COVID-19: Nani mkweli kati ya Serikali yetu na Ubalozi wa Marekani? Je, Tanzania tunawaogopa sana Wamarekani? Kwanini waseme uongo huu waachwe?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
Wanabodi,

Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa, huja na makala fikirishi, elimishi na hamasishi uzalendo za "Kwa Maslahi ya Taifa" ambazo hutolewa kwa mfumo wa maswali, makala ya leo ni kuhusu utoaji wa taarifa za Corona, COVID-19: Nani Mkweli Kati ya Serikali Yetu na Ubalozi wa Marekani?!. Jee Tanzania Tunawaogopa Sana Wamarekani?!. Kwanini Wamarekani Waseme Uongo Mkubwa kama Huu halafu Waachwe tuu hivi hivi?!.

Nimesoma with disbelief hii taarifa ya leo ya ubalozi wa Marekani, kwanini ubalozi unatoa taarifa ya uongo kuhusu hali ya COVID-19 nchini kwetu na wanaachwa hivi hivi?!, Jee hawa Wamarekani tunawaogopa?.

Taarifa yenyewe inapatikana hapa kwa wale wa kimombo
Tanzania International Travel Information
Kwavile taarifa yenyewe ni ya kimombo, kwa manufaa ya wenzangu na mimi, ninawawekea kakipande kadogo tuu ka mayai, na kukatafasiria kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili.

(Given the presumed ongoing community transmission in Dar es Salaam and other locations in Tanzania, the risk of contracting COVID-19 remains high. The Embassy has recommended that U.S. government personnel and their families reduce movement outside of their home except for essential activities and limit the number of visitors entering their home.

Healthcare facilities in Tanzania can become quickly overwhelmed in a healthcare crisis. There have been instances during the COVID-19 outbreak when hospitals in Dar es Salaam reached full capacity due to the high volume COVID-19 cases. Limited hospital capacity throughout Tanzania could result in life-threatening delays for emergency medical care)

Kwa kuanzia ni jana tuu, wakati kuna mwandishi wa habari wa kike gazeti wa gazeti la raia Mwema, ameozea jela kwa kushikiliwa kwa siku 14, kwa kusambaza ujumbe fulani wa Corona kwenye group la ofisi, jana hiyo nimepokea taarifa ya kifo cha mwandishi wa habari mkongwe mwenzangu katika fani ya upigaji picha za TV, nimefanya nae kazi DTV, kisha TBC, mimi nikatimuliwa kazi na kuingia mitaani, mwenzangu akaula na kuwa mpiga picha wa viongozi wakuu!, jana amefariki dunia hospitali fulani kwa ugonjwa fulani, leo tumemuaga, anazikwa kwao kesho!. Hatuwezi kutaja chanzo cha kifo kwasababu sisi sio familia yake, lakini tunakijua na kinazungumzwa wazi tuu msibani!.

Kama mpaka sasa update ya Corona kwa Tanzania ilitolewa mara ya mwisho tarehe 29 April wakati huo idadi ya vifo ni 16, na mpaka leo hakuna update hivyo idadi ya waliokufa kwa Corona Tanzania bara ni huo 16 tuu, na huu ndio ukweli wenyewe, kwanini Wamarekani
wanatusingizia uongo na kuitangazia dunia kuwa tunaficha data na wanaachwa hivi hivi?.

Rais wetu katangazia taifa kwa jiji la Dar es Salaam katika mahospitali wagonjwa wamepona na hakuna maambukizi mapya, kesho yake Waziri wetu wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu akatangaza Mlonganzila kumebaki wagonjwa 3, Amana amebaki mmoja Kibaha hakuna mgonjwa, hakuna kifo chochote, hakuna ambukizo jipya lolote, halafu leo, Ubalozi wa Marekani unatoa press release kuutangazia dunia kuwa Tanzania tunaficha data, wakati hakuna ambukizo jipya lolote, Wamarekani hawa wanatangazia dunia kuwa mahospitali yamefurika wagonjwa!, kwanini Wamarekani waseme uongo huu, waachwe, who the hell are they?!, au tunawaogopa?.

