Hivi nchi ina radio moja tu clouds? Mbona inawawasha sana wafuasi wa CDM? Kwanini msianzishe radio yenu na nyinyi? Kazi kuja kulialia kila siku hapa clouds clouds tumechoka
Nikiwa katika foleni kuelekea kuwajibika, napenda kusikiliza uchambuzi wa magazeti kutoka ktk radio tofauti tofauti.
Nimefungulia radio clouds, wakati Paul James (PJ) akichambua magazeti walipofikia kusoma habari ya Ukawa, Barbara Hassan akamwambia PJ hawa tuwapotezee maana wao wametupotezea.
Badala ya kurudi bungeni kusimamia tupate katiba nzuri wameamua kutupotezea basi nasi tusiwape kichwa tuwapotezee.
Kauli ambayo imeungwa mkono na PJ na Mbwiga na kuendelea kusoma habari zingine.
Hii inaonyesha ni kiasi gani wananchi wamekereka na ukawa waliokuwa wanawategemea kuleta changamoto kubwa ktk bunge la katiba hatimae kupata katiba nzuri.
Je maamuzi yao yametokana na uchanga wa uzoefu ktk siasa hasa katika mambo makubwa kubwa kama katiba kwa kutojua athari zake?
Au ni kususa baada ya kuona matumaini yao kuona yamepotea ya kuivunja Tanzania?
Maana kama ni kuleta machafuko hilo wasitegemee maana waTanzania hatujakulia katika mazingira hayo??
Nawasilisha.
Je, kama ukawa nao wakiamua kupiga kampeni ya kusema wananchi wanaowaunga mkono waipotezee clouds kama wanavyotaka wao,watabaki salama?
Mi nadhan clouds wangeondoa msemo wao wa radio ya watu kwani kiuhalisia si radio ya watu tena.Ni redio ya ccm!
Hiyo radio UKAWA inawauma kwasababu inawachana ukweli na kibaya zaidi ndo redio inayosikilizwa na watu wengi sana hapa tanzania. Hivyo madhara yake wanayajua.
Waulize swali kidogo. Lile gazeti la udaku la tanzania daima mbona linaandika ugoro wa ufipa kila siku na wanalitetea kwa kile liandikacho? Iweje iwe nongwa kwa vyombo vingine vya habari viandike againsit na wanavyotaka iwe nongwa?
Naomaba Nikulize kwanza Mleta Mada Utaenda kujadili kitu Ambacho sicho kilicholetwa Mwezani? Ile rasimu ya Jaji warioba kwani Ukawa ndio wameikata kuijadili? 2 Clouds nafikiri inajulikana inamrengo gani kwahiyo siyojambo lakushanga sana kwa hilo
We hujui hako ka radio ka CCM?
Rich Pol acha kuushangaza umati..unaposema wananchi wanaichukia ukawa unaongea wananchi gani??kama ni wakina Wasira,Sita,Nchemba na baadhi ya viongozi wa CCM sawa..ila ujue kua hata hao wanachama wa CCM baaadh wanaishangilia ukawa kila kukicha kwa kuyamulika yale ambayo wao wameshindwa kuyamulika kwakua wapo ndani ya CCM....Unapokuja kutuelezea maoni ya wachumia tumbo wa clouds hapa ambao tunajua sababu ya kushabikia CCM ntakushangaa sanaa...eti mbwiga,PJ,Babraa..embu waulize huwa wanatumia mda wao kufatilia mambo ya katba pamoja na kusoma rasimu ya warioba ilivyo watakwambia hapana zaid ya kufatilia mambo hayo kwenye magazetu ya uhuru..wakati mwingine muwe manapost mambo ambayo yanaeleweka hata km umetumwa ku post sio uonekane -------- hata na wapumbavu...
Chezea Ikulu sports club.Yani swagger zake na yeye mhhhhh???!
Mbona yupo bomba tu tena mrembo au ulitaka awe kama miss!!!,au we mama yako yukoje??
Nikiwa katika foleni
kuelekea kuwajibika, napenda kusikiliza uchambuzi wa magazeti kutoka ktk
radio tofauti tofauti.
Nimefungulia radio clouds, wakati Paul James (PJ) akichambua magazeti
walipofikia kusoma habari ya Ukawa, Barbara Hassan akamwambia PJ hawa
tuwapotezee maana wao wametupotezea.
Badala ya kurudi bungeni kusimamia tupate katiba nzuri wameamua
kutupotezea basi nasi tusiwape kichwa tuwapotezee.
Kauli ambayo imeungwa mkono na PJ na Mbwiga na kuendelea kusoma habari
zingine.
Hii inaonyesha ni kiasi gani wananchi wamekereka na ukawa waliokuwa
wanawategemea kuleta changamoto kubwa ktk bunge la katiba hatimae kupata
katiba nzuri.
Je maamuzi yao yametokana na uchanga wa uzoefu ktk siasa hasa katika
mambo makubwa kubwa kama katiba kwa kutojua athari zake?
Au ni kususa baada ya kuona matumaini yao kuona yamepotea ya kuivunja
Tanzania?
Maana kama ni kuleta machafuko hilo wasitegemee maana waTanzania
hatujakulia katika mazingira hayo??
Nawasilisha.
Kilichopaswa kujadiliwa ni RASIMU YA PILI YA KATIBA kama ilivyowasilishwa na TUME YA KATIBA MPYA.Na rasimu inapendekeza muundo wa serikali 3 ndani ya nchi iitwayo JMT.Kero inakuja pale CcM walipokuja na pendekezo la ajabu la SERIKALI 2 na kutaka hoja yao hiyo ijadiliwe badala ya kujadili jinsi ya kusanifisha mawazo ya wananchi juu ya muundo wa serikali 3.Sasa hiyo Rasimu ya katiba ilipelekwa bungeni kufanya nini kama hamtaki mabadiliko? Warioba alitakiwa akimaliza kazi yao angeipeleka kwa wananchi ipigiwe kura iwe katiba kamili, ni upuuzi kupinga isijadiliwe na nufanyiwa marekebisho kwa manufaa ya wachache.