Chanjo ni Lazima: Hoja ya Mbowe ina Mashiko

Chanjo ni Lazima: Hoja ya Mbowe ina Mashiko

Kama ni nia ni majadiliano ya hoja, basi shika kitu kimoja kimoja. Siyo kuruka ruka kama bisi kikaangoni.

Chagua tuanzie ipi?
Ujinga wa chanjo za korona, Unachanjwa halafu bado unakuwa na hifu ya kuambukizwa, Tofauti kabisa na chanjo zingine

Ni upotevu wa fedha za umma kuagiza chanjo hizi
 
Kuna magonjwa sugu ya miaka nenda rudi hayajaenda likizo ya kuua watu, nina babu zangu watano ktk mlela clan wamezaliwa mwaka 1928-1932 hawana habari na mibarakoa na wanapeta hadi Leo tangu ujio wa corona.

Kuna kinasaba kingine muhimu cha kuongezea pale kwenye ugonjwa huu:

"Hiki kirusi kina mahaba zaidi mijini, majiji, na hasa kunako mazingira ya safari na mikusanyiko ya watu."

Hiki si kirusi cha shamba kwa sasa. Japo tukizembea kitafika huko pia.

Bila shaka majibu ya mbio za mwenge na Nandy festival Mwanza umeyasikia. Bila shaka majibu ya miingiliano ya safari kati ya Moshi na Dar pia utakuwa umeyasikia. Huko ndiko nduguye Mbowe (rip) yaliko mfika.

Au kwa vile hawatoi takwimu ndiyo maana hujui wapi hiki kirusi kina tambaa?

Kumbuka kirusi hiki kimekuja kwa ndege.

Waliko wazee wako (mola awajalie maisha marefu) waache huko huko. Kwa kuwaleta mjini, unaweza kulazimika kumlaani mwendazake badala ya kumwacha akapumzika kwa amani.
 
Uganda na Rwanda hapana kuendekeza ujinga. Huko wala si ukuda bali utachezea kichapo!

Kumbuka ujinga si tusi. Ni suala la kutokuelewa tu. Ujinga dawa yake ni elimu dunia tu mkuu.

Huku kwetu tutabembelezana kwanza, ila baadaye kutakuwa na vikwazo hapa na pale. Mdogo mdogo tutafika tu.

Hiyo ndiyo sayansi ya chanjo.
Acha uongo mkuu! Rwanda na Uganda kote huko hakuna anayelazimishwa kuchanja isipokuwa vurnerable groups kama wafanyakazi sekta ya afya.

Hakuna nchi inayolazimisha chanjo, Indonesia ilitaka kulazimisha lakini sijui ilikuwaje hawajafanikisha. Kusema Mbowe anauchungu wa kufiwa na kaka yake na kuuguliwa na mtoto wake basi alazimishe ukoo wake wote na watu wake wa karibu (Ikiwemo wafuasi wake) ndiyo wachanjwe ili asifiwe tena kama anaamini hizo chanzo zinazuia vifo vya Corona. Hawezi kusema nchi nzima ichanjwe kisa kafiwa na kaka yake huo ni uzwazwa.
 
Ujinga wa chanjo za korona, Unachanjwa halafu bado unakuwa na hifu ya kuambukizwa, Tofauti kabisa na chanjo zingine

Ni upotevu wa fedha za umma kuagiza chanjo hizi

Na unathubutu kuuita "ujinga wa chanjo ya Corona" kwa werevu upi mkuu?

😂😂😂😂😂😂😂!

Kwa hali hizi nawaelewa jabisa akina Museveni na bwana Kagame. Wanaume wa shoka hawa.

Kwa hakika maendeleo hayawezi kuwasubiri wakaramojong au wamasai kuvaa suruali.

Kwamba hata ukichanjwa waweza ambukizwa?

IMG_20210718_063653_881.jpg


Ukishachanjwa hata ukiambukizwa tena hali inakuwa na unafuu mkubwa.
 
Kwa hiyo mbowe katumwa na upande wa pili kwa sababu upande wa pili unaona watu hawataki kuchanjwa? Anatumika kama kisemeo tu na upande wa pili. Mbowe ni mtu makini haya hayatoko moyoni bali yanatoka upande wa pili
Boooo! Boooo! Boooo!
 
