Chivundu
Platinum Member
- Dec 17, 2012
- 13,055
- 26,194
Wema una mipaka yake ukivuka mipaka unabadilika kuwa ugoigoi
Afu pia kuna wale ukiwafanyia wema, wanatafsiri ni udhaifu na kutaka kuutumia kukuumiza tena. 😊
Wema una mipaka yake ukivuka mipaka unabadilika kuwa ugoigoi
Hakika, unaonekana goigoi kabisaAfu pia kuna wale ukiwafanyia wema, wanatafsiri ni udhaifu na kutaka kuutumia kukuumiza tena. 😊
Uko sahihi, ilikuwa ni challenge ili tupanue mjadala.🤔🤔🤔🤔🤔🤔
Kuna watu wamesema kua ni mbaya
Kuna watu wanasema et ni mwema
Unajua huyo inaedaiwa alituma watu kuua anaweza kusema aliona tishio kwa usalama wake na nchi
Akaamua kuchukua maamzi magumu utamuamini?
Waliouwawa/ kujeruhiwa nao watasema waliona tishio la huyo mtu kwa nchi na uchumi na sababu zingine telee
so wakaona ngoja waingie front
Ndio yakatokea yaliyotokea
In fact kila mtu upande utajihesabia haki na kuona uliamua sahihi
Sasa kinachobaki ni wewe unaetazama unatazama kwa jicho gani?
Hapo nimekujibu tayari 😊
Tafadhari usiniombe jibu lingine babie 💋
Ukitumia nadharia/falsafa ya Johari Window utaweza kupambanua binadamu tulivyo. Hatutabiriki yan au ni vigumu sana mtu kujifunua/kujiweka wazzi hadi wenzake wamfahamu kwa kiundani wake i.e ni mwema au ni mbaya. Itategemea yule mtu anayefanya Tathmini juu ya mhusika. Wewe unayemwona Mbaya kwako ni Mwema kwa wenzio.& vice versa. Yule anayeonekana Leo ni mwema Kesho anaweza akaonekana ni Mbaya hadi waliosema ni Mwema wakashangaa n.k.n.k.Kwenye hii dunia vitu vingi vimeumbwa viwili viwili: binadamu, wanyama, wadudu
Hata kwenye tabia zipo nzuri na zipo mbaya
Watu wapo wema na wapo wabaya
Hapa sina maana ya muonekano wa mtu, I'm talking about character, kwa sababu tabia yako ndiyo itatuambia wewe ni nani, na tabia yangu ndiyo itawaambia mimi ni nani
Sasa je, tabia za nje zinatosha kumjua mtu kuwa ni mbaya au mwema?
Kwa mtazamo wangu jibu ni ndiyo, ila si mara zote tabia ya nje huonyesha kilichopo ndani
Kuna watu wanaonekana wema sana, lakini ndani wamejaa hila
Na kuna watu wanaonekana wakali au wagumu, lakini ndani wana mioyo safi sana
Lakini ukweli ni kwamba, actions speak louder than words
Mwisho wa siku tutakutambua kwa matendo yako
Sasa ni matendo gani ukiyaona kwa mtu unahitimisha kuwa huyu ni mtu mwema?
Kwangu mimi, mtu mwema nampima kwanza kwa upendo alionao kwa wengine
Mtu mwema mara nyingi habebi chuki wala roho mbaya kwa wengine
Mara nyingi watu wema huwa watulivu wanapoamua mambo, kwa sababu wanaamini wakifanya haraka wanaweza kusababisha matatizo au hasara kwa wengine
Watu wema hujali hisia za wengine Kama hawezi kukusaidia, mara nyingi hayupo tayari kukuumiza au kukupa matatizo
Mtu mwema hufurahia kuona wengine wakifanikiwa
Akiona mwenzake amepiga hatua hasemi
(Kwa nini yeye?)Badala yake anasema, Hongera🤗
Anaamini mafanikio ya mwingine hayapunguzi nafasi yake
Mtu mwema akimkosea mtu huwa yupo tayari kuomba msamaha
Na akikosolewa hasikii vibaya kila wakati, kwa sababu anajua hakuna binadamu mkamilifu
Kwa hiyo ukipata mtu wa aina hii kwenye maisha yako, usimchukulie poa
Watu wema ni wachache kuliko tunavyofikiri
Mara nyingi huwa ndiyo watu wanaokupa amani ya moyo wanakushauri kwa faida yako hata kama ukweli unauma wanakuombea mema hata ukiwa haupo nao, na wanabaki upande wako hata pale ambapo hawapati faida yoyote kutoka kwako
Ukiwa na mtu mwema karibu yako, mara nyingi unajikuta hata wewe unabadilika na kuwa mtu bora zaidi Positive people create positive lives
👇
Sasa twende kwa mtu mbaya...
