Nlifikiria mletaji wa post hii angelituwekea hicho walichosema hasa. Mimi nahisi kuna ukweli wa waliyoyaongea kwa kiasi hicho hicho mleta post hii alichotujuvya.
Na majibu yaliyofuata baada ya post hii, mengi yao yameakisi kule kule kwanye madai ya walalamikiwa ie Kibonde na Gadna, watu badala ya kujadili uhalali wa madai yao, wamekwenda kwenye vitu visivyonamsingi wowote kwenye hoja yao au malalamiko yao, masuala ya elimu, nani kawatafutia kazi za utangazaji, itikadi zao za siasa hazihusu kitu kwenye mada hii au madai waliyoyatoa zaidi ya kuthibitisha kile wanachokilalamikia humu jamvini. Hayo ndiyo yale mambo binafsi wanayolalamika kuwa jamvini humu yanashikiwa bango kuliko hoja za maana.
Sote tunakumbuka majadala wa kipuuzi uliowahi kuletwa humu jamvini kuhusu "ukabila" wa mwanamziki nguli, Lady jaydee. Mjadala ule ni wazi kuwa uligusa maisha yake binafsi zaidi kuliko mambo mengi ya maana ambayo unaweza kumuongelea mtu kama Jay dee, ukabila wa mtu ni mambo yanayomhusu mwenyewe unless otherwise, ameyaweka mwenyewe katika mjadala wazi unaoleweka na siyo mtu akurupuke tu kuja na mada ihusuyo mambo ya mtu kujisifia tu kwa raha zake.
Nionavyo, watu humu wabadilike, waache kujifanya kujuwa kwingi na kudhihirisha kuelimika kwao kudogo, ambako wao wanakuona kukubwa, kwa kuacha kujadili "issues" na kujadili watu, hayo ni mambo ya walioishiwa na hoja kama vile mwanamme mpumbavu anaposhindana na mwanamke kwa maneno, mwishowe akishindwa anaamua kurusha ngumi. Tubadilikeni jamani! na si kila anayesema ukweli zidi yetu aonekane adui au haipendi JF, sisi si malaika kama kila kitu tupo sawa, tunakosea na tunawakosea watu, kama waungwana na wasomi kweli, tunavyojidai, basi tukubali kujisahihisha tunapoikosea, siyo kupayukwa payukwa pale ukweli unapotugusa.