Kama ukichanjwa huambukizwi, hofu yako ni ipi kwa wasiochanjwa?

Tuandike mara ngapi?

IMG_20210720_094159_438.jpg


Hiyo hofu unaisoma wapi?

Rudini shule. Elimu haina mwisho. Na elimu ni uhuru!
 
Tatizo sio chanjo tatizo ni hao waliotengeneza hiki kirusi kwa makusudi kabisa je wanalengo lipi na wanadamu???

Kama suala ni kifo mbona ni jambo la muda tu na kila mmoja atakionja!!

Ni kweli ugonjwa upo na unaua bahati nzuri ni kwamba kila kitu kimeshawekwa wazi juu ya madhumuni na lengo la hili gonjwa pamoja na chanjo yake

Hivyo kuanza kulazimishana chanjo ni upuuzi na kila mtu aishi maisha yake ilimradi hauvunji sheria na kanuni za nchi

Mkuu hii ni hatua sana kwamba unatambua:

"Ni kweli ugonjwa upo na unaua."


Ila sasa, kwamba?

".. bahati nzuri ni kwamba kila kitu kimeshawekwa wazi juu ya madhumuni na lengo la hili gonjwa pamoja na chanjo yake .."

Hahahaa haa 😂😂!

Nani ameyaweka wazi madhumuni hayo na ni yapi ikiwamo lengo la chanjo yake?

Mwongozo wako tafadhali.

😂😂😂😂😂😂

NB: Nimelazimika kucheka muda wote nikiandika haya kama mazuri vile.

Hiiiiii bagosha!

Hata hivyo nisiache kumalizia:

IMG_20210719_183108_460.jpg
 
Mkuu hii ni hatua sana kwamba unatambua:

"Ni kweli ugonjwa upo na unaua."

Ila sasa, kwamba?

".. bahati nzuri ni kwamba kila kitu kimeshawekwa wazi juu ya madhumuni na lengo la hili gonjwa pamoja na chanjo yake .."

Hahahaa haa 😂😂!

Nani ameyaweka wazi madhumuni hayo na ni yapi ikiwamo lengo la chanjo yake?

Mwongozo wako tafadhali.

😂😂😂😂😂😂

NB: Nimelazimika kucheka muda wote nikiandika haya kama mazuri vile.

Hiiiiii bagosha!

Hata hivyo nisiache kumalizia:

View attachment 1860722
Labda unacheka kwa sababu unajua ila unajitoa ufahamu kwa maana kama wewe ni mtu wa kusoma nakala mbalimbali mtandaoni na nje ya mtandao unafahamu fika kwamba huu ni mchezo wa hatari ambao unachezwa na maisha ya watu ndio dhamana yake kuu

Soma mkuu
 
Labda unacheka kwa sababu unajua ila unajitoa ufahamu kwa maana kama wewe ni mtu wa kusoma nakala mbalimbali mtandaoni na nje ya mtandao unafahamu fika kwamba huu ni mchezo wa hatari ambao unachezwa na maisha ya watu ndio dhamana yake kuu

Soma mkuu

Mkuu, ugonjwa huu upo na unauwa. Ulitokea wapi na kwa nini, hayo yanaweza kuwa muhimu baadaye lakini kwanza tukiwa salama.

Ni busara kumkamata na kumdhibiti ng'ombe asile mazao ya watu, badala ya kuanza kumtafuta kwanza ambaye hakumfunga vyema kamba kwenye mti.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Mkuu, ugonjwa huu upo na unauwa. Ulitokea wapi na kwa nini, hayo yanaweza kuwa muhimu baadaye lakini kwanza tukiwa salama.

Ni busara kumkamata na kumdhibiti ng'ombe asile mazao ya watu, badala ya kuanza kumtafuta kwanza ambaye hakumfunga vyema kamba kwenye mti.

Au nasema uongo ndugu yangu?
Walioutengeneza lengo ni kuua wanadamu wanzao na wanadamu wenyewe hawana hofu ya kufa wameamua liwalo na liwe sasa nani anateseka na maisha ya mwenzake???
 