Mtu mbaya mara nyingi hubeba chuki dhidi ya wengine
Moyo wake huwa kama umekufa ganzi, hana anachojali kuhusu wengine
Hata kama hana cha kukusaidia, atafanya juu chini akupe maumivu
Mtu mbaya marafiki zake ni unafiki, uchonganishi, umbeya, ubinafsi, chuki na husda
Mtu mbaya hataki kuona wenzake wakifanya vizuri
Anataka yeye ndiye awe top kwenye kila kitu
Akiona wenzie wanasifiwa, roho inamnyonga akiamini hawastahili
Hufurahia maanguko ya watu
Yule alikuwa anajidai, sasa amekuwa kama sisi kiko wapi🤣
Mtu mbaya hubeba chuki ambayo mwisho wa siku hummaliza yeye mwenyewe kidogo kidogo
Lakini pia ni hatari kua karibu yake maana chuki aliyoificha ndani akiitoa njee ni majanga
Anaweza kutabasamu mbele yako, lakini ndani anateseka kwa sababu tu huwezi kuanguka kama anavyotamani
Na kitu kingine nilichokiona, mtu mbaya huwa ni mgumu sana kufurahia mafanikio ya wengine
Kila zuri analigeuza baya kila mafanikio anaona kuna mchezo umefanyika utasikia
(hapa si bure kuna kitu)
Shida ya kuwa karibu na mtu wa aina hii ni kwamba taratibu utaanza kupoteza amani yako bila kujua
Atakuvuruga kisaikolojia, atakufanya uwaone wengine wabaya kama yeye, atakukatisha tamaa kila unapopiga hatua na wakati mwingine anaweza kuwa sababu ya wewe kuharibu mahusiano yako na watu wasiokuwa na kosa
Watu wabaya hua pia wanapenda wakikosana na watu na wewe eti ukosane nao pia hua wanapenda kurithisha uadui🤣🤣
Watu wa aina hii wakishindwa kukutumia, wanaanza kukuchafua Ndiyo maana kuna msemo unasema, show me your friends and I'll tell you who you are
Mara nyingi tabia huambukiza, hivyo ukikaa sana na mtu mwenye roho mbaya bila kuwa makini, unaweza kujikuta unaanza kufanana naye bila hata kugundua
Sasa hapo tumeona baadhi ya tabia za watu wema na watu wabaya na huo ni mtazamo wangu
Wewe ongezea...
Ni tabia gani ukiiona kwa mtu unaamini kabisa huyu ni mtu mwema?
Na ni tabia gani ukiiona unaona huyu ana roho mbaya?
Halafu ukijipima wewe mwenyewe, kwa tabia zako za ndani na nje unajiona upo upande gani?
Happy Tuesday 😊
ShesRise_1 ✋️
Ohoo sawaI am kind to everyone,But if you're unkind to me,
Then kindness is not what you'll remember me for.
We acha tu maswali ni mengineNje ya mada!
Hivi kuna utafiti wowote uliowahi kufanyika juu ya uwezo wa wabongo kuelewa na kulijibu swali? Kama upo naombeni link.
Love you 😍Uko sahihi, ilikuwa ni challenge ili tupanue mjadala.
Na kwa majibu yako ndio maana tunapata kipimo cha wema au ubaya according to….
1.Culture
2.Dini
3.Sheria za nchi
4.sheria za kimataifa.
5. Individual (msingi wa mada yetu ya leo)
Watu karibu wote wamejibu vizuri, mada nzuri.
KabisaPeople change.Unaweza kumwona mwema kumbe ndiye adui yako namba 1.
Nimeshindwa kujibu swali aisee
Upo sahihi si katai kumfanyia utafiti mtu tena ule wa kina kama unavyosema ni kweli ndio utaweza kumfahamu zaidiUkitumia nadharia/falsafa ya Johari Window utaweza kupambanua binadamu tulivyo. Hatutabiriki yan au ni vigumu sana mtu kujifunua/kujiweka wazzi hadi wenzake wamfahamu kwa kiundani wake i.e ni mwema au ni mbaya. Itategemea yule mtu anayefanya Tathmini juu ya mhusika. Wewe unayemwona Mbaya kwako ni Mwema kwa wenzio.& vice versa. Yule anayeonekana Leo ni mwema Kesho anaweza akaonekana ni Mbaya hadi waliosema ni Mwema wakashangaa n.k.n.k.
Sawa mahi haya niambie ishara ambazo ukiziona unaanza kuhisi huyu mbaya au ni mwemaYani hapa pagumu sana ni kuishi kwa akili tu na mtu yeyote unayekutana nae.
In fact,Kwenye hii dunia vitu vingi vimeumbwa viwili viwili: binadamu, wanyama, wadudu
Hata kwenye tabia zipo nzuri na zipo mbaya
Watu wapo wema na wapo wabaya
Hapa sina maana ya muonekano wa mtu, I'm talking about character, kwa sababu tabia yako ndiyo itatuambia wewe ni nani, na tabia yangu ndiyo itawaambia mimi ni nani
Sasa je, tabia za nje zinatosha kumjua mtu kuwa ni mbaya au mwema?
Kwa mtazamo wangu jibu ni ndiyo, ila si mara zote tabia ya nje huonyesha kilichopo ndani
Kuna watu wanaonekana wema sana, lakini ndani wamejaa hila
Na kuna watu wanaonekana wakali au wagumu, lakini ndani wana mioyo safi sana
Lakini ukweli ni kwamba, actions speak louder than words
Mwisho wa siku tutakutambua kwa matendo yako
Sasa ni matendo gani ukiyaona kwa mtu unahitimisha kuwa huyu ni mtu mwema?
Kwangu mimi, mtu mwema nampima kwanza kwa upendo alionao kwa wengine
Mtu mwema mara nyingi habebi chuki wala roho mbaya kwa wengine
Mara nyingi watu wema huwa watulivu wanapoamua mambo, kwa sababu wanaamini wakifanya haraka wanaweza kusababisha matatizo au hasara kwa wengine
Watu wema hujali hisia za wengine Kama hawezi kukusaidia, mara nyingi hayupo tayari kukuumiza au kukupa matatizo
Mtu mwema hufurahia kuona wengine wakifanikiwa
Akiona mwenzake amepiga hatua hasemi
(Kwa nini yeye?)Badala yake anasema, Hongera🤗
Anaamini mafanikio ya mwingine hayapunguzi nafasi yake
Mtu mwema akimkosea mtu huwa yupo tayari kuomba msamaha
Na akikosolewa hasikii vibaya kila wakati, kwa sababu anajua hakuna binadamu mkamilifu
Kwa hiyo ukipata mtu wa aina hii kwenye maisha yako, usimchukulie poa
Watu wema ni wachache kuliko tunavyofikiri
Mara nyingi huwa ndiyo watu wanaokupa amani ya moyo wanakushauri kwa faida yako hata kama ukweli unauma wanakuombea mema hata ukiwa haupo nao, na wanabaki upande wako hata pale ambapo hawapati faida yoyote kutoka kwako
Ukiwa na mtu mwema karibu yako, mara nyingi unajikuta hata wewe unabadilika na kuwa mtu bora zaidi Positive people create positive lives
👇
Sasa twende kwa mtu mbaya...
