Clouds Wanadhalilisha Taasisi ya Urais

Clouds Wanadhalilisha Taasisi ya Urais

Hvi kweli jaman huyu Jk anajua anachokifanya, sijuwi hata washauri wa hyo taasisi wanajua nin cha kufanya., Pole zao an Slow slow yes Muvument 2tafika tu japo tutakuwa tumechelewa. Kila ninaposikia hilo tangazo nataman kufa
 
Ukitaka kujua upeo wa kufikiri wa mtawala wa jamii yoyote,angalia sifa za watu wanaomzunguka na kumshauri na uamuzi anaoufanya kulingana na ushauri anaopewa na wasaidizi wake.Wakimshauri ujinga naye akafanya uamuzi wa kijinga basi ujue naye upeo wake unalingane na wanaomshauri,ukiona kinyume basi ujue uyo mtawala yuko vizuri kichwani.
Viongozi wengi nchi hii wamepewa madaraka lakini hawajui uzito wa madaraka waliyonayo,mfano mzuri Muhongo,jaribu kumfuatilia anavyofanya uamuzi na kutamka maneno ya kuudhi yaani ni miongoni mwa viongozi ambao hajui kwamba akiongea yeye imeongea serikali.Watanzania tuna safari ndefu sana ya maendeleo.
Sijui protokali za Ikulu lakini sidhani kama kulikuwa na umuhimu wa Rais kuhudhuria shughuli kama ya Clouds ilihali kuna waziri wa michezo na utamaduni.
 
Nili Mwona Pia Pale TBC Akitangaza Biashara Ya Vyandarua, Aibu Kweli!
 
If u really wanna know the real culture of it's people........go to their markets!
 
Raisi mwenyewe msani, usikute alienda hapo kwakuwa alikuwa ameona kimwana. chezea JK, wewe
 
Hebu mwacheni JK wa watu apumzike kwa utarii wa ndani, akienda nje, mnasema Ooo! safari za nje zimezidi. aki tarii ndani Ooo! anatangaza matangazo ya biashara. mi siamini kama alienda hapo kutanzaza biashara. RIZ.1 ukowapi? ongea na mshua uje utujibu
 
nothing special to become the president of Tanzania rep ,hii nayo inaweza kuwa moja ya ndoto zangu sasa,viva mkuu kwa kutufumbua macho
 
Kuna vitu ambavyo lazima tuyaangalie kwa undani. Walichokifanya Clouds ni kitu cha kuigwa kutumia Jingle ya sauti ya Rais wangu ni kuwaambia watanzania kuwa wanazo Baraka zote toka kwa Rais.

Rais anatoa shukurani zake na kutuaminisha watanzania Fursa ilikuwa ya kuigwa.

Tuache kuwa biased. Tanzania ni yetu wew ukiona Negative sisi Tunaona Positive things.

What a joke from Great Thinker!

Ethics and its code of conduct INAKATAZA kwa taasisi yyt ya serikali ikiwemo IKULU kujihusisha na private owned investment isipokuwa kwenye issue ya kodi na ushauri!

Rais wa nchi kujihusisha na tangazo la private media ni aibu na kama ingeonekana ni muhimu sauti ya Rais itumike hilo tangazo lingerushwa na State Media-TBC

JK kafanya kila mtu aamini anaweza kuwa Rais na wala sijashangaa niliposoma jana kuwa Kigwangallah nae anataka agombee 2015!
 
mbona hiyo taasisi haijawahi kuwa na hadhi ...au hadhi ipi unayozungumzia
 
JK ameufanya Uraisi ni Kuongoza sio Utawala,hataki aonekane kama dikteta au Mfalme,JK mtu wa watu.hana majigambo wala kusujudiwa,wala Ikulu hataki ionekane kama peponi ni nyumba yetu na kila Mtu alieiletea Taifa heshma anawezakwenda,zamani hata Waandishi wa habari walikuwa Ikulu wanaiona kama Peponi.Jamaa akiondoka tutamkumbuka.
Tutamkumbuka sana maana hatujawahi kuwa na Rais asiye na msimamo na aliyefanya Serikali ni chombo cha washkaji kama huyu..
 
Japo sijasikia hilo Tangazo lakini Sidhani kama ni vizuri kutumia Taasisi hiyo kwa matangazo. Na mkuu mwenyewe sijui hilo halioni niliwahi kusikia sauti yake kwenye DUNIA YAKO CHAGUO LAKO. Hadi kwenye Fursa nadhani yupo heunda na hisa huko.

Uwezo wa kufikiri unamtegemea Dr Slaa anachosema na asiposema yeye huwezi kufikiri. Chadema family
 
Sasa hawa usalama wa taifa wanakazi gani watamuweka adi kwenye matangazo ya pombe na ya kumbi za starehe rais anaitaji heshima sauti yake kila wakati inasikika sasa ata hutuba yake watu watakuwa awasikilizi siwashazoea kusikia kwenye matangazo sauti yake
 
Back
Top Bottom