Na Karoli Vinsent
SAA chache kupita Baada Radio ya
Clauds Fm kutangaza Rasmi
kutozisoma Habari zozote
zinazowahusu Wajumbe wanaunda
umoja wa Kutetea Katiba ya
Wananchi UKAWA, kwa kile
wananachodai Umoja huo hauna
jipya bali unataka umaharufu tu.
Kauli hiyo ya ambayo
inakwenda kinyume na Maadili ya
Vyombo vya Habari imetolewa leo na
Mtangazaji wa Kipindi cha Power
breakfast Babla hassani wakati
wakichambua magazeti ya siku
ambapo alisema kwa sasa
hawatazisomi habari zozote
zinazohusu umoja huo wa Ukawa kwa
madai umoja huo ni wabinafsi na
hawana jipya bali wanataka
Umaharufu.
Naye Mwanasheria wa Umoja
wa kutetea katiba ya Wananchi
UKAWA ,Tundu Lissu amewavaa na
kusema Radio hiyo inajimaliza na
ndio itakuwa inaonekana wazi
inapendelea Upande moja Kisiasa.
Kauli hiyo Tundu
Lissu,ameitoa mda huu wakati
alipokuwa anaongea na Mwandishi
wa Mtandao huu,Kuhusu wao Ukawa
wamepokeaje Taarifa hiyo ya
kutosomwa Habari zao kwenye Radio
hiyo.Ambapo Lissu alisema hizo
taarifa anazisikia na kama ni kweli
wametangaza hivyo watakuwa
wamejimaliza.
Kwanza nimezisikia hizo
taarifa na kama kweli aliyosema huyo
mtangazaji ndio msimamo wa Radio
nzima basi watakuwa watu wa Ajabu
sana maana leo Nchi nzima habari ya
Mjini ni Ukawa,leo utasemaje ukawa
ni wabinafsi wakati wasomi na watu
wengine wanaungana na sisi leo
inakuwaje Radio hiyo iseme hivyo
kama wako upande mmoja wa
Kisiasa wesemealisema Lissu.
Tundu Lissu,ambaye naye ni
Mjumbe wa Bunge maalum la Katiba
alizidi kusema yeye sio mwanahabari
bali anachokijua huo utakuwa
msimamo wa Radio nzima na wao
Ukawa hawata ogopa na kuacha
kuwatetea wananchi kwani wako kwa
ajili ya kuwakomboa wananchi na
hawezi kukatishwa na tamaa na watu
wachache wenye maslai ya upande
mmoja.
Harafu inashangaza sana
leo nchi nzima inazungumzia Ukawa
harafu mtua aseme leo Ukawa
utotangaza habari zao kwa misingi
hipi?alihoji Tundu lissu.
Kauli hiyo ya Tundu
Lissu,imetolewa saa chache kupita
baada Mtangazaji wa kipindi cha
Power Breakfast Babla
Hassani,kutangaza Rasmi kwamba
hawatasoma Habari zozote
zinazohusu Umoja huo.
Mimi Naona kusoma Story
zinahusu Ukawa tunawapa kiki tu
wao siwamekuwa kutupotezea
kutorejea Bunge I whon doing,vile
vikao vinawanufaisha watanzania
wote wao ni wabinafsi tu,the best
ican do tuwapotezea Habari zao, na
ukiona habari inahusu Ukawa tu
usisome hapa kwenye Redio,na wakae
huko nje atuwataki Ukawa
bungenialisema Babla Hassani.
Kauli hiyo ya iliungwa Mkono
pia na Mtangazaji wa mwengine wa
kipindi hicho, Paul Jems
anayejulikana kwa jina la Umaarufu
PJ naye alisema kwanzia sasa
hatazisoma habari zozote zinazohusu
Umoja huo kwani wanapoteza pesa
za wananchi bure kwa kususia bunge
hilo.
Msimamo huo wa Watangazaji
hao unakwenda Kinyume na Mmiliki
wa Radio hiyo ya Clauds Fm Joseph
Kusaga alipokuwa anahojiwa na
kipindi kimoja cha runinga kutoka
nchini Uingereza kinachojulikana,The
Sporah Show ambapo katika kipindi
hiko alisema Radio yake haina
upande wowote wa Kisiasa na
kuongeza ni Redio huru inayofanya
kazi bila kushabikia upande wowote.
Lakini kwa sasa kauli ya
Mmiliki hiyo inakwenda tofauti na
ilivyo,na kama Radio ikifanya kama
inavyofanya hivyo kwa sasa,Basi
Redio hiyo itapelekea machafuko
makubwa kama yaliyowai kutokea
nchini Rwanda na kuua maelfu ya
watu,na sababu kubwa ni Radio za
nchini humu zilikuwa na misimamo
kama walioyonayo Clauds.
Umoja huo wanaupinga wa
Ukawa unaundwa na Muunganiko wa
Vyama vikuu vya Upinzani ikiwemo
Chama cha demokrasia na
Maendeleo CHADEMA,Chama cha
wananchi CUF,Chama cha Mageuzi
NCCR,ND pamoja na Baadhi ya
wajumbe 201 walioteuliwa na Rais
Kikwet e.
Umoja huo umegoma kurejea
kwenye Vikao vya Bunge la katiba kwa
madai rasimu inayotokana na Maoni
ya wananchi kuchakachuliwa,na
kitendo hicho cha Ukawa kimeungwa
mkono na wananchi mbalimbali
wakiwemo Viongozi wa Dini pamoja
wajumbe wa iliyokuwa tume ya Jaji
warioba.
source full habari blog.