Mtu mbaya mara nyingi hubeba chuki dhidi ya wengine
Moyo wake huwa kama umekufa ganzi, hana anachojali kuhusu wengine
Hata kama hana cha kukusaidia, atafanya juu chini akupe maumivu
Mtu mbaya marafiki zake ni unafiki, uchonganishi, umbeya, ubinafsi, chuki na husda
Mtu mbaya hataki kuona wenzake wakifanya vizuri
Anataka yeye ndiye awe top kwenye kila kitu
Akiona wenzie wanasifiwa, roho inamnyonga akiamini hawastahili
Hufurahia maanguko ya watu
Yule alikuwa anajidai, sasa amekuwa kama sisi kiko wapi🤣
Mtu mbaya hubeba chuki ambayo mwisho wa siku hummaliza yeye mwenyewe kidogo kidogo
Lakini pia ni hatari kua karibu yake maana chuki aliyoificha ndani akiitoa njee ni majanga
Anaweza kutabasamu mbele yako, lakini ndani anateseka kwa sababu tu huwezi kuanguka kama anavyotamani
Na kitu kingine nilichokiona, mtu mbaya huwa ni mgumu sana kufurahia mafanikio ya wengine
Kila zuri analigeuza baya kila mafanikio anaona kuna mchezo umefanyika utasikia
(hapa si bure kuna kitu)
Shida ya kuwa karibu na mtu wa aina hii ni kwamba taratibu utaanza kupoteza amani yako bila kujua
Atakuvuruga kisaikolojia, atakufanya uwaone wengine wabaya kama yeye, atakukatisha tamaa kila unapopiga hatua na wakati mwingine anaweza kuwa sababu ya wewe kuharibu mahusiano yako na watu wasiokuwa na kosa
Watu wabaya hua pia wanapenda wakikosana na watu na wewe eti ukosane nao pia hua wanapenda kurithisha uadui🤣🤣
Watu wa aina hii wakishindwa kukutumia, wanaanza kukuchafua Ndiyo maana kuna msemo unasema, show me your friends and I'll tell you who you are
Mara nyingi tabia huambukiza, hivyo ukikaa sana na mtu mwenye roho mbaya bila kuwa makini, unaweza kujikuta unaanza kufanana naye bila hata kugundua
Sasa hapo tumeona baadhi ya tabia za watu wema na watu wabaya na huo ni mtazamo wangu
Wewe ongezea...
Ni tabia gani ukiiona kwa mtu unaamini kabisa huyu ni mtu mwema?
Na ni tabia gani ukiiona unaona huyu ana roho mbaya?
Halafu ukijipima wewe mwenyewe, kwa tabia zako za ndani na nje unajiona upo upande gani?
Happy Tuesday 😊
ShesRise_1 ✋️

Maelezo haya mtu akiyafata anapoteaVyote viwili, Universe haitambui mtu mwema au mbaya, yenyewe ina respond kutokana na vibration unayo provide baada ya tukio kufanyiwa.
Ukiwa mwema hata kidogo then ukawa disappointed na matokeo ya wema huo najua utalalamika sana,
Hapa kuna mfanya na mfanyiwa, aliekufanyia ubaya universe haiwezi muhukumu coz he/she doesn’t give a f*ck so no vibration there
Kwa wewe mfanyiwa kule kulalamika kwako kutapelekea universe ione you deserve kile kitu hence matukio ya aina hiyo ya kufanyiwa ubaya hayataisha maishani mwako mpaka uanze na wewe roho ngumu.
Binadamu ni mbaya pia ni mwema ana darkside na right side
Kinachotokea Kuna ambao Wana balance hizo pande mbili na ambao wanashindwa na kuegemea upande Mmoja pekee .
Hiyo ni illusion uliyo iongelea hapoInteresting…. Wanasema hakuna mtu mbaya/mwema entirely.
Bali mtu anakuwa mwema/mbaya kulingana na vile anavyojisikia kuhusu wewe.
Ndio maana mtu akikuonesha ubaya kwa mara ya kwanza, muamini…. kwasababu kwanini amejisikia kuwa mbaya kwako kwa mara ya kwanza tu? Hajataka kukupa hata grace period…..
