CONFIDENTIAL: TANESCO, RICHMOND, DOWANS and BoT

Naona hata Serikali ikilipa bado ni fedha zetu, tunahitaji waliotuingiza kwenye hii MIKITABA wafilisiwe na pesa yao ilipe hili deni.

Na kama wakifilisiwa mali zao zikaweza kulipa Deni, Tutawahoji walizipate!
 
Ahsante sana Invisible kama kawaida yako unatufungua macho.

Heko Bodi ya Tanesco kwa uzalendo mulioonyesha hamkumung'unya maneno mulisimamia haki lakini michwa na viwavi akina Karamagi, Msabaha ma Katibu Mkuu wao wakijifanya viziwi, vipofu hawakuona umuhimi wa kutetea maslahi ya taifa.

Ahsante sana Mzee Utoh kwa kuyaona yote hayo wewe ni mzalendo.

Kwetu sisi wanachi ni kwamba senti tano isilipwe na waliohusika waswekwe ndani
 
Suala la Malipo kwa DOWANS Naona pole pole yanatutoa kwenye Point ya Msingi ambayo Wa Tanzania tunapaswa ku stick on.
Suala ni Dowans Kutokulipwa na sio Nani alipe Tanesco or Govt.

POAC inaposema Serikali ilipe Dowans na sio Tanesco huu ni usanii,suala ni Dowans kutokulipwa full stop.

Its high time now Great Thinkers, kuandika tuu hapa JF Haitoshi, sana sana naweza pandisha hasira na Kushindwa kufanya kazi ofisini vizuri.

Its high time now great thinkers kutoka nje ya JF, Ku demostarte yale tunayoyajadili hapa ndani.....

Lets arrange a date where we gonna meet ili tuweze kuyaweka haya tunayoyaandika into action.

Lets propose date and venue.

Rgds

HI! Uamuzi ulikuwa Serikali ilipe Dowarns baada ya mahakama kuamua ni haki ya Dws kulipwa, so tusubili uamuzi wa mahakama
 
Umesahau kitu kimoja kamanda, hoja nyingine ya msingi, pamoja na hiyo ya KUTOLIPWA DOWANS, pia wale waliotufikisha hapa tulipo wanapaswa KUPATA TREATMENT inayowastahili! Lakini baadhi yetu hatushangai, hasa mabo tumeamua kuwa 'alerted watazamaji' kuangalia hii kamati ya POAC ni kitu gani hasa linapokuja suala la nishati ya umeme na complications zote zilizomo ndani ya issue hiyo.

Sitaki kumtaja Zitto moja kwa moja hapa...
 
Umesahau kitu kimoja kamanda, hoja nyingine ya msingi, pamoja na hiyo ya KUTOLIPWA DOWANS, pia wale waliotufikisha hapa tulipo wanapaswa KUPATA TREATMENT inayowastahili! Lakini baadhi yetu hatushangai, hasa mabo tumeamua kuwa 'alerted watazamaji' kuangalia hii kamati ya POAC ni kitu gani hasa linapokuja suala la nishati ya umeme na complications zote zilizomo ndani ya issue hiyo. Sitaki kumtaja Zitto moja kwa moja hapa...
 
Jamani ni lini tutampata mkombozi wa nchi hii? Tukiendelea hivi mwisho wa siku hakitaeleweka!

Tumeshampata ila Dola haikumkubali, na kuna wengine pia wanatumiwa kumkataa.

Kama Dr Phd Slaa asingekataliwa na Dola na maoni ya walio wengi yangeheshimiwa wakati wa uchaguzi uliopita leo tusingekuwa tunaongea habari hizi, habari ya Richmod/Dowans ingekuwa ilishakwisha na wahusika wapo kule wanapotakiwa kuwa.

pia mambo kama;
Kuvunja Mikataba bomu,
Kulipa wazee wa EAC,
Kuanzisha Mchakato wa katiba (baadaye kuunda Tume Huru ya Uchaguzi)
Kuondoa kero za Muungano (Hasa kuuvunja ndio dawa ya Kudumu)
Kufanya Bunge. Takukuru,Mahaka,Majeshi na Usalama wa Taifa Kuwa Vyombo Huru.
Afya bora,
Elimu bora,
Mikakati bora ya Kuinua Uchumi wa Nchi.
Kuzuia Uchakachuaji wa Mafuta,
Kuzuia uingizwaji wa Bidhaa feki,
Kudhibiti Mfumuko wa Bei
Kuboresha usafiri wa miji mikubwa (mana watu wanapoteza masaa 4 Kila siku kwenye foleni barabarani)
NK,

Yangekuwa ndio kipaumbele na nina hakika yangekuwa yameanza kufanyiwa kazi.

