Mkuu
Manumbu kuna stats ameleta mkuu
kalou hapo juu zimekaa Pouwa sn..!
Nini mtazamo wako ktk kiwango cha Chelsea Tangu msimu umeanza Mpk sasaivi maana kuna wadau wanasema kasi ya Chelsea imepungua sio Km mwanzo Je wewe unalionaje Hilo?
Kuna mambo mawili ambayo swali lako linajaa humo, kuna moja, kasi ya timu kupungua na pili, Diego Costa kuonekana kama kasi imepungua
kwa mtazamo wangu, Pengo la Ramiles liko wazi sana, jamaa hana vitu vingi lakini focus yake kubwa ni vipi timu itapata ushindi, same kama anvyocheza Fabregas, ni aina ya wachezaji wanojaribu kupush timu kwa kuangalia mianya yote yenye kuleta faida kwa timu
kuumia kwa Ramires kulimuweka William kwenye hiyo nafasi kama mchezaji wa first 11 na sio kama sub tena, uchezaji wa William, Hazard na Oscer almost unafanana japo kuna tofauti ndogondogo, ni wachezaji wanaopenda kuhold sana mipira na pia wana ile hali ya kujiamini kuwa anaweza yeye mwenyewe kupasua ngome na kuingia ndani ya box, ni aina nzuri ya uchezaji lakini kwa kiasi fulani unaweza kupunguza kasi ya mchezo kwani kunakuwa hakuna ile team work, hao ni wachezaji wazuri sana kwenye timu lakini sio wote wacheze kwa pamoja kwa 90mins,
Ramires na Fabregas ni watu wa kuachia mipira, hivyo kila mtu anajua anytime atapokea mpira kutoka kwa hao viungo washambuliaji
Kasi ya Diego sio kama imepungua bali ni aina ya uchezaji wa Hazard, William, Oscer ndio unamfanya Diego ashindwe kufunga kama mwanzo, kama nilivyoeleza hapo juu, hao ni wachezaji wa kuhold na kujaribu kufunga wenyewe hata pale panapoonekana kuna ugumu, hatuwezi sema magoli yote yafungwe na Diego lakini Ki ukweli Diego anajua hasa siri ya kufumania nyavu, na yeye ni striker wa mwisho kabisa, na anajua kujiposition vizuri, na ndio maana Fabregas alikuwa anamchungulia kila saa na kumuona alipo, sasa Walliam, Hazard na Oscer wakiwa wanaingia kwenye (box) territory yake anapoteza position na mwisho anakuwa anasubiri rebounce tu
Na hope Ramires akirecover fully kasi yetu itarudi kama kawaida
japo inaonekana kama kasi imepungua still Chelsea ni timu nzuri sana, na mwaka huu tutafanya maajabu sana, kuna kila dalili ya kubeba makombe matatu kati ya manne tunayogombania mpaka sasa