Chenge ajiuzulu!

30ab861.jpg
Huyu ni mh anaekwenda kutoa salam ama?nani kamtuma?is he wearing a bullet proof?is he hiding some sort of weapons?Is he in the US or UK?Is he from tz?Nice photo anyways!kwi kwi kwi..!For the guy looks like he's on the dangerous mission!
 
Mwanatanu naona bado unaishi miaka ya 60..umesahau TANU iliungana na TAA na kuform CHAMA CHA MAPINDUZI!

Naomba nikusahihishe TANU iliungana na ASP na kuizalisha CCM.TAA kilikuwa chama kabla ya TANU..

Nadhani hata wewe ungekuwa rais kutokea CCM huwezi mara moja tu ukaamua vita...inatakiwa mbinu kuweza kuwatoa hawo mafisadi ambao chama kimewaleya kwa muda wote huo....mimi nashangaa watu wakimlaumu JK...Yeye amewakuta hawa mafisadi na sasa ameaanza kuwaondoa mmoja mmoja,mnafikiri Chenge asingekuwa waziri hii scandal tungeipata wapi? Besides isingekuwa kubwa kama ilivyo sasa, kuna watu behind the scene ambao wanazivujisha hizi data kuziweka kwenye public eye tofauti na miaka ya nyuma
 
ile habari kuwa serikali yetu iko kwenye AUTO PILOT naona ni kweli kabisa

Nadhani its better serikali nzima ikajiuzulu na sidhani kama kuna mtu ana akili timamu anataka kuwa waziri au kuwa part of this incompetent administration

Hata serikali nzima ikijiuzulu, itakayoundwa itakuwa ya kifisadi vilevile. inabidi Chama cha Mafisadi (CCM) cheyenyewe kiachie ngazi, maana hazina yote ya wana NAMBARI WANI imeoza. tatizo kubwa sasa hivi ni kwamba kuna gap kubwa hapo, maana hata CHADEMA, CUF, NCCR, wote hakuna ambaye yuko tayari kuunda serikali ya kuweza kuongoza nchi hii. wote hao wamekaa ki-nambari wani nambari wani hivi, wana hangover ya uccm. mimi nadhani inabidi kuwa na serikali ya mpito inayojumuisha watu mbalimbali mpaka hapo uchaguzi mkuu ufanyike. serikali ya mpito iunde katiba mpya na chini ya katiba hiyo, kusiwe na nafasi ya kuwa na wababaishaji ambao wanaweza kutamba katika ubabaishaji. Hili wimbi la UKIMA (UKOSEFU WA KINGA KWA MAFISADI) inaonekana bado linavuta kasi, mpaka litakapotulia nadhani shingo nyingi sana zitaanguka. kama ni watu wa maombi, vyama vya siasa, "whistle blowers", watu wa dini, JF, waandishi wa habari MAKANJANJA, na wengineo wote wanaosababisha ugonjwa huu wa UKIMA, waendelee kufanya usafi huu, nadhani tutaweza kuhamasisha wananchi tudai serikali ya mpito
 
Mwanatanu,
Achana na hizi za kujichombeza-chombeza kwa kisura Vasco da Gama. Kisura wako hajafanya lolote kuwaibua mafisadi. Isingekuwa hawa mafisadi kufanya mahesabu yao vibaya, tungeendelea kukiona cha moto wakati wao wakiendelea kuiba.

Kama kisura wako angekuwa mwadilifu, kwanini aliteua hata ambao waliokuwa wamekataliwa hapo awali, Lowassa n.k.?? JK ni wa kuondoa sio kupongeza.

I believe i am entitled to my opinion...Kama wewe unaona najichombeza basi kheri.

Unakataa kuwa mafisadi hawakuwepo toka enzi za Nyerere?au mwenzangu ni wa enzi za RUKSA?
 
Nimeimba sana kwanza muelewe kuwa hawa mafisadi hawajaanza leo walikuwepo toka era ya Nyerere na walikuwa wakibebwa na kulindwa na CCM.

