Changamoto za kupata mtoto mchanga ukiwa umri wa kustaafu, unakuwa ni Baba Babu. Dawa ni kujipanga kabla, vinginevyo ni kubebesha watu mizigo yako

Leo Ijumaa ya Tarehe 8 April, ni siku yangu ya kuzaliwa, nikiwa nimeipiga mingi nikikaribia 60! ambao ndio umri rasmi wa kustaafu, nikiwa tayari ni father of 8 +1= 9, Grand Pa of 6, and about to retire!.

Sababu ya makala hii ya leo sio kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa, bali kutoa mbinu za changamoto za ulezi katika umri mkubwa, huku unajiandaa kustaafu, huku vichanga vinaendelea kuzaliwa!.

Naomba kutoa taarifa ya ujio wa mgeni mwingine kwenye familia yangu, ujio wa mgeni huyu, ume concide na tarehe yangu ya kuzaliwa, mgeni huyu mpya, amebisha hodi hapa duniani leo, tarehe 8 April, 2022 majira ya saa 4:00 asubuhi, katika hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam, na kwa vile mgeni mwenyewe ni Jnr kidume, hivyo nimetoa jina langu la Pasco, hivyo ataitwa Pasco Mayalla -Jnr na kuanzia leo mimi nimebadili jina na kuwa Pasco Mayalla Snr baada ya ujio wa Pasco Jnr!.

Kupata mtoto katika umri mkubwa kama huu, kuna changamoto zake, changamoto ya kwanza, ni watoto wangu wakubwa 3, tayari wana watoto!, yaani mimi ni Babu, halafu unapata mtoto mdogo kuliko mjukuu!, hivyo kwa wajukuu wa watoto wangu wa kiume, huyu Pasco Jnr ni baba yao mdogo! na wajukuu wa mabinti huyu ni mjomba wao!, baba mdogo na mjomba kuwa ni mdogo kuliko wajukuu, haipendezei saana kivile!.

Kuna watu wataona ni ajabu kwa mtu over 50 kupata mtoto, japo nikweli sio kawaida sana, watu wanapaswa kujenga familia wakiwa wangali vijana, while still energetic, ukifika umri wa miaka 50 ni umri wa kujiandaa kustaafu na kuitwa babu, sio tena umri wa kuanza kulea vichanga na kuitwaa baba wakati umri ni wa babu!, lakini amini usiamini, kupata mtoto at 50 plus Kiafrika, ni kawaida sana!, tuna mfano mingi tuu, ukitafuta umri wa Chief Burito Nyerere wakati Julius Kambarage anazaliwa, hutashangaa!. Hata Nabii Ibrahim alipomzaa Isaka alikuwa na umri wa miaka 90!. Mfano mzuri wa karibu ni yule Mzee wetu fulani, Al maarufu na mashuhuri, alipata watoto twins at 74 years!, hivyo mimi kupata mtoto at 50 plus, ni bado kijana sana!, ila huyu Pasco Jnr ni last born!.

Lengo la makala hii ya leo ni kutoa somo la kujiandaa kustaafu, ili ustaafu bila stress. Kitendo tuu cha mstaafu mtarajiwa kupata mtoto at 50 +, hiyo peke yake tayari ni stress tosha!, kwasababu mtoto anatakiwa kutimiza the age of majority, akiwa total dependant!. Pesa za mstaafu, haziwezi kumlipia shule nzuri mtoto huyu, unless nikubali akasome St. Kayumba!. Kama hao wenzake 8, hakuna aliyesoma St. Kayumba, hivyo huyu kitinda mimba wa Baba Babu, kuja kusoma St. Kayumba, itakuwa sio kumtendea haki, hivyo I need kujipanga kweli kweli!. Hivyo makala hii, itakuwa ni msaada mkubwa sana kwa wazee wenzangu na wale wote wenye umri mkubwa, huku wakikabiliwa na changamoto za ulezi.

