Covid-19: Huu mgomo wa Umma kwa Rais wao utaliponya Taifa

KooZito

JF-Expert Member
Dec 14, 2020
396
1,377
Imezoeleka kuwa utawala wa Rais Magufuli umetia umma woga. Kwamba anachokisema Rais Magufuli ndio fainal hakuna wa kupinga au kutenda kinyume.

Msimamo wa Rais Magufuli ni kwamba hakuna Corona maana tutatishwa sana. Kilichopo ni changamoto ya kupumua ambayo dawa yake ni kujifukizia, kufanya kazi kwa bidii "na ndio maana hatuvai barakoa". Alisema mbele ya dunia huko Chato.

Hata hivyo umma mpana umemgomea Rais Magufuli na badala yake unawasikia viongozi wa dini na Shirika la Afya Duniani, WHO. Magufuli amegomewa, hasikilizwi maana watu wameamua kuvaa barakoa, wananawa mikono kila mara kwa maji tiririka na sabuni, ulaji wa matunda ya asili kwa sana, vitunguu swaumu, limao, ukaaji kwa nafasi nk. Hakuna cha nyungu wala vyungu. Huu ni mgomo wenye kheri!

Endeleeni hivyo hivyo maana Corona ipo. Tupambane nayo kama Jakaya Kikwete alivyoamua kuvunja ukimya na kuvaa barakoa hadharani. Akili ya kupewa changanya na zako.

Maisha yako hayako mikononi mwa mtu yeyote ni wewe. Vaa barakoa kujiokoa na kuokoa wengine. Ugonjwa upo!
 
Shaur yenu ndiyo tabia zenu hizo. Nlimwambia mapema hakunisikia. Kila mtu apambane na hali yake
 
Hivi Rais hata jana kahimiza watu kuchukua tahadhari. Maana ya tahadhari unajua wewe. Au ni chuki binafsi zinakusumbua. Binafsi nimejifunza kuamini na kukubaliana na kila kitu anachokisema rais wangu, he is super intelligent na anafikiria seven billions than regular human being.s. corona ya kwanza kama nilikuwa simwamini hivi ila baadae nikagundua I was wrong.
 
Hamna kitu JPM yupo sahihi 💯Ukitangaza lockdown hapa hao hao watz wanaanza kujadili matatizo wanayoyapata kutokana na namna serikali inavyokabiliana, kilichobak ni kuwaacha kila mmoja ajiponye nafsi yake , wakifa fresh, watakaobaki wataendeleza nchi.

Hatuwezi kufa wote. Membe amekimbilia kujificha kijijini anayethamin maisha yake asitishe kila kitu asepe Pori huko, Kwan serikali imekuzuia au mpak itangaze?

Kama unauwezo nenda nje kapigwe chanjo Rudi, jipige rockdown kimya kimya. Japan ww2 ilipoteza takribani watu milion 4 sababu ya maamuzi ya viongozi na bado washkaj wanaendelea.
 
Atufundishe namna ya kuomba mpaka korona ipotee, pengine viongozi wetu wa dini wanakosea.
 
Samahani miderators hawa watu wanatulazimisha tu kuwatukana af tunapigwa ban.hivi rais hata jana kshimiza watu kuchukua tahadhari. Maana ya tahadhari unajua wewe. Au ni chuki binafsi zinakusumbua. Binafsi nimejifunza kuamini na kukubaliana na kila kitu anachokisema rais wangu, he is super intelligent na anafikiria seven billions than regula human being.. corona ya kwanza kama nlikuwa simwamini hivi ila baadae nikagundua I was wrong
Unadhani ni kwa nin viongozi hawavai barakoa?
 
Hamna kitu JPM yupo sahihi 💯.... Ukitangaza lockdown hapa hao hao watz wanaanza kujadili matatizo wanayoyapata kutokana na namna serikali inavyokabiliana ....ma-mae kilichobak ni kuwaacha kila mmoja ajiponye nafsi yake , wakifa fresh, watakaobaki wataendeleza nchi ..... Hatuwez kufa wote ... Membe amekimbilia kujificha kijijini anayethamin maisha yake asitishe kila kitu asepe Pori huko, Kwan serikali imekuzuia au mpak itangaze?? Kama unauwezo nenda nje kapigwe chanjo Rudi ... jipige rockdown kimya kimya ....Japan ww2 ilipoteza takribani watu milion 4 sababu ya maamuz ya viongozi na bado washkaj wanaendelea ....
So
 
Hakuna aliyegoma acha uchochezi bwashee!
Watu wanaanza kumgomea
Alianza waziri mpango alipowaambia wafanyakazi wa wizara wachukue tahadhari ya Corona

Akaja kikwete juzi ameonekana amevaa barakoa na baadhi ya watu kwenye msiba kasoro wale chawa wake

Jana Waziri mkuu amesema watu wachukue tahadhari ya Corona na wavae barakoa

Umewasikia maaskofu wa TEC walivyotoa tamko juzi Sina haja ya kuelezea

Umemsikia Mganga mkuu

Na nk nk
 
Karudi Baba mmoja, toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapafu, na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali,
Wakataka na ukweli, uwafae maishani.

Akatamka mgonjwa, ninaumwa kweli kweli,
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali,
Pumzi naona yaisha , kifo kinanikabili,
Kama mwataka ukweli, semeni niseme nini.

Yakawatoka kinywani, maneno yenye akili,
Baba yetu wa thamani, sisi tunataka ukweli,
Uhai tunatamani, mali yetu ya halali,
Sema unaumwa nini , tujikinge maishani.

Baba aliye kufani, akajibu lile swali,
Nina kufa na korona, baba yenu nina homa,
Neno moja lishikeni, vaa barakoa matembezini ,
Kama mnataka ukweli, mtaupata hospitalini.
 
hasikilizwi maana watu wameamua kuvaa barakoa, wananawa mikono kila mara kwa maji tiririka na sabuni, ulaji wa matunda ya asili kwa sana, vitunguu swaumu
kuna sehemu rais alikataa kuyafanya haya?
 
Back
Top Bottom