Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

282acf8e6d6aab04a1663cf900f8dd4b.jpg

Dah Newcastle amenyakua Ubingwa akitokea nafasi ya Pili huku akiwa aliachwa kwa alama 7 na Brighton zikiwa zimebaki mechi tatu ligi kuisha,Brighton wakapoteza mechi mbili na kutoka sare lakini Newcastle akashinda zote na kutawazwa Bingwa leo! Dah nasi Tuhakikishe hatufanyi mchezo kama Brighton maana wamenyang'anywa tonge mdomoni
 
Kiungo wa Chelsea N'golo Kante amepigiwa kura na kushinda tunzo ya Mchezaji Bora wa Umoja waandishi wa habari za mpira ya mwaka 2017.

Kante amemshinda mchezaji mwenzake wa Chelsea Eden Hazard kwenye tuzo hiyo FWA - Football Writers' Association, japo Hazard nae kaonekana kung'ara msimu huu. Dele Alli wa Tottenham amekuwa mshindi wa tatu.

Kante ni mchezaji wa 18 kushinda tuzo za PFA na FWA kwa pamoja kwa msimu mmoja. Wengine ni Thierry Henry na Cristiano Ronaldo ambaye alishinda hivyo mara mbili.

Kante na Hazard wamepata zaidi ya asilimia 65 ya kura zote. Kante atakabidhiwa tuzo yake siku ya tarehe 18 mwezi May
 
Taarifa ya Tianjin.

Tianjin Quanjian imejibu taarifa zinazo wahusisha na usajili wa mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa.

Sky Sports jana walitoa taarifa kwamba klabu hiyo ya Ligi kuu ya China wanajiamini kwamba watamsajili Costa majira ya kiangazi lakini wamedai kwamba mazungumzo bado hayajaanza.

Taarifa ya klabu inasomeka hivi...

"Kwa vyombo vya habari na mashabiki wa soka, kuhusiana na tetesi zinazoendelea kuhusu mchezaji wa Chelsea, Diego Costa kujiunga na Tianjin Quanjian, Klabu ingependa kuweka wazi kwamba hakuna mazungumzo ambayo yamefanyika kuhusu uhamisho huo."
6b4d27782503d5d3e63e93dea19ffedd.jpg

Ni striker mZuri, lakini anaweza kwenda tu, the way Conte anavyopanga kikosi chake anaweza kupata striker mwingine na akawa mzuri tu, hiyo pesa ya Wachina itatusaidia sana kupata wing back wa kumsaidia Moses na pia kupata mido ya kumsaidia Matic, pesa y Hazard ni kumtafuta striker mzuri na Hazard mwingine wa bei rahisi, na Chenji itakuwa ya Dirisha dogo January
 
Chelsea team tonight: Courtois; Azpilicueta, David Luiz, Cahill (c); Moses, Fabregas, Matic, Alonso; Pedro, Diego Costa, Hazard.

Substitutes v Middlesbrough - Begovic, Terry, Zouma, Ake, Chalobah, Loftus-Cheek, Willian
 
Aweka nyingine kabatini.

N'Golo Kante amepigiwa kura nyingi za kuwa mchezaji bora wa mwaka wa EPL kutoka kwa chama cha waandishi wa habari wa Uingereza.

Kante amejikusanyia kura nyingi kutoka kwa wanachama 340 wa waandishi wa habari wa nchini Uingereza akiwazidi Eden Hazard namba mbili na Dele Alli namba tatu.

Kante ni mchezaji wa tano katika misimu sita kukamilisha tuzo mbili kubwa kwa msimu mmoja baada ya hapo awali kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka kwa kupigiwa kura na wachezaji wenzake.

Kante usajili wa majira ya kiangazi kutoka Leicester atakuwa mchezaji wa kwanza wa ndani ( Sio eneo la Golikipa ) kutwaa mataji mara mbili mfululizo akiwa na vilabu viwili tofauti kama Chelsea wakifanikiwa msimu huu.

Alisema," ni heshima kubwa sana kutwaa tuzo hii. Kukiwa na wachezaji wengi wazuri sana kwenye kikosi cha Chelsea na ligi kwa ujumla kwa chama cha waandishi wa habari kunichagua mimi ni swala la kujivunia sana."

Orodha kamili ya wachezaji waliokuwa wanashindania hii tuzo:-

Sergio Aguero (Man City), Toby Alderweireld (Tottenham), Dele Alli (Tottenham), Cesar Azpilicueta (Chelsea), Diego Costa (Chelsea),

Philippe Coutinho (Liverpool), Jermain Defoe (Sunderland), Ben Foster (West Brom), Eden Hazard (Chelsea), Zlatan Ibrahimovic (Manchester United),

Harry Kane (Tottenham), N'Golo Kante (Chelsea), Anthony Knockaert (Brighton),

David Luiz (Chelsea), Romelu Lukaku (Everton), Alexis Sanchez (Arsenal), Gylfi Sigurdsson (Swansea).
b5a7a391885c4655ede1b681ade095da.jpg
 
Rekodi ya Dunia kwa Costa ?

Diego Costa anaweza kusaini kwa Tianjin Quanjian,lakini kama tu wanaweza kutoa kitita cha pauni milioni 127, kwa ajili yake , kwa mujibu wa taarifa kutoka SFR Sport.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa amekuwa akihusishwa na kuhamia nchini China tangu mwezi januari, lakini Chelsea hawapo tayari kumuachia Costa bila kupigana.

Rekodi ya uhamisho wa Dunia kwa sasa inashikiliwa na Paul Pogba alipohamia Manchester United kwa ada ya pauni milioni 89 kutoka Juventus majira ya kiangazi yaliyopita.
3e3115716692026c6e9897d3492f1dd8.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom