Chama Cha Wananchi CUF Kufutiliwa mbali

Chama Cha Wananchi CUF Kufutiliwa mbali

Kwanza nakupongeza kwa kuwa mjinga namba 3 ukifuatiwa na jecha no 1 na shein 2 ,pili ujinga wako peleka kwa mkeo, tatu kile chama cha waislam kule misri kipo au hakipo, kama cjasahau ntakujibia coz ww hujui ,nikwamba kimefutwa lkn ni bora kisingefutwa misri kungekuwa na amani na mwisho nakuambia ndio unayotuzuiya magaidi wa Tanzania kwa hyo bila Cuf amani hakuna Tanzania nasema Tanzania cjasema Zanzibar nadhani umenielewa
 
Mkuu Pasco mbali na kutoa tahadhari ya yaliyopangwa kuhusu mustakabali wa CUF, toa mwanga pia jinsi unavyouona mustakabali wa demokrasia nchini. Umenukuu vifungu vya sheria kwenye hoja yako.

Unaamini kweli sheria inatumika inavyostahili nchini? Yaani nchi hii inaweza kujidai kwamba inaendesha utawala unaozingatia sheria na haki? Kama sivyo, badala ya kuwa "msoma matangazo ya vifo" kwa wapinzani, toa pia mawazo nini kifanyike kurejesha demokrasia ya kweli, haki na utawala wa sheria nchini?
 
Visiwa vya Zanzibar na Pemba ndio kitu gani?, hata wewe hujui kwamba neno Zanzibar ni Unguja,Pemba na visiwa vingine vidogo vidogo katika Jamhuri ya Zanzibar.

Pia,ni kosa kubwa sana kujiona unajua kila kitu.Kasome maandiko ya God utaona kilichomtokea Musa/Moses.
 
Yaaani huyu Pasco wa Jamii Forum ni miongoni mwa wapumbavu,wanafki na wachumia tumbo niliowahi kutana nao,takataka
 
Cuf walifanya kosa sana kujiunga na chagadema hili kosa wallahi awatalisahau na wanajutia kwann walikurupuka. Wenyewe walipanga hivi CUF wachukuwe visiwani CDM wachukuwe bara then muungano wavunje. Lakini kwa uwezo wa mungu wameshindwa .na tunaomba mungu washindwe
 
Makala nzuri, tena sana. Hayo ni matakwa ya sheria na umeyaeleza vema na bayana. Shaka yangu lakini iko kwenye kutojiamini kwako. Kwanini ujifiche kwenye kivuli cha hofu ilhali unaeleza ukweli. Sawa na umekitia kitumbua mchanga (Naona, hata ivyo, huo umekuwa ni utaratibu hapa). Mada basi hainogi kisa wababe wa kivita, shutuma na maandamo watazikunja nyuso zao. La, hapana. Hilo likome.
 
Hivi katika nchi inayoendeshwa katika demokrasia ya kweli, kati ya CCM na CUF ni chama kipi hasa ambacho msajili wa vyama vya siasa alipaswa kukifuta?

Hebu tikukumbushe kidogo Pasco msingi mkuu wa multipartism ambao ni kuwa kuna KUSHINDA na KUSHINDWA.

Uchaguzi mkuu ulishafanyika tarehe 25/10/2015 huko Zanzibar na kushuhudiwa na waangalizi wa ndani na nje ya nchi walitoa taarifa zao kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na haki.

Jecha alitoa matangazo ya matokeo hsyo kwa siku 2 mfululizo.

Wadimamizi wa uchaguzi walishatoa hadi vyeti vya ushindi kwa washindi wa nafasi za uwakilishi.

Kwa mshangao wa dunia nzima tarehe 28/10/2015 Jecha akaibukia ZBC na kutangaza kufuta matokeo yote kwa kuamrishwa' na watawala kwa kutekeleza ile slogan yao kuwa Zanzibar kamwe haitokuja kutolewa kwa vijikaratasi vya kupigia kura!

Hivi katika mazingira kama hayo Pasco unaditiki kuongea toka ndani ya moyo wako kuwa CUF ndiyo kinapaswa kufutwa katika orodha ya vyama vya siasa badala ya CCM?!

Ama kweli Pasco unatekeleza kwa vitendo ule msemo unaosema kuwa mtumikie kafiri upate 'mlo' wako........

Lakini Pasco unapaswa pia kujikumbusha historia kuwa hata mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 yalisababishwa na waandishi wa habari 'uchwara' wa dizaini kama yako.
 
Hicho kifungu ulichokitaja kwamba kinaweza kutumika kufutwa kwa chama cha siasa huoni kwamba moja kwa moja kinahusu ccm? Wamefanya na wanaendelea kufanya hayo yote ulioyaorodhesha, mbona hutabiri kufungiwa? Badala yake unatabiri victims wa ccm kufungiwa? ATumieni akili zenu vizuri.
 
Wanabodi,

"Chama Cha Wananchi CUF, Kufutiliwa Mbali!... Iwapo Itathibitika Kinahusika/ Kitahusika na Vurugu, Ugaidi, Uvunjifu wa Amani Zanzibar na TZ!.

Nyingi ya theads humu ni threads kuhusu matukio yaliyotokea, lakini tuna threads chache sana kuhusu mambo yatakayokuja kutokea, hivyo hii ni thread ya mambo yatakakuja kutokea kutokana na kitu kinachoitwa "trend readings" na sio utabiri kama wa Sheikh Yahya (RIP) au Nostra Damas.