Sasa ametokea Mzalendo kisura wetu Kikwete kwa baraka zake i mean ameruhusu system iwaweke hawa mafisadi hadharani hii ina maana wakati wa Nyerere,Mwinyi na Mkapa hawa mafisadi walifichwa na kulindwa,hawa mafisadi ni very powerful na wana mtandao mkubwa sana...huwezi ukawa rais na ukaweza kuvunja mtandao wenye mizizi takriban 50yrs overnight.

Naimba tena tumpe credit JK kidogo



Ndugu MWANATANU, are you serious??
I hope you are just kidding!
Kwa kufikiria kwako wewe unafikiri JK hayumo umo? Hapa tunazunguka tu, hawa wezi walipokuwa wakiiba yeye alikuwa anaona na ananyamaza kimya or worse he's into it too. Na kama alinyamaza kimya, it doesn't make him right, he is very wrong as them.
ACHA KUMFAGILIA HUYO KISURA WAKO HAPA JF!!! OH AU NDUGUYO NINI?Maana wewe unaonekana huna uchungu na TANZANIA.
 
Chenge kujiuzulu ni hatua nzuri, tumedai sana hapa kuwa aachie ngazi, lakini bado hata sasa baada ya kujiuzulu bado tuna wasiwasi kuwa huenda hii ikawa ni fursa kwake kuendelea kujitumbulia mabilioni yetu ambayo kwake ni "vijisenti" tu! Inapaswa hatua za kisheria dhidi yake zifuate, lakini sioni matumaini ya hili kutokea wakati waliomtangulia kina Lowassa, Karamagi na Msabaha wanaendelea kutumbua huku wakisifiwa na chama chao kuwa ni "mashujaa" kwa kujiuzulu! La pili ni kuwa huyu fisadi amesubiri hadi kutuhumiwa na SFO ya UK ndipo akachukua hatua ya kujiuzulu. Ikumbukwe kuwa SFO hawakuwa wanachunguza habari za Chenge, wao walikuwa wanafuatilia ufisadi wa kampuni ya BAE iliyouzia Tanzania radar, ndipo wakagundua pia kuwa Chenge alilambishwa mshiko katika dili hilo. Kampuni hiyo ya BAE pia inatuhumiwa kuiuzia serikali ya Saudi Arabia vifaa vya kijeshi vya zaidi ya pound 40bn, ambako madalali fisadi walilamba rushwa ya kueleweka. Tony Blair alipokuwa waziri mkuu alizuia ucunguzi dhidi ya BAE katika dili la Saudi Arabia usifanyike, akitoa sababu feki za kuogopa kukosa ushirikiano wa waarabu hao katika vita ya Iraq, lakini Gordon Brown alipoingia madarakani akaruhusu uchunguzi uendelee, na ndio uliotuwezesha kuyapata haya ya Chenge. Kwa hiyo hii ya Chenge imekuja kama "side effect" ya uchunguzi wa SFO dhidi ya BAE ya UK. Swali ni kuwa sisi tutaendelea kuishi kwa kudandia hadi lini? Yaani system zetu hazina uwezo wa kufichua mafisadi hadi "waibuliwe kwa bahati" kwenye uchunguzi wa wengine? Kumbukeni hata masuala ya kina Balali na EPA huko BoT yaliibuliwa na kampuni ya kigeni ya auditors, Deloitte and Touche (ambayo hata hivyo ilitimuliwa na waziri aliyekuwepo) nakuja kuthibitishwa na kampuni nyingine ya kigeni pia iliyopewa tenda hiyo na CAG. Kwa hiyo kumbe sisi wenyewe hatuna uwezo wa kudhibiti mifumo yetu ya uwajibikaji, ama saratani ya ufisadi imeenea kila mahali, hakuna wa kuaminiwa tena! Labda sasa JK aiombe SFO ya Uingereza ije kumchunguzia serikali yake yote, pengine ataamini ripoti yao kuliko vyombo vyake vya ndani!
 
Hili linchi linatuumiza tu roho na kutia uvivu, Tumuuzie mmarekani afanye Dampo la Nyuklia tugawane pesa kila mtu akatafute maisha kwingine.

Imefikia sehemu nimekata tamaa.

Umekata tamaa? ndugu yangu that is the good news. the bad news ni kwamba utaendelea kuliwa tu kwenda mbele, jamaa hawaangalii kama umekata tamaa au umeunga tamaa. tuendelee kutafuta ufumbuzi tu ndugu yangu
 
Naomba nikusahihishe TANU iliungana na ASP na kuizalisha CCM.TAA kilikuwa chama kabla ya TANU..

Nadhani hata wewe ungekuwa rais kutokea CCM huwezi mara moja tu ukaamua vita...inatakiwa mbinu kuweza kuwatoa hawo mafisadi ambao chama kimewaleya kwa muda wote huo....mimi nashangaa watu wakimlaumu JK...Yeye amewakuta hawa mafisadi na sasa ameaanza kuwaondoa mmoja mmoja,mnafikiri Chenge asingekuwa waziri hii scandal tungeipata wapi? Besides isingekuwa kubwa kama ilivyo sasa, kuna watu behind the scene ambao wanazivujisha hizi data kuziweka kwenye public eye tofauti na miaka ya nyuma
Neno mapinduzi then ndio linapata maana kamili hapa..na kama mh rais anataka kuwa upande wa wananchi ambao ndio upande mzuri wa historia..then ni yeye mwenyewe atakaye yasimamia mapito haya ili kusiwe na vurugu za mapinduzi kwa sababu hakutakuwa na reconciliation tena kama akisubiri mapinduzi yatokee!Ni wakati wake wa kuitumia nafasi hii!Hata kama ni kushirikiana na viongozi wengine bila kujali itikadi!mradi kuwe na timu yenye kuwafanyia kazi wananchi na sio yenye kufanyiwa kazi na wananchi na kuwanyonyahuku wakipiga domo kuwa wananchi wafanye kazi kwa bidii kwa style ya kilowassa lowassa!It is a defining moment in any defintion of it!
 
