Zion Train
JF-Expert Member
- Jun 5, 2008
- 501
- 78
thubutu,chenge keko? labda watamuongezea ulinzi nyumbani hili asidhuliwe!
Habari zaidi zinasema hakuua kwa risasi, bali aligonga Bajaj na kuua watu wawili, na Kova ataongea na waandishi asubuhi hii saa 5.
Hiyo pole kwa wafiwa ndio cha msingi kwa wakati huu, kuliko huo utumbo mwingine...!Ndiyo matatizo ya kuwaachia hawa mafisadi wakiendelea kupeta mtaani wakati kuna ushahidi wa kutosha dhidi yao. Angekuwa amekamatwa na kuwekwa rumande kusaidia uchunguzi wa tuhuma dhidi yake basi hao Watanzania aliowaua labda wasingekutana na umauti wao. Mwenyezi Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi~AMEN.
Huyu mnyantuzu nae anatuaibisha tu sisi wapiga kura wake!Zee zima saa tisa za usiku linatoka kujirusha!wakati sisi wanaBariadi tunaishi chini ya dola moja kwa siku mbili!haki ya nani mwakani hatumpi UBUNGE
Huyu mnyantuzu nae anatuaibisha tu sisi wapiga kura wake!Zee zima saa tisa za usiku linatoka kujirusha!wakati sisi wanaBariadi tunaishi chini ya dola moja kwa siku mbili!haki ya nani mwakani hatumpi UBUNGE
Chenge kaachiwa kwa dhamana na ameondoka ndani ya gari aina ya Toyota Harrier namba T193 AYL.Ditto aliyeua kwa risasi aliachiwa mitaani na kutukana watu mpaka Mola alipoingilia kati.
Hivi kila siku nikisikia ajali imetokea dereva kakimbia ile ya Salome Mbatia dereva kakimbia hadi leo mabasi madereva haswa mbio dawa ni nini? na hawa ndio wenye clue ya kuelezea what happen na sheria kufuata mkondo wake
Chenge kaachiwa kwa dhamana na ameondoka ndani ya gari aina ya Toyota Harrier namba T193 AYL.
Taarifa za kipolisi zinasema mwenye Bajaj ndiye alikuwa na makosa na huenda ndiyo sababu iliyopelekea yeye kukimbia (anageuziwa kibao?)
Kuna walinzi waliokuwa eneo la tukio, huenda hawa wakatoa msaada wa hali halisi. Walinzi hao wanasema kwamba, dereva wa Bajaj alipona gari la Chenge linamfuata upande wake akalikwepa na kuruka ndipo kina dada wa watu waliokuwa wakitokea Club Maisha wakajikuta hawana msaada na kugongwa wakiwa pekee bila dereva. Kwa kuwa dereva hajulikani alipo, kila kitu kitamuelemea yeye na huenda akionekana ataambulia vijisenti akanunue Bajaj zake kadhaa (asiajiriwe tena).
Kuna habari kwamba kina dada hao wanatokea mkoani Mwanza na leo walikuwa waelekee Zanzibar kwa ndege kufanya shopping kabla ya kurejea kwao, mmoja akitajwa kuwa Bi harusi mtarajiwa
Hivi inawezekana ilikua hivi?....
Taarifa za kipolisi zinasema mwenye Bajaj ndiye alikuwa alikuwa na makosa na huenda ndiyo sababu iliyopelekea yeye kukimbia (anageuziwa kibao?)
.... Kwa kuwa dereva hajulikani alipo, kila kitu kitamuelemea yeye na huenda akionekana ataambulia vijisenti akanunue Bajaj zake kadhaa (asiajiriwe tena).
...nahisi chozi lanilenga...
Enewei chenge ni mjanja kwa kuepa hiki kihunzi and kwa kuwa anaijua sheria. Nahisi alipoamka asubuhi alipiga simu kwa vijana wake kuulizia kama kuna malalamiko au ripoti ya ajali, alipoona hakuna ripoti inayomkonect akaamua kutumia njia ya kujisalimisha ili aonekana ni mtiifu wa sheria. ila swali langu ni kwa nini asingeenda hata kutoa taarifa kama si kujisalimisha soon baada ya kuwagonga marehemu?? angelikuwa msafi mpaka ktk nadhiri zetu kuwa he is responsible citizen kama angelikwenda saa tisa ile ile kuripoti. Kwa nini alifululiza home huku akijua walipakodi wake amewafanya vile???
Can I cry?
Chenge kaachiwa kwa dhamana na ameondoka ndani ya gari aina ya Toyota Harrier namba T193 AYL.
Taarifa za kipolisi zinasema mwenye Bajaj ndiye alikuwa na makosa na huenda ndiyo sababu iliyopelekea yeye kukimbia (anageuziwa kibao?)
Kuna walinzi waliokuwa eneo la tukio, huenda hawa wakatoa msaada wa hali halisi. Walinzi hao wanasema kwamba, dereva wa Bajaj alipona gari la Chenge linamfuata upande wake akalikwepa na kuruka ndipo kina dada wa watu waliokuwa wakitokea Club Maisha wakajikuta hawana msaada na kugongwa wakiwa pekee bila dereva. Kwa kuwa dereva hajulikani alipo, kila kitu kitamuelemea yeye na huenda akionekana ataambulia vijisenti akanunue Bajaj zake kadhaa (asiajiriwe tena).
Kuna habari kwamba kina dada hao wanatokea mkoani Mwanza na leo walikuwa waelekee Zanzibar kwa ndege kufanya shopping kabla ya kurejea kwao, mmoja akitajwa kuwa Bi harusi mtarajiwa