Tatizo Tunaongea sana, Tunalala tukiamka tunaanza kuongea na kulala tena, haitusaidii!. jamaa watazidi kula na kunywa na kusaza huku sisi na jamii zetu tukiishia kunung'unika tu. Jamani kwa mambo kama haya! Mtindo wa Tunis na Misri ndiyo suluhu kwisha, Maana kwa Mwendo huu hatutakaa tushuhudie Uchaguzi Huru na wa Uwazi na Kweli
 
Ludovick Utoh for president. This guy is a pro.

i like the language used by Utoh, amewagonga nyundo za kichwa huku anawapuliza ... btw hav u guys noticed Balali's involvement in this saga ... dah inaonekana kuna uozo wa hali juu umefichwa huko katika inner circle .... come the day ... watu wataumbuka sana!!
 
Utoh amefanya kazi yake ya ukaguzi; kama akilekezwa afanye uchunguzi (investigation) basi hapo tutapata wa kupeleka mahakamani!

Lakini pamoja na mdudu yote hayo, sisi wananchi tunachukua hatua gani? Mbwa kabweka, mwenye mbwa si lazima utoke nje umsaidie - mwambie kamata kamata.. ndipo akamate mwizi!

Utoh kabweka, lakini sisi tunabaki ndani tumelala !!!!
 
Hata kama miaka itapita kila aliyehusika na hii shame lazima atatafutwa mahali alipo ili ashitakiwe . Mambo haya yanatia hasira sana kwani ndio yanayochangia umaskini usiokwisha.
 
China watu kama hawa wanafilisiwa afu ndio wanapigwa hukumu ya kifo kwa kupigwa risasi mpaka wawe kama chujio!!

I hate the leaders of this country, Mungu Ibariki nchi yetu Tanzania!
 
Hata kama miaka itapita kila aliyehusika na hii shame lazima atatafutwa mahali alipo ili ashitakiwe . Mambo haya yanatia hasira sana kwani ndio yanayochangia umaskini usiokwisha.
Kama hii ni kweli lakini naona Mzee Mwinyi bado anatesa na Loliondo aliipiga bei, na Katabalo Stanslaus alizikwa kwa hilo! Masikitiko
 
Pendekezo lako linaelekea kufanana na la POAC walilotoa; serikali (si TANESCO tena) ndo ilipe gharama hizi!

It still does not make sense. Serikali ikilipa maana yake ni kuwa mimi na wewe tumelipa. Hii kitu tuigomee kwa maandamano ya amani na wahusika walipe kutoka kwenye mali zao za wizi!!

Ooops, ingawa nazo ni pesa zetu pia.
 
Ludovick Utoh for president. This guy is a pro.

Mkuu Atapigwa vita tu na ile Dhambi ya CCM walioianzisha ya U zone (Kaskazini haitotoa Rais according to them)...
Pia atagombea kwa Chama gani Kaka, Maana jamaa lazima atakuwa na U CCM tu ndani yake though the guy seems to be muadilifu
 
Tatizo Tunaongea sana, Tunalala tukiamka tunaanza kuongea na kulala tena, haitusaidii!. jamaa watazidi kula na kunywa na kusaza huku sisi na jamii zetu tukiishia kunung'unika tu. Jamani kwa mambo kama haya! Mtindo wa Tunis na Misri ndiyo suluhu kwisha, Maana kwa Mwendo huu hatutakaa tushuhudie Uchaguzi Huru na wa Uwazi na Kweli
HAPO SASA.....MNAONGEA SANA NA HAMNA ACTION MUNAOCHUKUA.
MTA BRAINSTORM SANA HAPA, BUT AT THE END OF THE DAY WHAT WILL HAPPEN....??
OK TUMESHA SOMA HII, NA ZINGINE NYINGI....NOW WHAT?
MPAKA CKU MUTAKAPOAMUA KUCHUKUA HATUA......UNTIL THEN.....TUTABAKI NA AMANI YETU!! C TUNALALA NA KUAMUKA VIZURI! BANA:bored:
 
Samahani: Mbwa wa nyumbani kwangu anachagua vyakula, naamini angerushiwa mfupa unaonuka kama RICHMOND asingeusogelea hata kuunusa. Sasa nashindwa kuelewa hawa watanzania wenzangu (Presd, PM + Waziri-N&M) kama wana 'pua' au hawana. Na kama hawana pua basi hili li sirikali limeoza na dawa yake ni kutupwa dampo na kuchomwa moto. Ili ma-injinia waingie kazini..!
 
k1av0.jpg
 
Back
Top Bottom