Nenda kaungane na wakina Joti kuchekesha, Mbowe hawezi kutufanya watu timamu misukule, najua kuna misukule yake kila akibadili Gia angani nayo inabadili
Kama umekaa na shangazi zako hapo kibarazani na kuona nawaletea vichekesho,basi mnatakiwa mpimwe akili.
 
Kama mwuungwana tokea pande za Pwani niliyeukataa ukanjanja katika nyanja zote, nina lazimika kutia neno juu ya maneno ya hekima yake Mwamba Aboubakar Laigwanan Mbowe (Mola amjalie maisha marefu).

Uhalisia kuhusiana na chanjo yoyote ni huu hapa:

"Chanjo ina maana kama tu idadi kubwa na ya kutosha katika jamii inakuwa imeipokea. Vinginevyo inakuwa haina maana."

Kiuhalisia chanjo ni kwa manufaa ya wanayoipokea. Serikali zina wajibu wa kuona watu wake wananufaika chanjo husika.

Kuweza kuwapata idadi kubwa kadri iwezekanavyo mbinu mbali mbali hutumika zikiwamo kutoa elimu, ushawishi na hata kutumia nguvu ikibidi.

Kwa wanaume wa shoka, pande za Rwanda na Uganda, huko hakuna cha lele mama au mswalia mtume. Huko kuchanjwa ni lazima na bakora kumhusu mtu anayeleta ujuaji wala si issue.

Kwingine uthibitisho wa chanjo huhitajika kabla ya kupata huduma kama vile usajili, usafiri, ruhusa nk kama kishawishi. Chanjo inakuwa hiari, lakini ni lazima kabla ya huduma husika.

Kwa jamii zilizostaarabika vilivyo na zenye kujitambua, huko chanjo ni vitu vinavyoeleweka.

Rejelea hali halisi ya kwetu ambapo tokea Apr 2020 hazipo takwimu mpya za Corona. Yaani tokea hapo hakuna mgonjwa wala aliyekufa kwa Corona isipokuwa kaka yake Mbowe.

Katika kipindi hicho pia watu wameaminishwa kuwa huu ugonjwa haupo. Bali Corona ni vita vya kiuchumi na chanjo hizi ni sehemu tu katika kuwaangamiza wao.

Hiiiiii bagosha!

Waliowaaminisha hivyo ni Rais wa nchi akishirikiana na wizara yenye dhamana na afya za watu. Katika walioaminishwa hivyo, wengi wao ni "the ignorant mass" vijijini; wakiwamo sungu sungu, wapiga debe, machinga, vibaka vibaka na wa namna hiyo.

Una ibadili vipi mitizamo ya watu kama hao, huku watu wakiendelea kufa?

Ikumbukwe kuwa hadi sasa serikali yetu haitoi takwimu zozote na hayupo ajuaye hali ni njema au mbaya kiasi gani.

Kwa hakika mwenye kujua faida za chanjo na kuthamimi maisha ya watu hatachelea kutumia nguvu kuwataka watu kuchanjwa ambayo aghalabu ni kwa faida yao.

Ama kwa hakika itakuwa jambo la kushangaza kwa serikali yoyote, kama itakaa kimya iache watu kufa iwapo matumizi ya nguvu tu yangali nusuru maisha dhidi ya ujinga wao.

Viva Museveni na viva Kagame kwa kuyajali maisha ya watu wenu vilivyo kiasi cha kutumia nguvu stahiki inapobidi katika kuwanusuru.

Kwa hakika waja nyie mnayo thwawabu kubwa huko mbinguni, Inshallah!
Kulazimisha mtu kuchoma chanjo Sio lazima mtu ashikwe KWA nguvu, bali ni kuweka taratibu za kumfanya mtu achomwe chanjo,

Kauli ya Mh mbowe ipo sawa, utakichoma chanjo baki wilayani kwako, au mkoani kwako, hatuwezi chukulia Mambo mazito Kama CORONA Kimzaa zaaa
 
Naomba unipe maana halis kwann mtu anachomwa chanjo?...tuanzie hapo...na chanzo maana yake nin...

Mfano mim nishaumwa korona.wadudu walishaingia mwilin mwangu...mwili ukatengeneza kinga ukapambana nikapona...maana yake nina kinga tayar..