Chenge kujiuzulu ni hatua nzuri, tumedai sana hapa kuwa aachie ngazi, lakini bado hata sasa baada ya kujiuzulu bado tuna wasiwasi kuwa huenda hii ikawa ni fursa kwake kuendelea kujitumbulia mabilioni yetu ambayo kwake ni "vijisenti" tu! Inapaswa hatua za kisheria dhidi yake zifuate, lakini sioni matumaini ya hili kutokea wakati waliomtangulia kina Lowassa, Karamagi na Msabaha wanaendelea kutumbua huku wakisifiwa na chama chao kuwa ni "mashujaa" kwa kujiuzulu! La pili ni kuwa huyu fisadi amesubiri hadi kutuhumiwa na SFO ya UK ndipo akachukua hatua ya kujiuzulu. Ikumbukwe kuwa SFO hawakuwa wanachunguza habari za Chenge, wao walikuwa wanafuatilia ufisadi wa kampuni ya BAE iliyouzia Tanzania radar, ndipo wakagundua pia kuwa Chenge alilambishwa mshiko katika dili hilo. Kampuni hiyo ya BAE pia inatuhumiwa kuiuzia serikali ya Saudi Arabia vifaa vya kijeshi vya zaidi ya pound 40bn, ambako madalali fisadi walilamba rushwa ya kueleweka. Tony Blair alipokuwa waziri mkuu alizuia ucunguzi dhidi ya BAE katika dili la Saudi Arabia usifanyike, akitoa sababu feki za kuogopa kukosa ushirikiano wa waarabu hao katika vita ya Iraq, lakini Gordon Brown alipoingia madarakani akaruhusu uchunguzi uendelee, na ndio uliotuwezesha kuyapata haya ya Chenge. Kwa hiyo hii ya Chenge imekuja kama "side effect" ya uchunguzi wa SFO dhidi ya BAE ya UK. Swali ni kuwa sisi tutaendelea kuishi kwa kudandia hadi lini? Yaani system zetu hazina uwezo wa kufichua mafisadi hadi "waibuliwe kwa bahati" kwenye uchunguzi wa wengine? Kumbukeni hata masuala ya kina Balali na EPA huko BoT yaliibuliwa na kampuni ya kigeni ya auditors, Deloitte and Touche (ambayo hata hivyo ilitimuliwa na waziri aliyekuwepo) nakuja kuthibitishwa na kampuni nyingine ya kigeni pia iliyopewa tenda hiyo na CAG. Kwa hiyo kumbe sisi wenyewe hatuna uwezo wa kudhibiti mifumo yetu ya uwajibikaji, ama saratani ya ufisadi imeenea kila mahali, hakuna wa kuaminiwa tena! Labda sasa JK aiombe SFO ya Uingereza ije kumchunguzia serikali yake yote, pengine ataamini ripoti yao kuliko vyombo vyake vya ndani!
Bado tuna uwezo wa kuung'oa ufisadi na mizizi yake yote!Kwa wale waelewa..i dont know about you,tunajua kuwa mh rais ana mamlaka makubwa kupita kiasi yenye kuweza kuutokomeza ufisadi kwa muda mfupi bila ya athari nyingi kutokea!Mwalimu alipata shida wakati wa nyuma kwasababu ya uchache wa wasomi pamoja na wasiwasi wake wa kuwapa madaraka watu wasiokumbatia ujamaa to the fullest!This time Mh rais anatamani angekuwa mwananchi wa kawaida tu!kwani ni wazi kuwa ingekuwa mimi ningekubali kuandika ukurasa mpya wa kihistoria kwa ku"acknowledge" vita viko dhidi ya ufisadi na kukubali hata kupoteza marafiki wa karibu ambao hawana nia nzuri na nchi hii!Aache ile "mob mentality" kwa sababu anapigiwa saluti kila siku na kuitwa mkuu na watu wanaomzunguka na kumfanya asahau kabisa dunia ya watanzania wa kawaida ambao hata mlo kwao ni wa kubabia!This time Mungu yupo upande wa taifa letu kwani inawezekana amesikia kilio cha mnyonge na kusababisha issue hii ya ufisadi isipotee kama viongozi wananvyotaka iwe..badala yake tunataka kuona mbadiliko makubwa na kuwa na serikali mpya kabisa na pia mh rais kuwaomba wananchi msamaha!Na kuhakikisha uwajibikaji unatake place ili iwe funzo kwa yeyote anayekimbilia madaraka kwa nia mbaya!
 
-Wananchi ndio wanachagua wabunge, yes then what? Hiyo siyo sababu ya kumfanya RAISI WA NCHI AWE MJINGA, AFUATE MKONDO. NDIO MAANA TUNASEMA RAIS NA VIONGOZI WAKE SIO COMPETENT. HATA KA-UZALENDO NA NCHI HAWANA.

Je unafikiri watu Tanzania nzima wangekuwa wanapata news za ufisadi kama zinavyotoka mijini wangekuwa wanawachagua hao mafisadi? Au wangekuwa na elimu ya kutosha huko vijijini wangewachagua hao MAJANGILI WA CCM? Kumbuka bado watu hawaelewi tuko katika mfumo gani wa kisiasa/kiuchumi. Watu wachache walioko madarakani na wasomi ndio wanachukua fursa hii kuwaibia wananchi na rasilimali za nchi. It's a shame, big shame to these few selfish monsters.

Lets keep pushing the hot buttons until all these suckers learn the lesson.
 
kufukuzwa au kujiuzulu bt what about the tax payer's money which sits on some offshore account?
 
According to the dataz, ni kwamba alikuwa na barua ya kujiuzulu tayari toka akiwa u-China, ndio maana hakwenda US, hizi filimbi za vijisenti alikuwa anazuga tu kwani alikuwa tayari amemfahamisha rais walipopata habari tu kule China kuwa anajiuzulu mara moja,

More dataz ni kwamba kuna wanasiasa wa hapa bongo wakishirikiana na wa UK hasa Blair, wanamshinikiza Brown, asimamishe uchunguzi wa Radar uliomponza Chenge..........!

tunaendelea kuzitafuta dataz on how it happened.....mpaka Chenge kujiuzulu!

