Christian Pulisic; karibu darajani japo mwez wa nane mbali sana
Kutokana na kuonekana upepo kukata kwa Williun na Pedro, huu usaji ulikuwa bingo sana kumalizia msimu kwa Chelsea.... Okay...! Kwa sasa Hazard na Kante ndio waendeshaji wa mashambulizi kwa Chelsea(inawezekana Sarriball iliwahitaji pia Williun na Pedro kwenye kuendesha timu kwenda mbele).
Kuna wakati timu inamuelemea zaidi Kante, vivyo hivyo kwa Hazard. lakini pia kuna wakati timu inahitaji mtu wa kumsaidia Hazard, haswa kutokana na mara kadhaa amekuwa drafted kama mshambuliaji wa katikati.... Pulisic ni suluhisho kwa sasa.
Pulisic angeichukua ile flank ya kulia, kushoto awe mwenye timu Hazard na katikati aendelee kuendesha Kante..... Hii ingekuwa na faida sana kwa Chelsea kuelekea kuumaliza msimu kwa tumaini la kujikita zaidi ndani ya top 4.
Huyu ni mtu sahihi sana kama mbadala wa Pedro na Williun msimu huu. Bado sijaijua target ya Marina Granovskaia, inawezekana Sarri hana shida na miguu ya bwana mdogo huyu kwa sasa, au inawezekana hizi ni miongoni mwa zile sajili za Boss himself.