Tunapigana vita vya kiuchumi…wana pakukimbilia: Chongolo
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Daniel Chongolo amesema Tanzania ikiwa sehemu ya dunia, iko katika mapambano ya vita vya kiuchumi asubuhi, mchana na jioni, akiwataka Watanzania kuwa makini na watu wachache, katikati ya mapambano hayo, wenye dhamira ovu kwa nchi yetu, wanaotaka kutumia mjadala wa uwekezaji bandarini kuvuruga amani iliyopo, kwa sababu wanapo mahali pa kukimbilia nje ya nchi, kama baadhi yao walivyofanya miaka michache iliyopita.
Ndugu Chongolo amesema kuwa ingawa uhuru wa nchi ulipatikana baada ya kuwaondoa wakoloni, mapambano ya kujikomboa kiuchumi yako katika changamoto ya vita vya kiuchumi ambavyo havionekani kwa macho waziwazi, lakini vinahitaji akili, busara na mikakati zaidi kuvipigana na kwamba nchi inatakiwa kuwa imara ili isiyumbiwe wala kutolewa kwenye mstari sahihi na wapinzani au maadui wasioitakia mema.
Katibu Mkuu Chongolo amesema hayo wakati akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika leo Jumatano, Julai 19, 2023, katika Uwanja wa Shule ya Mazoezi, mjini Korogwe, mkoani Tanga, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake, kufafanua na kuwaelimisha wananchi masuala mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali kupitia Ilani ya CCM ya mwaka 2020 – 2025, ikiwemo suala la makubaliano ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai yanayolenga kuanzisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa ajili ya uboreshaji wa uendeshaji wa Bandari ya Dar Es Salaam.
“Niwaambie miaka ya 50 kwenda ya 60 tulipigania uhuru wa nchi yetu. Uhuru ulipatikana na sasa Tanzania iko huru. Lakini vita haijaisha. Vita inaendelea. Sasa hivi hatupiganii uhuru tena. Kwa sababu upo. Vita ya sasa ni vita ya uchumi. Na hii ni vita ya dunia. Na sisi Tanzania ni sehemu yake. Na sisi tunapigana vita hiyo, asubuhi mchana na jioni. Ndugu zangu wana-Tanga, vita ya uchumi ni vita ya kutumia akili, busara na ya kimkakati zaidi.”
“Huwezi kuiona kwa macho, hauwezi kuishika kwa mkono. Lakini ni vita tena ni vita kubwa, kuliko ile ukombozi wa wakati huo. Ni vita ambayo ukikaa kienyeji umeenda na maji. CCM hoyee…CCM hoyee…Vita hii ukikaa kienyeji umeenda na maji. Kwanini nasema ukikaa kienyeji umeenda na maji? Kwa sababu fursa tunazopigania wote, kuzipata na kuzitumia ili kujiendeleza ni fursa za aina moja na zinapatikana kwenye maeneo yale yale. Kwa hiyo kila mmoja anaiangalia fursa kwa jina lake, kwa jicho lake, kwa namna yake na kwa mazingira,” amesema Ndugu Chongolo.
Ndugu Chongolo ambaye katika mkutano huo aliongozana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Ndugu Steven Wassira, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Ndugu Atupele Mwakibete (Mb) na Mbunge wa Jimbo la Ukonga (CCM), Ndugu Jerry Silaa wakitoa ufafanuzi wa kina kuhusu ukweli na uhalisia wa mkataba wa uboreshaji utendaji wa bandari na manufaa yake,
Amesisitiza kuhusu umuhimu wa Watanzania kuilinda amani, amesema kuwa hiyo ni mojawapo ya tunu ambazo waasisi wa Tanzania walihakikisha inakuwa ni utambulisho wa taifa na inatakiwa kulindwa na kutetewa kwa nguvu zote bila kuwaonea aibu wala kuwaogopa wote wanaotishia kuivuruga kwa maslahi ya kisiasa.
“Mwalimu (Nyerere, Baba wa Taifa) alisema ukiulizwa Tanzania una nini, sema una amani huku ukijidai. Amani hii si amani rahisi, si amani ya lelemama, kuna watu wametoka jasho na wanatoa jasho ili hii amani iwepo. Tusiache amani hii ipotee kwa sababu ya wajanja wachache wenye dhamira ovu kwa nchi yetu, wenzetu wana mahali pa kukimbilia.”
“Na ushahidi tumeuona miaka michache iliyopita. Walivyoona huku mambo yao yamekaa vibaya walitafuta pa kuishi. Sisi tuna wapi pa kukimbilia nje ya Tanzania? Kama hatuna tujue tuna wajibu wa kuilinda amani ya nchi hii, tuna wajibu wa kuiendeleza nchi hii. Na tuna wajibu wa kusimamia maslahi ya nchi hii bila aibu wala kumuogopa yeyote,” amesema Ndugu Chongolo akisisitiza pia kuwa CCM itahakikisha maoni ya wananchi yenye tija na chanya, yanafanyiwa kazi na Serikali katika hatua za kuingia mkataba wa utekelezaji.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Daniel Chongolo amesema Tanzania ikiwa sehemu ya dunia, iko katika mapambano ya vita vya kiuchumi asubuhi, mchana na jioni, akiwataka Watanzania kuwa makini na watu wachache, katikati ya mapambano hayo, wenye dhamira ovu kwa nchi yetu, wanaotaka kutumia mjadala wa uwekezaji bandarini kuvuruga amani iliyopo, kwa sababu wanapo mahali pa kukimbilia nje ya nchi, kama baadhi yao walivyofanya miaka michache iliyopita.