Mkuu FMES,
Sidhani kama ni kweli huyu mkulu Chenge alikuwa tayari kujiuzulu tokea u-China. Ingekuwa hivyo asingewaambia waandishi kuwa hana hilo wazo la kujiuzulu. Kama tujuavyo, wabongo hawajiuzulu mpaka waji..rishie. Kama isingekuwa kuchemsha na msemo wa "vijisenti", labda wangetafuta jinsi ya kuendelea naye.

Halafu Chenge hakuwa na cha kufanya US. Yeye hahusiki kwenye vikao vya UN-General Assembly. U-China alienda kwa ajili ya ile omba omba yetu probably kwenye treni na barabara.

Hiyo ya Blair iko wazi mpaka magazetini wala sio siri maana Blair alishazuia uchunguzi kabla ya Brown kuingia 10 Downing St. Nashauri mkuu aliyekupa data umminye zaidi akupe majina ya hao wakuu wa TZ walio na ubavu wa kumshinikiza Brown maana hizi walizokupa hazi-add up.
 
Hivi jamani huyu Mh.Rais anafanya background check ya wateule wake? kama sivyo ni bora aanze vinginevyo ataweka rekodi ya kiongozi mwenye mawaziri wengi waliojiuzuru kwa kashfa
 
Mkuu FMES,
Sidhani kama ni kweli huyu mkulu Chenge alikuwa tayari kujiuzulu tokea u-China. Ingekuwa hivyo asingewaambia waandishi kuwa hana hilo wazo la kujiuzulu. Kama tujuavyo, wabongo hawajiuzulu mpaka waji..rishie. Kama isingekuwa kuchemsha na msemo wa "vijisenti", labda wangetafuta jinsi ya kuendelea naye.

Halafu Chenge hakuwa na cha kufanya US. Yeye hahusiki kwenye vikao vya UN-General Assembly. U-China alienda kwa ajili ya ile omba omba yetu probably kwenye treni na barabara.

Hiyo ya Blair iko wazi mpaka magazetini wala sio siri maana Blair alishazuia uchunguzi kabla ya Brown kuingia 10 Downing St. Nashauri mkuu aliyekupa data umminye zaidi akupe majina ya hao wakuu wa TZ walio na ubavu wa kumshinikiza Brown maana hizi walizokupa hazi-add up.

Siyo Blair hata Tories sasa wana support SFO wasimamishe uchunguzi lakini sio kwa sababu ya Chenge au BAE bali kwa sababu inawahusisha wazee wa mafuta SAUDIS na inawezekana Saudis Royals involved.

KUBWAJINGA soma hii link
http://www.guardian.co.uk/world/2008/apr/12/bae.defence
 
...ni vigumu sana kumtenganisha kikwete na uchafu kwa kuwa ni rais aliyetokana na mbinu chafu...kwa hiyo simply ni mchafu....ni rais mfujaji wa pesa zetu walipa kodi kwa starehe..hata kama hachukui kama wenzake ...ni rais mwenye kiwango kidogo cha uelewa na usimamizi wa serikali yake...hafai!!!!


Nilikuwa nashindwa tu kuweka maneno kama ulivyoyapanga wewe mkuu ila ndivyo nami navyomona yuhu kiongozi wetu.
 
phillemon mikael

...ni vigumu sana kumtenganisha kikwete na uchafu kwa kuwa ni rais aliyetokana na mbinu chafu...kwa hiyo simply ni mchafu....ni rais mfujaji wa pesa zetu walipa kodi kwa starehe..hata kama hachukui kama wenzake ...ni rais mwenye kiwango kidogo cha uelewa na usimamizi wa serikali yake...hafai!!!!

It is easy to criticise. Nauliza je ni nani angefaa kwa mawazo yako?
 
It is easy to criticise. Nauliza je ni nani angefaa kwa mawazo yako?
Kabla ya kujiuliza kwamba nani anafaa ama nani hafai..ni lazima kwanza hatua zichukuliwe dhidi ya wale ambao hawafahi..wawajibishwe kwanza..then tuangalie wale wanaofaa!Ni maoni yangu tu!
 
Back
Top Bottom