Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Goli la Chelsea lilifungwa na Willian kunako dakika ya 62 kwa shuti zuri lililopita miguuni mwa mabeki wa Barcelona.

Kwa sare hiyo Barcelona imekuwa na faida ya goli moja la ugenini, kabla timu hizo hazijakutana tena katika mchezo wa marudiano utakaochezwa kwenye Uwanja wa Camp Nou, Jumatano ya March 14 2018.
 
Na itakua hivi hivi shambani kwao nou camp
eb7810dd3508080bedf24c819787b917.jpg
 
Goli la Chelsea lilifungwa na Willian kunako dakika ya 62 kwa shuti zuri lililopita miguuni mwa mabeki wa Barcelona.

Kwa sare hiyo Barcelona imekuwa na faida ya goli moja la ugenini, kabla timu hizo hazijakutana tena katika mchezo wa marudiano utakaochezwa kwenye Uwanja wa Camp Nou, Jumatano ya March 14 2018.
Numbisa wewe chama gani? Ili nikupe pole zako mkifungwa.
 
‘There’s still 90 or 120 minutes to play and we’ll go with everything to try to get into the next round!’ Cesar Azpilicueta
 
Willian: Man of the match:

Kwa nini Conte huwa hampi majukumu stahiki Willian kama alivyofanya jana? mchezaji wa caliber ya Willian anaingizwa substitute kama vile hana manufaa zaidi ya substitute kweli!. Mchezaji ambaye ni creative kwenye kutengeneza nafasi, ana mashuiti ya nguvu. Ni mchezaji nadhani anayeongoza championship katika kufunga magoli nje ya box. Katika mchezo wa jana katika shots 11 za Chelsea yeye alipiga shots 4 (kati ya hizo 2 ziligonga mwamba) na kuwa mchezaji aliyepiga shots nyingi zaidi akifuatiwa na Hazard mwenye shots 2. Goli alilofunga baada ya kuwahadaa zaidi ya wakabaji wa Barca kama nane hivi na kupeleka shuti la kisomi pembeni bila hata mmoja ya wakabaji kuwazia kama angepiga hivyo. Mtu mwenye akili kama Wilian halafu hapewi priority kwenye startup XI ya Conte
 
lembu,conte ni chizi yaani anamapungufu mengi sana unapochukua ubingwa wa ligi kwa nchi husika tayari wewe unacheza UEFA kombe hili kiuzoefu ni mbinu tu zitakubeba sasa wachezaji wa mbinu wameuzwa,ameuza costa,ameuza matic hawa ndio walikuwa wanatuliza chelsea na kuleta ubingwa fikiria mechi zote ngumu anachezesha viungo tu sasa unashindaje UEFA kwa mtindo ule! conte anaonesha uzaifu wake if possible conte go out
 
Mkuu kwenye ukweli tuseme tu. Jana konte angemchezesha striker Chelsea wangeibuka washindi. Lakini kitendo cha kumpanga hazard kama false striker amearibu mwenyewe.
Conte kashajibu kuwa kwa Barcelona angeweka striker Chelsea ingezidiwa na ingefungwa 4 au 5 bila kama anavyofanya kule kwenye laliga. Kasema alifanya hivyo makusudi "It was a tactical plan" na huo mchezo walishapanga kucheza hivyo ila tu kosa moja la beki mchanga likaigharimu timu
Chelsea news: Antonio Conte explains why he benched Morata & Giroud | Metro News
 
Nimewafollow baadhi ya mastaa wetu katika Instagram zao na wengi baada ya match dhidi ya barcelona walionekana kusikitika kuipata sare
Wengi wakiwemo hazard ,Willian, alonso, kante, christensen, aspiliqueta wanaamini watapambana kufa kupona pale nyumbani kwa barcelona mi nasubiri ili kuona kile watakachokionesha uwanjani siku hiyo
Narudia tena wakifanikiwa kuitoa hongera zao nyingi sana
Nawatakia mpambano mwema
 
Nimewafollow baadhi ya mastaa wetu katika Instagram zao na wengi baada ya match dhidi ya barcelona walionekana kusikitika kuipata sare
Wengi wakiwemo hazard ,Willian, alonso, kante, christensen, aspiliqueta wanaamini watapambana kufa kupona pale nyumbani kwa barcelona mi nasubiri ili kuona kile watakachokionesha uwanjani siku hiyo
Narudia tena wakifanikiwa kuitoa hongera zao nyingi sana
Nawatakia mpambano mwema
Mkuu unakosa imani na timu hata kabla haujaingia uwanjani!? Sasa kila shabiki akiwa kama ww timu itapata wa kuisindikiza Nou Camp
 
Mkuu unakosa imani na timu hata kabla haujaingia uwanjani!? Sasa kila shabiki akiwa kama ww timu itapata wa kuisindikiza Nou Camp
Mkuu nina imani ila wakati mwingine unaweza usiielewe hii team maana uwanjani hujui watakupa nini na kwa wakati gani
Imani yangu itarudi wakiitoa barcelona maana walinikera sana dhidi ya wattford
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom