Naomba msaada nahitaji kufanya edit ya profile kwenye ajira portal lkn nashindwa kufuta. Eg. O level imeandika mara 2 nahitaji kufuta moja sion option. Akhsante
 
Upo sahihi sana mkuu hata mimi nimeshindwa leo kufanya application kwa sababu hiyo na wakati wameandika equvailent

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa jamaa wanazingua kinyama mimi mwenyewe toka nimejiregister nimefanikiwa ku apply mara 2 tu,baada ya hapa kila niki apply "job application failed"ndo message nayipata mpaka nimechoka.
 
Kumbe wana ofisi UDOM,ipo sehemu gani aisee hata mi portal yangu mizinguo weli kila nikiapply job inafeli na requirement nikiangalia ziko sawa.
Ukiwa Sabasaba unapanda magari yanayoenda Social /bondeni, ukifika mwisho wa gari unatembea kunyoosha na hy barabara then mkono wa kushoto utaona nyumba ya kawaida hapo ndio ofisi zao zinaitwa Asha rose Migiro, ukienda naomba unichek mana mm pia nna shida nao afu niko mbali na Dodoma
 
Ukiwa Sabasaba unapanda magari yanayoenda Social /bondeni, ukifika mwisho wa gari unatembea kunyoosha na hy barabara then mkono wa kushoto utaona nyumba ya kawaida hapo ndio ofisi zao zinaitwa Asha rose Migiro, ukienda naomba unichek mana mm pia nna shida nao afu niko mbali na Dodoma
Nitakurudishia mrejesho.
 
Nimeshindwa kuomba kazi ajira portal yan nikijaribu inakataa sujui nakosea wapi katika kujaza......nukuu ya mtu wa karibu
 
=Baada ya kuapply kazi husika. utasubiri kwa muda fulani , kupitia web ya utumishi watatoa majina ya wahusika waliochaguliwa kwenda kufanya interview( utaelekezwa mahali,siku na saa).
=utakwenda kufanya interview , utakaa tena kwa muda kusubiri. Kama utabahatika kufaulu interview, utapewa siku kadhaa za kujiandaa kwenda kuchukua barua ya kazi ambayo inaeleza ofisi, taasisi n.k unayotakiwa kuripoti kama kituo chako cha kazi. hiyo barua utakwenda kuchukua huko huko utumishi.
=baada ya hapo . huko kituo ulichapangiwa watamaliza taratibu zako zote za ajira kama mikataba ya kazi na kadhalika.

Sent using Jamii Forums mobile app

Samahani naomba kujua kama umesomea ualimu unaweza pia kujiunga ajira portal??
 
Samahani naomba kujua kama umesomea ualimu unaweza pia kujiunga ajira portal??
Binafsi sijawahi kuona utumishi wakitangaza kazi za Ualimu.. hizo naona zinahusika huko Tamisemi(sijui wanaitaga OTEAS.. acha kusumbuka na Ajira portal walimu wenzio washaanza kuomba kazi huko Tamisemi.
 
Wakuu profile yangu kabla sijaweka pasport size ilikuwa inasoma 95%. Hivi sasa tayari nimeweka passport size na imekubali ila cha ajabu bado asilimia hazijaongezeka.

Naomba kwa anayejua anisaide nifanyeje ili asilimia zisome 100% wakuu. Asanteni.
 
Back
Top Bottom