Nikiwa katika foleni kuelekea kuwajibika, napenda kusikiliza uchambuzi wa magazeti kutoka ktk radio tofauti tofauti.
Nimefungulia radio clouds, wakati Paul James (PJ) akichambua magazeti walipofikia kusoma habari ya Ukawa, Barbara Hassan akamwambia PJ hawa tuwapotezee maana wao wametupotezea.
Badala ya kurudi bungeni kusimamia tupate katiba nzuri wameamua kutupotezea basi nasi tusiwape kichwa tuwapotezee.
Kauli ambayo imeungwa mkono na PJ na Mbwiga na kuendelea kusoma habari zingine.
Hii inaonyesha ni kiasi gani wananchi wamekereka na ukawa waliokuwa wanawategemea kuleta changamoto kubwa ktk bunge la katiba hatimae kupata katiba nzuri.
Je maamuzi yao yametokana na uchanga wa uzoefu ktk siasa hasa katika mambo makubwa kubwa kama katiba kwa kutojua athari zake?
Au ni kususa baada ya kuona matumaini yao kuona yamepotea ya kuivunja Tanzania?
Maana kama ni kuleta machafuko hilo wasitegemee maana waTanzania hatujakulia katika mazingira hayo??
Nawasilisha.