Ndugu Chongolo amesema kuwa ingawa uhuru wa nchi ulipatikana baada ya kuwaondoa wakoloni, mapambano ya kujikomboa kiuchumi yako katika changamoto ya vita vya kiuchumi ambavyo havionekani kwa macho waziwazi, lakini vinahitaji akili, busara na mikakati zaidi kuvipigana na kwamba nchi inatakiwa kuwa imara ili isiyumbiwe wala kutolewa kwenye mstari sahihi na wapinzani au maadui wasioitakia mema.
Katibu Mkuu Chongolo amesema hayo wakati akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika leo Jumatano, Julai 19, 2023, katika Uwanja wa Shule ya Mazoezi, mjini Korogwe, mkoani Tanga, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake, kufafanua na kuwaelimisha wananchi masuala mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali kupitia Ilani ya CCM ya mwaka 2020 – 2025, ikiwemo suala la makubaliano ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai yanayolenga kuanzisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa ajili ya uboreshaji wa uendeshaji wa Bandari ya Dar Es Salaam.
“Niwaambie miaka ya 50 kwenda ya 60 tulipigania uhuru wa nchi yetu. Uhuru ulipatikana na sasa Tanzania iko huru. Lakini vita haijaisha. Vita inaendelea. Sasa hivi hatupiganii uhuru tena. Kwa sababu upo. Vita ya sasa ni vita ya uchumi. Na hii ni vita ya dunia. Na sisi Tanzania ni sehemu yake. Na sisi tunapigana vita hiyo, asubuhi mchana na jioni. Ndugu zangu wana-Tanga, vita ya uchumi ni vita ya kutumia akili, busara na ya kimkakati zaidi.”
“Huwezi kuiona kwa macho, hauwezi kuishika kwa mkono. Lakini ni vita tena ni vita kubwa, kuliko ile ukombozi wa wakati huo. Ni vita ambayo ukikaa kienyeji umeenda na maji. CCM hoyee…CCM hoyee…Vita hii ukikaa kienyeji umeenda na maji. Kwanini nasema ukikaa kienyeji umeenda na maji? Kwa sababu fursa tunazopigania wote, kuzipata na kuzitumia ili kujiendeleza ni fursa za aina moja na zinapatikana kwenye maeneo yale yale. Kwa hiyo kila mmoja anaiangalia fursa kwa jina lake, kwa jicho lake, kwa namna yake na kwa mazingira,” amesema Ndugu Chongolo.
Ndugu Chongolo ambaye katika mkutano huo aliongozana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Ndugu Steven Wassira, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Ndugu Atupele Mwakibete (Mb) na Mbunge wa Jimbo la Ukonga (CCM), Ndugu Jerry Silaa wakitoa ufafanuzi wa kina kuhusu ukweli na uhalisia wa mkataba wa uboreshaji utendaji wa bandari na manufaa yake,
Amesisitiza kuhusu umuhimu wa Watanzania kuilinda amani, amesema kuwa hiyo ni mojawapo ya tunu ambazo waasisi wa Tanzania walihakikisha inakuwa ni utambulisho wa taifa na inatakiwa kulindwa na kutetewa kwa nguvu zote bila kuwaonea aibu wala kuwaogopa wote wanaotishia kuivuruga kwa maslahi ya kisiasa.
“Mwalimu (Nyerere, Baba wa Taifa) alisema ukiulizwa Tanzania una nini, sema una amani huku ukijidai. Amani hii si amani rahisi, si amani ya lelemama, kuna watu wametoka jasho na wanatoa jasho ili hii amani iwepo. Tusiache amani hii ipotee kwa sababu ya wajanja wachache wenye dhamira ovu kwa nchi yetu, wenzetu wana mahali pa kukimbilia.”
“Na ushahidi tumeuona miaka michache iliyopita. Walivyoona huku mambo yao yamekaa vibaya walitafuta pa kuishi. Sisi tuna wapi pa kukimbilia nje ya Tanzania? Kama hatuna tujue tuna wajibu wa kuilinda amani ya nchi hii, tuna wajibu wa kuiendeleza nchi hii. Na tuna wajibu wa kusimamia maslahi ya nchi hii bila aibu wala kumuogopa yeyote,” amesema Ndugu Chongolo akisisitiza pia kuwa CCM itahakikisha maoni ya wananchi yenye tija na chanya, yanafanyiwa kazi na Serikali katika hatua za kuingia mkataba wa utekelezaji.