Chanjo nijuavyo mim ni kwamba unaingiziwa wadudu mfu ili mwilk wako utambue na kutengeneza kinga dhid ya hao wadudu...

Sasa kwasisi ambao tushaumwa korona tukapona..mnatulazimishaje tudungwe chanjo?

Mkuu sikuwa nimeiona comment yako hii kabla. Bila shaka kutokana na kuwa imekuwa ni siku ndefu yenye uhitaji mkubwa na kuweka kumbukumbu nyingi sawa sawa.

Kujibu maswali yako:

1. Kwa nini mtu anahitaji kuchomwa chanjo?:

-- kwa kawaida mwili una namna kujikinga (antibodies) na viingiavyo mwilini vyenye kuweza kuleta magonjwa (antigens).
-- kila antigen inahitaji antibody yake.
-- mwili unaposhambuliwa na antigen fulani, huugua wakati ukipambana kutengeneza antibody husika.
-- mwili ukisha tengeneza antibody husika sasa unakuwa unaijua antigen hiyo na kuwa uko tayari kwa mpambano.
-- si antibodies zote zinabakia mwilini siku zote.
-- antibodies za Corona kwa mfano hubakia mwilini kwa takribani miezi 5.
-- antibodies za ebola hubakia kwa muda mrefu zaidi ambapo hata ni sahihi kusema mtu akiugua ebola hawezi kuugua tena.

2. Kwa nini mtu anachomwa chanjo?:

-- mtu anachomwa chanjo ili kuufanya mwili kutengeneza antibodies kabla ya hatari.
-- hii huwa si tu kuwa ni wadudu waliodhoofu peke yake.
-- wanaweza kuwa ni wadudu dhoofu yaani walioodhofishwa, au waliokufa, au hata vipande (au kipande chao) yaani inactivated, attenuated, particles au wakiwa wafu.
-- si haba kukubali kuwa beberu yuko mbali na si mwenzetu.
-- hivi vikiingizwa mwilini, mwili huhamasishwa kutambua ujio wa antigen mwenye ufanano nao ili kutengeneza antibody stahiki kumsubiria.
-- antigen huyo akija mwili huwa katika nafasi nzuri zaidi ya kupambana naye ukiwa katika afya njema.

3. Kama ulishaugua Corona kwanini kuchanjwa tena?

-- kama ilivyo elezwa kabla antibody kwa Corona kutokana na ugonjwa zinakaa kwa takribani miezi 5.
-- ikumbukwe hizi zinakuja kukiwemo na kusukwa sukwa na ugonjwa wenyewe, kama vita kamili.
-- haiyumkiniki kuuacha mwili ukiwa pia na irreparable damages.
-- ipo tofauti ya maisha ya antibodies za kutokana na chanjo na za kutokana na maambukizi ya ugonjwa mwilini.
-- tofauti hii ikutokana na sababu mbalimbali zikiwamo technologies, dozi na labda pia ile kuwa mwili unapokea kichocheo ukiwa uko mzima.
-- kumbuka chanjo nyingi zina dozi 2 - 3.
-- antibody ya chanjo ina nafasi ya kuwapo kwa muda zaidi ikiwamo hata vikorombwezo zaidi.

Kulikuwa na uzi huu humu jamvini labda pia ungeupitia kwa kumbukumbu zaidi:

Corona: Tunavyongopeana kwenye hili la tiba na chanjo
 
Kuna watu wanaogopa kuchomwa sindano. Mijoga kweli.😝😝😝😝😝
Kwani si ukachanje wewe ? Ukichanjwa hutaugua wewe sasa pilipili usizozila zakuwashia mini? Anayetaka akachanje usilazimishe mtu kwani kuna ajrnda gani nyuma mpaka iwe lazima!?
 
Kulazimisha mtu kuchoma chanjo Sio lazima mtu ashikwe KWA nguvu, bali ni kuweka taratibu za kumfanya mtu achomwe chanjo,

Kauli ya Mh mbowe ipo sawa, utakichoma chanjo baki wilayani kwako, au mkoani kwako, hatuwezi chukulia Mambo mazito Kama CORONA Kimzaa zaaa

Tuko pamoja mkuu:

IMG_20210719_185857_625.jpg
 
Back
Top Bottom