Ndio ni kweli kwa wale wenye imani wanaelewa sana hiiIn fact,
mambo yamebadilika sana nyakati hizi,
na uovu mwingi umejificha kwenye wema, na kwahivyo ni vigumu mno kuditect ubaya wa muovu unless kuna Neema na Baraka za Mungu za kipekee na za kutosha ndani yako.
Ni kwelihata hivyo,
ukigusa strengths yake muovu mapema,
kwa kujua au kutokujua, ni wazi unaweza kugundua haraka aina ya ukali wake ambao unaweza kukuwezesha kuhisi, kujua au kutambua nia yake ovu dhidi yako.
Amen ♥️May the blood of Jesus Christ protect you and your family from every form of evil planned against you.![]()
Shukran mkuu hakika umeongea jambo nadhani kila mmoja atafaidika na hii commentBinadamu ni pande mbili kwa wakati mmoja
1. DARK SIDE
Hii ni sehemu ya wivu, hasira, tamaa, ubinafsi, kulipiza kisasi.
Ni ile sauti inayosema "chukua yako kwanza", "watalia wao".
Haitoweki. Iko ndani ya kila mtu.
2. RIGHT SIDE / LIGHT SIDE
Hii ni huruma, upendo, uaminifu, kutoa, kusamehe.
Ni ile sauti inayosema "msaidie", "fanya kilicho sahihi hata kama hakuna anayeona".
Kwa nini wengine wanapotea?
Kama ulivyosema kuna watu 2:
Aina 1: WENYE BALANCE
Wanajua wana darkside, lakini hawaiachii iwaongoze.
Wanaitumia hasira yao kujitetea, sio kuwadhuru.
Wanaitumia tamaa yao kujenga, sio kuiba.
Hawa ndio tunasema "ana moyo mzuri lakini si mjinga"
Aina 2: WENYE KUEGEMEZA UPANDE MOJA
1. Wale wa Light tu → Wanakuwa wajinga. Watu wanawatumia. Mwishoni wanachoka na kuwa wachoyo zaidi ya wengine
2. Wale wa Dark tu → Wanakuwa wakatili. Wanapata vitu haraka lakini wanakufa wakiwa peke yao
Siri ya Balance ni nini?
Sio kufuta darkside. Sio kujifanya malaika 24/7.
Balance = Kujua lini kutumia upande gani
Mfano:
Ukimya = Right side. Lakini wakati mwingine lazima useme "Hapana" = Dark side yenye mipaka.
Kutoa = Right side. Lakini wakati mwingine lazima ujilinde = Dark side yenye hekima.
Watu wenye balance wanaamani ndani. Hawajipingi wenyewe.
---
Carl Jung alisema: "Huwezi kufika nuru bila kwenda ndani ya giza lako kwanza"
Binadamu ni pande mbili kwa wakati mmoja
1. DARK SIDE
Hii ni sehemu ya wivu, hasira, tamaa, ubinafsi, kulipiza kisasi.
Ni ile sauti inayosema "chukua yako kwanza", "watalia wao".
Haitoweki. Iko ndani ya kila mtu.
2. RIGHT SIDE / LIGHT SIDE
Hii ni huruma, upendo, uaminifu, kutoa, kusamehe.
Ni ile sauti inayosema "msaidie", "fanya kilicho sahihi hata kama hakuna anayeona".
Kwa nini wengine wanapotea?
Kama ulivyosema kuna watu 2:
Carl Jung alisema: "Huwezi kufika nuru bila kwenda ndani ya giza lako kwanza"
Ndio wale watu wanaojifanya wema sana kwako ila muhudumu wa bar au restaurant anamfokea ama kumtukana.binafsi kitu kinachoanza kunistua kwamba huenda inawezekana kwa asilimia kubwa mtu niliyekutana nae eidha ana intensions mbaya na mimi ama inaweza isiwe intensions mbaya ila anataka kunitumia kwa hila ( taking advantage ) mapema sana nikiona mtu ananiiga hasa character yangu ama namna ninavyoyatizama mambo umakini unaongezeka juu ya mtu huyo. hiyo huwa ni sign yangu ya awali kabisa.