Kama Serikali ya Tanzania inasema ukweli, hakuna wanaokufa kwa Corona, hakuna maambukizi mapya na wagonjwa mahospitalini wamepona na kuruhususiwa na hakuna tena karantini yoyote, halafu Marekani akaitangazia dunia kuwa Tanzania tunaficha ukweli, dunia itawaamini nani kati ya sisi na Wamarekani?.

Tena taarifa hiyo ya Marekani, haijuishia tuu kutusingizia uongo kuwa serikali yetu inaficha data, wakati serikali yetu inasema ukweli, bali pia wametatishia mashirika yote ya ndege ya kimataifa yaliyotangaza kuanza safari za kuja Tanzania kuleta watalii, Marekani imewatisha kwa kutumia mtindo wa innuendo kwa kuyataja majina hayo mashirika, kuonyeshea wasipo cancel safari hizo, then hatua ya pili ni kuwataka Marekani na washirika wao, kuyasusia mashirika hayo.

Hivyo naomba kuwaanda kabla msije kushangaa, baadhi ya mashirika waliokubali kurejesha route ya Tanzania baada ya tishio hili la Marekani, wakafanya risk analysis kati ya kuleta abiria wa Tanzanians kupoteza soko la Marekani, au waitose Tanzania na kulinda soko la Marekani!.
Kama rais Magufuli juzi kasema Corona imepungua, jana Waziri Ummy kathibitisha kwa data, leo Marekani inaibuka na kesema hizo taarifa zinazotolewa na viongozi wetu ni taarifa za uongo, na kutusingizia serikali yetu inaficha data, nani mkweli na nani muongo?.

Kwanini Wamarekani waseme uongo waachwe?!. Kama serikali yetu itawanyamazia hawa Wamarekani bila kuwaonya au kuwachukulia hatua yoyote kwa uongo wao, then waelewa wataelewa nani ni muongo kweli na nani ni mkweli, na pia huu utakuwa ni uthibitisho kuwa Mmarekani tunamuogopa, hata utusingizie uongo gani sisi, tunanyamaza tuu!.

Tanzania na rais wetu Magufuli na serikali yetu tumekuwa tukisingiziwa uongo mwingi na sometimes hata kutukanwa na kudhalilishwa na media za nje, lakini tunanyamaza ama kwa kuwapuuza, ama kwasababu Tanzania kwa sasa hatuna watu wenye the capacity kujibu tuhuma kama za The Economist, lakini enzi za Kikwete, aliposingiziwa na balozi wa Marekani kuwa amehongwa suti, Ikulu yetu haikunyamaza, baada ya kupiga kelele humu, Marekani walikanusha.

Lakini sasa leo rais wetu anasema ukweli, kesho Waziri wetu wa Afya anasema kweli, halafu kesho yake, ubalozi uliopo hapa hapa Tanzania unaibuka na taarifa za uongo kuonyesha serikali yetu inaficha ukweli!, ukificha ukweli maana yake unachoripiti ni uongo!. Sasa huu uongo unaosemwa nchini, na ubalozi fulani, usipokanushwa, itaamaanisha ama tunawaogopa Wamarekani, ama tunachoelezwa na serikali yetu ni .. na wanayoyasema Wamarekani ndio ukweli wenyewe, ilaikitokea hawa Wamarekani ni waongo, swali linabaki "Hivi hawa Wamarekani wanatutakia nini?!. Kwanini watutungie uongo na kuueneza dunia nzima?. What is their motive behind and what do they wish to achieve?.

Paskali
 
Kila mtu anajua Corona ipo sana Tz, watu wanaugua kimya kimya na kuzikana kimya kimya pia. Serikali ilichokifanya ni kusitisha kutoa taarifa rasmi (ili kuhalalisha harakati za kimaisha ziendelee) lakini wakati huo huo taarifa za reja reja zikiendelea kuzagaa mitaani.

Hivyo ubalozi wa USA yuko sahihi kwa 100%, na hakuna ajabu yoyote kwa USA kutoa taarifa zenye lengo la kulinda raia wake waliopo hapa Tanzania. Ndio kazi iliyemleta Tanzania, na analipwa kwa kodi za wamerekani. Hatuwezi kumpangia cha kusema wala kufanya juu ya raia wa nchi yake.

Na sisi balozi wetu wa Tz aliyepo kule USA anapaswa kutoa taarifa za kulinda raia wa Tz waliopo huko USA au wanaotaka kwenda USA (ikiwezekana wasiende kabisa!) maana huko Corona ipo na kuna ghasia za maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi. Bahati mbaya balozi wetu huko USA yuko usingizini tu. Hajui anachotakiwa kufanya, sijui anasubiri kuambiwa na kina Bashiru au Pole Pole kitu cha kufanya
 
Marekani wako sahihi kabisa, tuache ubishi. Soma AYA ya pili kwenye barua niliyoambatanisha hapo ndiyo utajua mkweli na muongo.

uganda.jpg
 
Kila mtu anajua Corona ipo sana Tz, watu wanaugua kimya kimya na kuzikana kimya kimya pia. Serikali ilichokifanya ni kusitisha kutoa taarifa rasmi (ili kuhalalisha harakati za kimaisha ziendelee) lakini wakati huo huo taarifa za reja reja zikiendelea kuzagaa mitaani.

Hivyo ubalozi wa USA yuko sahihi kwa 100%, na hakuna ajabu yoyote kwa USA kutoa taarifa zenye lengo la kulinda raia wake waliopo hapa Tanzania. Ndio kazi iliyemleta Tanzania, na analipwa kwa kodi za wamerekani. Hatuwezi kumpangia cha kusema wala kufanya juu ya raia wa nchi yake.

Na sisi balozi wetu wa Tz aliyepo kule USA anapaswa kutoa taarifa za kulinda raia wa Tz waliopo huko USA au wanaotaka kwenda USA (ikiwezekana wasiende kabisa!) maana huko Corona ipo na kuna ghasia za maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi. Bahati mbaya balozi wetu huko USA yuko usingizini tu. Hajui anachotakiwa kufanya, sijui anasubiri kuambiwa na kina Bashiru au Pole Pole kitu cha kufanya
Tanzania inaficha hata idadi ya madaktari waliopukutika kama vumbi la kwenye kimbunga baadhi ya majina ninayo.
 
Takwimu za kidunia zinasema kuwa wastani wa 5% ya watu waliombukizwa Corona ndio hufariki. (Yaani katika kila kifo kimoja cha mgonjwa wa Corona basi nyuma yake kuna watu 19 waliopata Corona na hawajafa, yaani wako fit mtaani).

Kwa hapa Tz, karibu kila siku kuna at least mtu mmoja mwenye umaarufu wa kati ambaye amefariki (kwa ugonjwa unaelezwa na ndugu zake wa karibu kuwa ni COVID).

Sasa hapo ndipo utajua tupo wapi na tunakwenda wapi.
 
Kwa kuanzia ni jana tuu, wakati kuna mwandishi wa habari wa kike gazeti wa gazeti la raia Mwema, ameozea jela kwa kushikiliwa kwa siku 14, kwa kusambaza ujumbe fulani wa Corona kwenye group la ofisi, jana hiyo nimepokea taarifa ya kifo cha mwandishi wa habari mkongwe mwenzangu katika fani ya upigaji picha za TV, nimefanya nae kazi DTV, kisha TBC, mimi nikatimuliwa kazi na kuingia mitaani, mwenzangu akaula na kuwa mpiga picha wa viongozi wakuu!, jana amefariki dunia hospitali fulani kwa ugonjwa fulani, leo tumemuaga, anazikwa kwao kesho!. Hatuwezi kutaja chanzo cha kifo kwasababu sisi sio familia yake, lakini tunakijua na kinazungumzwa wazi tuu msibani!.
Poleni Sana kwa Msiba Uliosababishwa na "UGONJWA FULANI UNAOKUMBA MADEREVA WA NCHI JIRANI"

Juzi tu ameitwa balozi wao kwa kuzusha mambo na leo wamezusha tena wakati covid TZ nzima wagonjwa ni wanne tu waliofariki ni 21.
 
Mambo kama haya ni kawaida sana katika vita ya kiuchumi, Marekani yupo kimasilahi kupitia siasa zake.
Ujasusi unaeleza watu wabaya hujivika ngozi za kondoo, wema upendo na kusaidia hasa misaada kwa jamii au Taifa japo nyuma ya pazia ni watu hatari sana ( USA).