Kutokana na maandalizi duni ya kustaafu, wastaafu wengi hujikuta hawana vitega uchumi vya kutosha kuwa sustain baada ya kustaafu, hivyo kuishi maisha ya stress, wengine kusumbua watoto kwa kupiga muzinga, hali inayopelekea ikiona tuu simu ya dingi, unahisi ni mzinga, hivyo ukijiona uko apeche alolo, unaogopa hata kupokea simu ya dingi wako ukidhani ni mzinga!, kumbe sometimes, simu nyingine za madingi, wala sio mizinga!, ni dingi tuu amekukumbuka na anakupigia ili kukusalimia tuu!, hivyo natoa kwa wote, ukiona simu ya dingi, pokea tuu!, ila madingi nao sometimes wanazi!, anakupigia simu, uko very busy, hupokei!, ukiona anafululiza kupiga, unapokea ukijua, anashida!,
"haloo, shikamoo baba".
"marahaba mwanangu, nilikupigia kukusalimia tuu, nina kiu!"
unatamani kukata!.
Wa Maza hawanaga simu za hivi, maza akikupigia simu anashida ujue ni shida kweli!.

Kitu kinacholeta stress kubwa Kwa wastaafu wengi, ni wengi kutofanya biashara yoyote wakati wa utumishi wao, halafu akiisha staafu yale malipo ya mafao ya pensheni ya mkupuo kuyatumia kama mtaji wa kuanzisha biashara, biashara isipokwenda vizuri, matokeo yake ni kupata stress, kuchoka mapema na kuchakaa, na hapo hapo maradhi ya depression na mwisho ni kufa mapema kwa ma pressure, heart attacks, maumivu ya viungo, organ failure etc.

Ili kuzuia stress za kustaafu, kama unapanga kufanya biashara fulani baada ya kustaafu, start small!, anza kidogo kidogo ukingali kazini kupata uzoefu wa kutosha ukiona unaweza ndipo ukistaafu ujikite zaidi.

Ushauri wangu wa the best way ya kustaafu, ni zile fedha za mafao yako ya kustaafu ambayo umelipwa kupitia benki, wastaafu wengi huziweka fedha hizo Benki kama akiba, na kuzitumia kidogo kidogo.

Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu sana. Fedha hizo zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni kwa kuwekeza kwenye ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 12%!.

Sasa tupige hesabu ya pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 12. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 6 kila miezi 6.

Ukiisha nunua bonds zile Bondi certificate ni dhamana ya uhakika ya kupata mkopo Benki yoyote kufanyia biashara yoyote.

Nakushauri, fanya utaratibu na Benki yako, badala ya kusubiri kupokea gawio lako la milioni 12 kwa mwaka, unaomba ulipwe shilingi milioni 1,000,000 kila mwezi kwa muda wa miaka 25, bado wewe mstaafu utakuwa na stress au kusumbua kupiga mizinga watoto?.

Wastaafu wenzangu watarajiwa, ni muhimu sana kupanga uzazi, ni muhimu kupanga familia, ni muhimu kujipanga kustaafu bila stress, ila ikitokea umepata ugeni kama wa Pascal Mayalla Jnr, mida ya machweo, mpokee tuu mgeni with positivism after all kila mtoto anakuja na rizki yake!,
Karibu Pascal Mayalla Jnr.
Happy Born Day Pascal Mayalla Jnr
Happy Birthday Pascal Mayalla Snr
Paskali
Update ya Kilichopelekea Kuendelea Kutengeneza Watoto Post 50 Years!.

Mkuu Goldschmidt , kwanza asante sana kwa kuwa mkweli, bonafide genuine, watu huwa hatupendi kuambiwa ukweli mchungu, hiki ulichosema hapa ni ukweli mchungu!.

