Albaab
JF-Expert Member
- Jun 6, 2015
- 1,606
- 2,281
Kiukweli walichofanyiwa Chelsea ni ungese mtupu! Ni wapinzani wangu lakini kwa hatua hii hata ladha ya Mpira imekufa kabisa!Wamezuia hata washabiki kununua ticket kuingia kuangalia team zao hakuna kununua jezi hakuna kununua au kuongeza mkataba wa mchezaji kama huna nia ya kuuwa team ni nini? mfungie huyo owrner ambaye miaka 19 walifunga macho hata wakati Russia wanapiga Syria na kuuwa watu walikuwa kimyaa leo macho ya blue ndio binadamu hawa wengine mbwa. Hakuna mtu anapenda vita ila sote tunapenda kuona haki na maisha yote kuwa sawa. Russia kauwa sana watu Syria walikuwa wapi hawa UK? Double standard inaumiza sana usiombe ya kukute kuona huthaminiwi kwa sababu ya uraia wako au rangi yako inauma. Watuachie mpira wetu kama wao wanaume waende kupigana. Kama wana jeuri wapokonye Man city na Newcastle maana Saudia na UAE mwaka wa saba wanapiga Yemen na ndege watu kibao wamepoteza maisha hao sio watu?
Mpira unakokotwa na matukio ya kisiasa ya upande mmoja tu, mambo ya kishamba sana.
Wanaikomoa Chelsea baadala ya kumkomoa R.A
Sijapenda kwakweli
YNWA!