa?

Kwani sugu hajakanyaga shule kabisa.......
 
Mi nimefuatilia michango mingi ya sugu akiwa bungeni, michango yake huwa ni mizuri sana kuwashinda wengi waliosoma ambao muda wao mwingi ni kupongeza waziri fulani, kupongeza raisi wa awamu ya nne na pumba nyingi kama hizo. Kama una bifu na sugu usitumie jamii forums tafuta njia nyingine.
 
Elimu ya kitaa aliyonayo ndiyo tunayoihitaji. wenye hiyo elimu unayoifikiria wewe wameshaifanyia nini nchi hii???? kama sio kuifisidi!
 
utata wangu ni ple tunapokuwa na mwakilishi ambaye hawezi kutoa na kuwa na mipango ya kuwasaidia wanaichi wake sasa wakazi gani mtu kama huyu jimboni.

Sasa hapo ni utata juu ya elim yake au utata juu ya michango yake bungen?
 
90 % ya wabunge wa CCM nafikiri elimu zao ni utata mtupu kwa hii design unayozungumzia. Ikiwezekana kabisa Sugu hakumaliza shule kama unavyosema lakini hakugushi kama akina Mlugo. Sasa sijui utata uko wapo hapa. Wana CCM wabovu wa kuchangia ni wengi mpaka inasikitisha. Hivi mpango wa Prof. Maji Marefu au Lusinde ni nini????
 
jaman ni wabunge wangapi wa ccm wana phd lakini wanalala bungeni wakisubiri waseme ndioooo? Je ndo elimu yake inapowatuma? Ni bora huyo msema chochote kuliko hao wanaolala bungen
 
Unajua maana ya neno kielelezo au Vielelezo? au na wewe elimu yako ina utata?

Mimi nikisema tu kuwa wewe hujamaliza form four katika shule uliyofukuzwa tayari nitakuwa nimekupa kielelezo cha utata wa elimu yako??

tuletee basi hivyo vielelezo vinavyoonyesha kuwa sugu kamaliza form four. maana miaka yote tangu amefukuzwa sekondari tumekuwa tukimuona akiranda tu mitaani na makazi alibadili
 
Back
Top Bottom