Chanzo cha Saratani Kanda ya Ziwa ni majitaka yenye Zebaki (Mercury)kutoka migodini siyo maji ya maiti!

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,520
17,426
Binafsi napinga kauli ya makamu wa Rais kuhusu chanzo cha saratani kanda ya ziwa kuwa maji ya maiti yenye chloroform.

Ni heavy metals pekee kama mercury, lead, zinc na nyinginezo ambazo zinaweza kukaa kwa muda mrefu kwenye maji na ardhini hadi kuyeyuka kwenye maji na kudhuru watumiaji wa maji hayo.

Kuhusu formaline na chloroform hizo ni volatile in nature, haziwezi kuishi kwa muda mrefu hewani kwenye joto la kawaida hadi kumfikia mlaji. Yaani huyeyuka kutokana na joto na kuwa gesi hivyo haziwezi kuishi kwenye kiumbe kwa muda mrefu na kusababisha madhara makubwa kiasi hicho.

Kauli ya Makamu ni ya kisiasa wala siyo ya kikemia. Ni kawaida kwa wanasiasa wetu kuleta taharuki kwenye jamii kwa malengo fulani.

Najua kauli hiyo imelenga kuua uchumi wa samaki na kuwabeba wawekezaji wa migodi nchini, kama ile kamati iliyokuja na majibu ya kizembe. Eti kinyesi cha ng'ombe na mkojo ndiyo vilivyosababisha maji ya Mto Mara kuchafuka! Kamati ile na majibu yake ni muendelezo wa siasa chafu kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa dhidi ya wamiliki wa migodi wa kanda ile.

Hatujui kauli ya Makamu wa Rais inaspin kitu gani hasa wakati huu wa maumivu ya Tozo, lakini sisi kama wasomi wa kemia hatuwezi kukubali taaluma yetu kudharaulika kisiasa!
 
Hii yako ni hypothesis tu, usimbishie makamu wa rais, ana access na information nyingi sana za siri na za wazi.
Una undugu na DR UCHWARA? Simuoni jamvini ckuiz.

Pia kwann Makamo wa Rais asihusishe na Dawa za kuhifadhia maiti aseme maji ya maiti kuwahususha waganga wa Jadi wakati hata maji hayo hutolewa na watumishi wa Serikali wakiwauzia waganga na washirikina, wafanya biashara ktk butchers?

Kwann Kanda ya ziwa?

Samaki wanaohifadhiwa ktk majokofu ni wanasafirishwa Nchi nzima, masokoni hawatunzi samaki ktk majokofu.

Samaki wa maji chumvi wafanyabiashara hununua dawa hizo. Why Kanda ya ziwa?

Hii ni hujuma Kwa Uchumi wa Kanda ya ziwa, sijui wanalenga nn!
 
Kumejaaa Viwanda vidogo vinavyotumia kemikali kienyeji tu katika maeneo mengi ya kanda ya Ziwa Serikali wala haijachukua hatua kudhibiti hii hali ni hatari Kansa imekua janga kubwa eneo hilo la nchi.

Itakua balaa zaidi mana hamna anaejali.
 
Binafsi napinga kauli ya makamu wa Rais kuhusu chanzo cha saratani kanda ya ziwa kuwa maji ya maiti yenye chloroform...
Maji ya kuoshea maiti ni hayahaya maji ya kawaida kabisa sanasana na sabuni hizi hizi za,kawaida inapobidi.

Maiti wala haoshwi kwa kutumia pipa zima la maji sasa hizi tuhuma sijui waziri kadanganywa na nani huko halafu naye bila kufanya utafiti kujiridhisha akakimbilia kwenye media

Sent from my LM-V500N using JamiiForums mobile app
 
Binafsi napinga kauli ya makamu wa Rais kuhusu chanzo cha saratani kanda ya ziwa kuwa maji ya maiti yenye chloroform...
Wewe nawe ni mtupu kwenye sekta ya madini. Ni mgodi gani wa mwekezaji unaotumia mercury? Kama hujui, hakuna mgodi hata mmoja wa wawekezaji unaotumia mercury.

Mercury hutumika, tena kwa kiasi kidogosana, na wachimbaji wadogo.
 
Nimefurahi kuona mtaalamu unatoa ufafanuzi, hii ipo kwenye mtandao unaitwa Quora
Huyu hana utaalam wowote. Ni mgodi gani wa mwekezaji, wewe uliwahi kuambiwa unatumia mercury?

Huyu anazungumziae ti hizo chemicals za kuhifadhia maiti ni volatile, kitu asichokijua ni kuwa toxic material inaweza kuwa volatile ikiwa kwenye open air, lakini haiwezi kuwa volatile ndani ya mwili wa mwanadamu.
 
Formalin nimewahi kuisikia kua mbali na kutumika kuhifadhia maiti,huwa inatumika pia kuhifadhia samaki,hivyo mwisho wa siku huleta madhara kwa mtumiaji wa samaki,kwa kumsababishia upofu n.k.
 
Chanzo cha kansa ni heavy metal zinazo toka migodini samaki wana digest na binadam anakula kula samaki zenye heavy metal mwisho wa siku ni kansa mwanzo mwisho niliogopa watu elfu 70 kila mwaka wanatibiwa kansa wanatoka kanda ya ziwa, makamo alipotosha kwakweli
 
Binafsi napinga kauli ya makamu wa Rais kuhusu chanzo cha saratani kanda ya ziwa kuwa maji ya maiti yenye chloroform.

Ni heavy metals pekee kama mercury, lead, zinc na nyinginezo ambazo zinaweza kukaa kwa muda mrefu kwenye maji na ardhini hadi kuyeyuka kwenye maji na kudhuru watumiaji wa maji hayo.

Kuhusu formaline na chloroform hizo ni volatile in nature, haziwezi kuishi kwa muda mrefu hewani kwenye joto la kawaida hadi kumfikia mlaji. Yaani huyeyuka kutokana na joto na kuwa gesi hivyo haziwezi kuishi kwenye kiumbe kwa muda mrefu na kusababisha madhara makubwa kiasi hicho.

Kauli ya Makamu ni ya kisiasa wala siyo ya kikemia. Ni kawaida kwa wanasiasa wetu kuleta taharuki kwenye jamii kwa malengo fulani.

Najua kauli hiyo imelenga kujua uchumi wa samaki na kuwabeba wawekezaji wa migodi nchini, kama ile kamati iliyokuja na majibu ya kizembe. Eti kinyesi cha ng'ombe na mkojo ndiyo vilivyosababisha maji ya Mto Mara kuchafuka! Kamati ile na majibu yake ni muendelezo wa siasa chafu kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa dhidi ya wamiliki wa migodi wa kanda ile.

Hatujui kauli ya Makamu wa Rais inaspin kitu gani hasa wakati huu wa maumivu ya Tozo, lakini sisi kama wasomi wa kemia hatuwezi kukubali taaluma yetu kudharaulika kisiasa!
Nakubaliana na wewe mkuu.

Kama dawa za kuhifadhia maiti ndizo zingelikuwa zinatumika kuhifadhia samaki, nadhani madhara yake yangelikuwa kwa watu wa mbali na kanda ya ziwa ambapo samaki zilizohifadhiwa zinasafirishwa kwenda huko.

Kanda ya ziwa kwa asilimia kubwa wanakula samaki freshi. Kemikali zinazotumika kwenye migodi ndiyo primary source ya kuongezeka kwa saratani kanda ya ziwa, period.
 
Back
Top Bottom