It's true watoto 8, now 9 ni wengi!. Mimi ni a modern man, niliao a classmate sweetheart mimi nikiwa at 25 years mwenzagu at 21, straight chuo TSJ, into kujenga familia!, tukahama nchi kwenda UK tukapata mtoto wa kwanza a girl then tukahamia US tukapata mtoto wa pili, a boy tukaamua that is it. Hatuhihitaji tena kuongeza watoto!.

Wife akapata full sponsored fellowship ya 4 years US mimi ndio niwe house husband na babysitter wa watoto wetu wawili. Very unfortunately, nilishindwa nikamwacha wife US na kurudi Bongo!.

Long distance relationships doesn't work well kwa baadhi ya makabila, so does maisha ya u Marioo, yaani mke ndio mwenye kazi, pesa, mimi niwe Marioo!. Wasukuma ni one of such tribes!, nilishindwa!.

Hivyo niliporudi kuishi bongo huku wife US, nikajikuta wametokelezea watoto 3 wengine!. 2 boys and a girl hivyo I had 5 kids!. (naomba usiulize ufafanuzi wowote kuhusu hawa watoto 3 please!).

Wife baada ya kumaliza shule with news ya uwepo wa watoto wengine wa3, wife akaamua kugomea US hivyo mimi nikawa sina jinsi bali kurudi Bongo na kuendelea kuendesha life.

Mwaka 2008 I suffered a bad terrible motor accident, I was confirmed to a wheelchair!. Hapa akajitokeza kabinti fulani with a heart of gold, she came with love and care , kiukweli mtu ukiwa invalid confined to a wheelchair, akatokea mtu kupenda hivyo ulivyo, ni very rare and amazing love.

She told me something was telling her tukijaribu pengine, nitaweza kupona. She made some efforts tukahangaika huku na kule, tukaenda South gharama zikatushinda , tukaenda India, ndiko nilikoponea na kusimama tena!.

Baada ya kupona na kurudi Bongo,
kwanza nilitoa shukrani kwa yote niliyopitia Waraka wa Pascal Mayalla - Asanteni Sana! nikajikuta zawadi pekee kwa huyu binti ni ndoa!, hivyo 2010 nikaoa tena, by then nikiwa over 40!.

Kabinti kakanizalia 3 beautiful daughters the number was 8, ilipotokea tena dalili ya ugeni, we didn't say no!, then ndio hiyo jana kaleta kidume, na kiukweli hapo sasa ndio mwisho.
P
Hii makala tamu sana
 
Asante sana ndugu yangu Rashidi Jololo , hili ni swali zuri sana na la msingi sana!.
Siku zote ndoa inapovunjika, sio wanandoa wote hukubaliana amicably, sometimes kuna bitterness na hostilities, ikitokea mama kuachiwa watoto na baba ku abandons and neglects total child support, usually women becomes very bitter, na humwaga sumu kwa watoto kumhusu baba yao!.

Ndio muhimu sana nawasisitiza vijana, ukimpenda msichana, ukadhamiria kumuoa, it's very good to be friends kwanza, before you are lovers!, go steady.

Hivyo mkiwa friends before your are lovers, ikija ku happen that you can't be lovers anymore, you can still be friends!, hivyo mama hawezi kumwaga sumu kwa watoto against baba yao!.

Mimi we are still friends and sometimes not often, we talk about kids!.
P
Hayat mtu mnene hakufanya urafiki kwanza, alioa akazaa, ndoa ikaisha. Akaacha watoto, mama akabikamu bita na kujaza sumu mbaya sana kwa watoto. Hata alipotaka amani na watoto, wakakimbilia kwa dada kimbaumbau na kuharibu sana mtandaoni, anyway case closed.
 