Ukweli ambao wengi hawaufahamu ni kuwa wamarekani wengi wana maisha magumu sana hasa kwenye public services kama vile hospitali na Mashule huduma zao ni mbovu tena mbovu sana tofauti na private services.(wapo vizuri wamiliki ni hao mabepari wanao tupa misaada).
zaidi wanatumia vyombo vya habari kam BBC. N.k kusambaza propaganda kwa mataifa kama yetu kwao hakuna uhuru wa vyombo vya habari kuripoti matatizo ya kwao (hili lipo wazi).

Kwa akili za kawaida sio kwamba USA wanatupa msaada bali wanataka kunufaika kupitia misaada na mikopo wanayotoa.
Hiki USA wanacho kifanya, mkuu Pascal Mayalla ni ajenda za kisiasa( wanatuchafua kisiasa) hapa sio corona kuna mambo yao
No mercy under capitalism.
 
....Nani mkweli na nani muongo sisi raia hatuwezi kujua kusema kweli maana njia tulizotumia kupambana na hili janga.......???
 
Taarifa za uhakika ni za waziri wa afya mh Ummy Mwalimu kwamba kuna wagonjwa wanne

Maendeleo hayana vyama!
Haya pasi- kali hiyo tutamwambia jiwe kwa muundo Wa setikali yetu kuna waziri Wa
(1) mambo ya ndani - wizara yake inafanya kazi nzuri tu ya kubonya watu na hakuna mtanzania anaelalamika
(2) wizara ya mambo ya nje - inafanya kazi nzuri ya kuwasiliana na masangoma Wa nje ya nchi
Na tuna kitengo kimoja cha
(1) msemaji wa serikali - anajitahidi sana kuitetea serikali kwa wananchi
Sasa tutamwambia jiwe aanzishe kitengo cha
(1) msemaji Wa serikali mambo ya nje - na wewe uwe msemaji mkuu hiyo idara
Na ili msigombane na kina johnmbatizaji huyu tuanzishe kitengo cha msemaji Wa mambo ya chato ili msigombanie cheo hicho kimoja na ili kufuta uvumi kuwa chato hakuna ikulu
MAMBO NI MENGI NA MUDA NI MCHACHE - OKO- TOBA. IS AROUND THE ROUND A BOUT
 
Mambo kama haya ni kawaida sana katika vita ya kiuchumi, Marekani yupo kimasilahi kupitia siasa zake.
Ujasusi unaeleza watu wabaya hujivika ngozi za kondoo, wema upendo na kusaidia hasa misaada kwa jamii au Taifa japo nyuma ya pazia ni watu hatari sana ( USA).

Ukweli ambao wengi hawaufahamu ni kuwa wamarekani wengi wana maisha magumu sana hasa kwenye public services kama vile hospitali na Mashule huduma zao ni mbovu tena mbovu sana tofauti na private services.(wapo vizuri wamiliki ni hao mabepari wanao tupa misaada).
zaidi wanatumia vyombo vya habari kam BBC. N.k kusambaza propaganda kwa mataifa kama yetu kwao hakuna uhuru wa vyombo vya habari kuripoti matatizo ya kwao (hili lipo wazi).

Kwa akili za kawaida sio kwamba USA wanatupa msaada bali wanataka kunufaika kupitia misaada na mikopo wanayotoa.
Hiki USA wanacho kifanya, mkuu Pascal Mayalla ni ajenda za kisiasa( wanatuchafua kisiasa) hapa sio corona kuna mambo yao
No mercy under capitalism.
Umeandika vitu out of context.
Issue hapa ni Corona, wewe unazungumzia vita ya Kiuchumi utadhani Corona ni suala la nchi moja moja au Marekani inapambana kiuchumi na Tz.
Jenga hoja kama Tz tunasingiziwa kuhusu Corona ama la. Hivyo blah blah za maisha ya wamarekani tuwaache wamarekani na marekani yao.

Hata hivyo huwezi kunishawishi kwa lolote kuwa maisha ya kiujumla ya wamarekani yako duni kiasi cha sisi kujilinganisha na wao.

Tuseme ukweli tu, 90% ya sisi watanzania tunatamani tungezaliwa marekani au kuishi marekani maisha yetu yote. Wenzetu wako mbele mnoo kwa kila kitu tukijilinganisha na sisi. Sisi bado tunaishi kukamilisha utaratibu tu (kupumua, kula, Kulala) lakini wenzetu wanaishi kuenjoy maisha.
 
Back
Top Bottom