Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Utakaa na Mchezaji anayekaa injuries mechi tano anacheza moja kisa ni mchezaji mzuri?ni sawa na Madrid Gareth ni mchezaji mzuri Ila injuries zina ipa team hasara ,anunuliwe savic kuongeza depth ya midfielders
Hizo injury za kante zimeanza lini? Kwamba tuneshindwa kabisa kumvumilia kante?
 
Sasa hapo tunasema makosa yalitokea kwenye build up ya hilo goli.
Silver alinawa lakini Refa hakuona, Liverpool tukaona Faulo lakini haikutolewa. Hapo ikawa ni Advantage kwa Man City, Lakini wakashindwa kuitumia nafasi.

Then kwenye hiyo Move TAA akanawa pia Refa hakuona, Man City wakaomba Faulo lakini hsikutolewa. Hapo ikawa ni Advantage kwa Liverpool na Wakaitumia.

Sasa hapo ilikuwa ni Win Win situation Mkuu but uzembe wa Man City kutokutumia nafasi wanazozipata ndiyo ulioleta Shida.
Football sio ujanja ujanja na kutengenezeana mazingira,matukio haya yangekuwa yanatokea kipindi cha nyuma kweli ila kwa sasa mimi nasema kuna WALAKINI,

siipigi madongo liverpool kwasababu siichukii hata kidogo ila hawa walioleta VAR wametuletea tabu,maana washabiki,wachezaji,makocha na wacheza kamari wote amani imetoweka na naamini kama itaendelea kuwepo kwa miaka 15 ijayo basi VAR ndio utakuwa ugonjwa unaoongoza kuuwa watu zaidi ya UKIMWI.....
 
Tammy Abraham afunga goli lake la kwanza la kwa timu yake ya Taifa
 
Maeneo matatu ambayo Chelsea itahitajika kuziba January kama adhabu itapunguzwa
LB: Lampard ameshamchoka Alonso na huenda January akaruhusiwa kuondoka na mbadala wake anahitajika sana na Chelsea wanamlenga Ben Chilwell wa Leicester city
Winger: Pedro mkataba wake unaishia na Willian bado wako kwenye mjadala wa kusaini mkataba mwingine
Atahitajika winger makini wa kusaidiana na Pulisic na Odoi na anayelengwa hapa ni Jadon Sancho
Striker: Olivier Giroud muda wake darajani umefikia mwishoni na Batsuayi bado hajafikia kwenye viwango vya Lampard. Kwa hiyo striker wa kusaidian na Tammy atahitajiwa sana
 
Bado willian ni muhimu kwa Chelsea ana offer vitu vingi kwenye uchezaji wake labda chelsea wamuuze Kama watapata replacement yake tofauti na hapo Chelsea itastruggle sana.Pedro ndo mchezaji wa kumuuza pale Chelsea.huwezi ukatabiri eti fulani akiongezewa mkataba ataflop kwani wewe ni mungu.
Nadhani hujanielewa. Sijasema ataflop nilichosema ni ile kawaida yake hasa anapotoka kusign mkataba anaanza kulega lega. Yan hizi juhudi unazoziona sasa yawezekana ni mbinu ili asign mkataba kama miaka ya huko nyuma.

Willian ni mchezaji muhimu lakini siyo reliable wakati wote.
 
Kwa mfumo wa Sarri sio huu wa Lampard. Makocha waliopita walikuwa hawaweki nindhamu kwenye kambi mpaka wachezaji wanalalama ovyo wakati wa Sarri. Kwa Lampard mchezaji akicheza ovyo mchezo mmoja tu, next game hana namba na Willian analijua hilo
Ngoja tuone kamari nyingine.
 
Ngoja tuone kamari nyingine.
Inavyoelekea watampa mkataba wa miaka miwili kwa sababu Willian ndio hitaji lake vinginevyo angeshasaini mkataba wa mwaka mmoja kama bodi inavyotaka. Akiwepo Willian na kumleta Jadon Sacho, kama winga ili wasaidiane na akina Pulisic na Odoi, kule mbele tutakuwa tumekamilika itakuwa bado kwenye LB tu ambapo huyo Ben wa Leicester akija, mwakani tunabeba ndoo.
 