Trend ni inahusiana na usomaji wa historia ya kilichowahi kutokea nyuma, kulinganisha na kinachotokea sasa, ili kujua kitakachokuja kutokea huko tuendako.

Kichwa cha habai kimejieleza wazi kuwa Chama cha Wananchi CUF, kitafutwa rasmi (toka kwenye daftari la Msajili wa Vyama vya Siasa), kama itathibitishwa pasipo shaka,without any reasonable doubt, kuwa kinahusika, au kitahusika na matukio yoyote ta kihalifu, ya kigaidi au ya uvunjifu wa amani, Zanzibar, Pemba au eneo lolote la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa sababu kitakuwa kimepoteza sifa za kuitwa chama cha siasa kwa mujibu wa sheria ya Vyama vya Siasa ya Mwaka 1992! ambayo kisheria inajulikana kama The Political Partie Act of 1992 au Chapter 258.

Sheria hiyo imeweka sifa mbalimbali za chama cha siasa kinachoweza kusajiliwa, lakini pia imeweka sifa mbali za chama cha siasa ambacho hakiwezi kusajili, na miongoni mwa sifa ambazo chama cha siasa hakiwezi kusajiliwa, ni pamoja na kipengele hiki kwenye ibara ya 8, 2-c
"it accepts or advocates the use of force or violence as a means attaining its political objectives"

Ibara hii inamaanisha kama chama kiliishasajili, lakini baadae kikagundulika kina kiuka kipengele hicho, kinakuwa kimepoteza sifa hivyo kinastahili kufutwa kutoka kwenye daftarri la msajili.

Viongozi, wanachama, wafuasi, wapenzi na mashabiki wa CUF, msije kunirikia kuwa nawawangia au kuwachuria chama chenu kifutwe, bali nawapa tuu angalizo la matakwa ya kisheria, ikiwa na endapo itathibitishwa pasi shaka, "beyond reasonable doubts" kuwa CUF kama chama, kinahusika na kupanga, kuratibu na kutekeleza vitendo vyovyote vya kihalifu, vya kigaidi na vya kuvuruga amani na utulivu wa visiwa vya Zanzibar na Pemba ambazo ni sehemu za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hii ni kufuatia CUF kususia kushiriki uchaguzi wa marudio, hivyo kimesusia na kupanga vurigu, uhalifu na ugaidi ili uchaguzi usifanyike, kama huo ndio mpango wenu, endeleeni na mipango hiyo, lakini huku mkijiandaa kufutwa rasmi!.

Ili ikikutikana wanaofanya vitendo hivyo ni wana CUF individually bila uhusika au uatibu wowote wa CUF kama chama, CUF kama chama, kitabaki salama, na hao wanachama, watashughulikiwa kama wahalifu wengine wowote kwa sababu uhalifu ni uhalifu tuu, hauna chama, hauna dini, hauna kabila, hauna rangi wala jinsia, uhalifu ni uhalifu tuu, na wahalifu wote ni watu wa kulaaniwa na sheria ichuke mkondo wake dhidi yao!.

Sheria zipo lakini hazitekelezwi, ila kufuatia JK kuwa dhaifu, na serikali yake kuwa dhaifu, kuliwapa wahalifu mawanda ya kutamba hadi kumchea simba sharubu na hakufanya lolote, hizi nyakati sasa zimebadilika, nyie mliozoea kuchezea sharubu za simba dhaifu, msijaribu kuchezea sharubu za huyu aliyepo, huyu sii yule mtu wa kucheka cheka na ngedee na kuyavuna mabua!, sasa nyakati zimebadilika, hili ni angalizo tuu nawapa, mlipokee au mlipuuzie, yakitokea ya kutokea, msilalamike kuwa hamkuambiwa!.

Naombeni msije kunisdhutumu kuwa ninachuki na CUF, maneno kama haya ninayowaeleza leo, pia niliwahi kuwaeleza wenzenu na washiika wenu Chadema, na pia niliwahi kuyatoa kwa chama dola CCM!.

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Kufutwa Kwa Mujibu wa ...
Tuhuma Hii: CHADEMA Kuendeshwa Kwa Katiba "Fake" Ikithibitishwa ...

Chonde Chonde Rais Kikwete: Msimamo wa CCM wa Serikali Mbili ndio ...
Tahadhari ya hatari: CCM Imepania Kufanya Kinyume cha Maumbile ...

Wasalaam.

Pasco wa jf!.


WEWE UJIITAYE PASCO, HATA KUFIKILIA HUWEZI. UNADHANI CUF IKIFUTWA NI UBINGWA, YAWEZA KUPELEKEA TANZANIA KUTOTAWALIKA TENA. HIVI YATOKEAYO UTURUKI SUICIDE BOMB KILA LEO, NCHI ILIYO JIONA INAENDELEA NA KUFIKIA VIWANGO VYA MAGHARIBI NA POLISI WALO FUNZWA WAKAFUNZIKA NANI ALITARAJI?!

BE VERY CREFULL WITH YOUR WORLD WEWE NDIO UNASTAHILI KUFUTWA KWA UCHONGANISHAJI WAKO. HAKUNA MWENYE HAKI ZAIDI NCHI HII AWE CCM, AWE, CUF AU CHADEMA HATA ACT NK WOTE NCHI YETU NA TUNA HAKI SAWA.
 
(pasco)
(Chabruma.)
(makonda.)
hizi ID ukifuatiria maneno ya ndani ni yanafanana yaani mtu anatuma thread kisha anajijibu alafu anajikoment kuangalia upepo.


swissme
 
Back
Top Bottom