No ,mi huwa nabisha sn , inategemea na mtu,watu hawafanani... mama angu (nurse) alizaa akiwa na zaidi ya 40 na wote tuko vzr Tena tulikuwa tuna akili balaa class...dada angu wa ba mkubwa,amezaa akiwa na 43 na ana mimba nyingine Tena very healthy na watt hawana shida
Rfk ake dada angu nae ana 45 + amezaa na mtt Yuko vzr Hana shida yyt mkubwa kabisa.
Labda hayo mambo yako huko mjini
Huku bush wanawake mpk 50 wapo wanao breed kabisa
Huyo ni exceptional kama Sara wa kwenye Biblia aliyezaa mtoto wake wa kwanza Isaka mwenye akili nyingi akiwa na umri wa miaka 90

Sio kitu cha kawaida lakini kuna exceptionally kwa wachache sana kwenye dunia

Kuzaa at 40 years sipendekezi ni Risk zone for many women
 
Kwa mwanaume Miaka 60 aweza zaa mtoto strong tu

Ila kwa mwanamke mwisho Miaka 40 zaidi ya hapo kuzaa anatafuta matatizo aweza zaa mtoto zezeta au lenye akili nusu.Jinga hasa.
Wanawake pia hukauka mapema hivyo ni vyama kwa mwanamke kuwahi kuzaa mapema ukifika 40 ndio uzae last born vinginevyo utagombana na manesi na waweza zaa kwa operation

Anyway Mayala Mkeo ana umri gani? Kama beyond Miaka 40 be prepared. For the worse
Kuna Mwanamke ana 35 juzi ameenda clinic coz anakaribia kujifungua...Daktari wa Wanawake akamshauri asichelewe kuzaa watoto wengine kwsbb misuli ya uzazi imeshakomaa

Alikuwa disappointed sana siku nzima, nilimwonea huruma

Sasa akifika 40 sijui kama itawezekana tena
 
No ,mi huwa nabisha sn , inategemea na mtu,watu hawafanani... mama angu (nurse) alizaa akiwa na zaidi ya 40 na wote tuko vzr Tena tulikuwa tuna akili balaa class...dada angu wa ba mkubwa,amezaa akiwa na 43 na ana mimba nyingine Tena very healthy na watt hawana shida
Rfk ake dada angu nae ana 45 + amezaa na mtt Yuko vzr Hana shida yyt mkubwa kabisa.
Labda hayo mambo yako huko mjini
Huku bush wanawake mpk 50 wapo wanao breed kabisa
Kuna mother ana age 54 ana breed,dah yani sijahamini kabisa
 
Kuna mother ana age 54 ana breed,dah yani sijahamini kabisa
Hahaa
Ndio wapo mama angu aliniambia vijijini wako wengi tu umri huo wanao breed.
I think na vyakula pia vinachagia.
Hivi Kuna mdada Marekani at 51 amezaa,mpk NBC walitangaza.
Sa huyo akifika 90 mtt ana 30 si ana familia yake hapo,😅Tena wanamtumza mama Yao vzr.
 
Kuna Mwanamke ana 35 juzi ameenda clinic coz anakaribia kujifungua...Daktari wa Wanawake akamshauri asichelewe kuzaa watoto wengine kwsbb misuli ya uzazi imeshakomaa

Alikuwa disappointed sana siku nzima, nilimwonea huruma

Sasa akifika 40 sijui kama itawezekana tena
Hana Imani
Mi jmn Dr sio msemaji wa mwisho,ila Mungu. hospital naenda, nasikiliza na kufuata
Baadhi ya ushauri lkn siachi kumuomba Mungu!
 
Huyo ni exceptional kama Sara wa kwenye Biblia aliyezaa mtoto wake wa kwanza Isaka mwenye akili nyingi akiwa na umri wa miaka 90

Sio kitu cha kawaida lakini kuna exceptionally kwa wachache sana kwenye dunia

Kuzaa at 40 years sipendekezi ni Risk zone for many women
Wala sshv watu wanazaa tu mbona
Cha mhimu,afya iwe vzr nenda hospital,sikiliza na fuata ushauri wa dr
 
Back
Top Bottom