Real Madrid add Chelsea star Callum Hudson-Odoi to transfer target list

 
Inavyoelekea watampa mkataba wa miaka miwili kwa sababu Willian ndio hitaji lake vinginevyo angeshasaini mkataba wa mwaka mmoja kama bodi inavyotaka. Akiwepo Willian na kumleta Jadon Sacho, kama winga ili wasaidiane na akina Pulisic na Odoi, kule mbele tutakuwa tumekamilika itakuwa bado kwenye LB tu ambapo huyo Ben wa Leicester akija, mwakani tunabeba ndoo.

Hivi unaijua bei ya Sancho lakini? Kawaulize Manure.

Najua Timu yenu inahela lakini sidhani kama imeshafikia class ya kununua wachezaji wa £130m
 
Inavyoelekea watampa mkataba wa miaka miwili kwa sababu Willian ndio hitaji lake vinginevyo angeshasaini mkataba wa mwaka mmoja kama bodi inavyotaka. Akiwepo Willian na kumleta Jadon Sacho, kama winga ili wasaidiane na akina Pulisic na Odoi, kule mbele tutakuwa tumekamilika itakuwa bado kwenye LB tu ambapo huyo Ben wa Leicester akija, mwakani tunabeba ndoo.
Willian atapewa huo mkataba kwa sababu ya experience yake ila kiukweli kuna uhitaji mkubwa wa kumleta Sancho kwa ajili ya kuchukua ile nafasi ya Willian.
 
Real Madrid add Chelsea star Callum Hudson-Odoi to transfer target list

Hawa Madrid hata kama ni kujenga timu hii sasa inakua ni tamaa. Wana Vinicius Jr, Rodrigo, Hazard, Vazquez, Bale sasa wanamtaka na Odoi. Hii habari niliiona jana ila nikaamua kuipuuzia
 
Unasahau eneo muhimu la goalkeeper, sasa hv tatzo kubwa tulionalo kwa chelsea ni goalkeeper

Kepa amekuwa hana msimu mzuri kwa kipindi hki, anahitaji changamoto
Maeneo matatu ambayo Chelsea itahitajika kuziba January kama adhabu itapunguzwa
LB: Lampard ameshamchoka Alonso na huenda January akaruhusiwa kuondoka na mbadala wake anahitajika sana na Chelsea wanamlenga Ben Chilwell wa Leicester city
Winger: Pedro mkataba wake unaishia na Willian bado wako kwenye mjadala wa kusaini mkataba mwingine
Atahitajika winger makini wa kusaidiana na Pulisic na Odoi na anayelengwa hapa ni Jadon Sancho
Striker: Olivier Giroud muda wake darajani umefikia mwishoni na Batsuayi bado hajafikia kwenye viwango vya Lampard. Kwa hiyo striker wa kusaidian na Tammy atahitajiwa sana
 
Unasahau eneo muhimu la goalkeeper, sasa hv tatzo kubwa tulionalo kwa chelsea ni goalkeeper

Kepa amekuwa hana msimu mzuri kwa kipindi hki, anahitaji changamoto
Huyo anachohitaji ni coaching tu. Kepa ni kipa mzuri sana, Lampard anataka kumleta kocha wake wa makipa kule Derby County, bwana Given
Kumbuka kuwa huwezi kuwa na makipa wengi wa kaliba ya juu kwenye timu moja, hawatakaa, makipa sio kama wachezaji wa uwanjani. Kipa hachoki useme utampumzisha, mara chache sana kipa kwenda majeruhi. kama Kepa hafai ni wa kuuza na kumleta mwingine kitu ambacho sitegemei kitatokea
Anahitaji kufanyiwa technical, psychological and mental coaching tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom