CHADEMA wanaingilia Ngome ya CUF - Mtatiro

CHADEMA wanaingilia Ngome ya CUF - Mtatiro

Badala ya kuungana wanahasimiana.Ndipo pale CCM inaposhinda kwa kutumia Divide and Rule policy.
 
Unarudi lini Tanzania kutoka ughaibuni? Fuatilia basi hata matokeo ya uchaguzi yakitangazwa japo kwa kupitia JF!

Mkuu taja jimbo moja Tanzania bara linalo shikiliwa na mbunge kutoka CUF. Taja jimbo kisha na mbunge wake. Ukiweza kufanya hivi mimi nitaomba radhi kwa post yangu.
 
Kwa hiyo mbunge wa Temeke katoka CUF? Au tusemeje?

Hawa nadhani wanafananisha "fanatic supporters" na kuwa na support sehemu. Wafuasi wako kuwa na kelele sehemu fulani haimaanishi hiyo ni ngome yenu kama hao wafuasi wakati wa uchaguzi hawa equate nyie kushinda uchaguzi hapo.
 
Kwahiyo unataka kutuambia kwamba cuf inafanya mambo yake kwa kufuata maelekezo ya Mbowe ama ulitaka kusemaje?
Kwenye hayo majadiliano ninyi cuf mlikuwa mmeazimisha vichwa vyenu hata msiju zuri ni lipi na baya ni lipi? Subirini kesho muione nguvu ya umma. Endeleeni na fungate yenu na magamba muda si mrefu mtakuja kutulilia.

cuf ni chama kinachokosoa serikali na kisha kuonesha njia,kina hazina ya wataalam waliobobea katika uchumi wa kimataifa.mbowe hana taaluma yoyot
 
CUF hiki chama kina gubu sana..kama mwanamke wa kizaramo!
Hujakosea Mkuu! Hata hivyo CUF,ni Waswahili kwa Jinsi Chama chao kinavyo jiendesha.Wawakilishi wao wengi ni Waswahili wa Pwani!

Mtatiro yawezekana haijitambui na kama anajitambua ni kuwa kiasi kidogo mno!

Alisahau kwamba wao walizinduwa Operation yao mwaka jana Viwanja vya Jangwani kwa maelekezo ya Mume wao CCM, na wakapangiwa kwenda Arusha, kufanya Mkutano!
Anataka kutuambia hakujua kuwa Arusha ni Ngome ya CDM,???

Kama wao CUF walisomba watu wa Zanzibar na Dar es salaam,kuja kuujaza Mkutano wao wa Arusha, lakini bado Arusha imebaki kuwa ni Ngome ya CDM! Anaonaje na CDM nao wakienda kwenye hiyo anayoita Ngome yao??

Au kunya ni Akinya KUKU!! Akinya BATA ni Kuharaa?????????

MUNGU IBARIKI TANZANIA!!!!
MUNGU IBARIKI CHADEMA!!!!
 
alafu ccm B walikuwa idle sana kwenye saga la masrahi ya wananchi
 
Kapiga marufuku maandamano lakini karuhusu mkutano.

Ahaa huyu naye ni tatizo sana nchi hii unaweza kushangaa kwenye taarifa ya habari ya saa tano usiku anaibuka kupiga marufuku na mkutano pia. Nadhani katiba mpya lazima vyeo kama hiki watu waombe na wafanyiwe interview kama wakenye wanavyofanya. Halafu lazima waundiwe na mamlaka ya kuthibiti utendaji wao maana mahusiano yake na wananchi ni mabaya kuliko mfano wowote!
 
cuf ni chama kinachokosoa serikali na kisha kuonesha njia,kina hazina ya wataalam waliobobea katika uchumi wa kimataifa.mbowe hana taaluma yoyot

Sasa kama cuf kina hazina ya wataalamu waliobobea katika uchumi wa kimataifa na mumo serikalini kwa kushirikiana na mwandani wenu ccm mbona bado nchi yetu iko hoi bin taaban kiuchumi na kijamii?

Na kama kweli cuf ina wataalamu waliobobea, walishindwa nini kutumia taaluma zao na ubobezi wao katika majadiliano hadi Mbowe akawazidi nguvu? Huo usomi wao na ubobezi wao hauna tija yoyote kwa chama chenu.
 
tatizo la chadema hawaheshim taaluma za watu,ndio maana aki na zzzk na arfi wanapigwa vita,kwa chadema ni kuhakikisha uongozi wa nchi unageuzwa kuwa parokia,waislam walielewa hili na ndio mana wako tayari nchi isitawalike kwa lengo la kulinda mtaguso wa vatikan,waislam naamini wataiwajibisha uchaguzi ujao siri imesha fichuka.watu wanayo barua ya mbowe kwenda kwa adrinali pengo.imesmbazwa miskiti yote tanzania.
 
tatizo la chadema hawaheshim taaluma za watu,ndio maana aki na zzzk na arfi wanapigwa vita,kwa chadema ni kuhakikisha uongozi wa nchi unageuzwa kuwa parokia,waislam walielewa hili na ndio mana wako tayari nchi isitawalike kwa lengo la kulinda mtaguso wa vatikan,waislam naamini wataiwajibisha uchaguzi ujao siri imesha fichuka.watu wanayo barua ya mbowe kwenda kwa adrinali pengo.imesmbazwa miskiti yote tanzania.

Mhh ndugu..ushaanza UDINI kwenye maslahi ya wananchi sio tabia nzuri kila jambo unaingiza udini..kwa nini wewe mdini hivii?? Udini tanzania umeingiliwa kinyume.
 
Hawa nadhani wanafananisha "fanatic supporters" na kuwa na support sehemu. Wafuasi wako kuwa na kelele sehemu fulani haimaanishi hiyo ni ngome yenu kama hao wafuasi wakati wa uchaguzi hawa equate nyie kushinda uchaguzi hapo.

Sasa ni nani mwenye "fanatic supporters"'kati ya CUF na CHADEMA kwa makelele na fujo? Kwa umati tuliokuwa tukiuona kwenye TV kabla ya uchaguzi 2010, DR asingepata kura milioni 2! Ajaban!
 
sijawahi kusikia slaa akisema atafaya nini akiingia madarakani zaidi ya kuwashawishi watu waichukie serikali,msomi hapaswi kuongeza tatizo linaloikabili jamii badala yake anapaswa kutatua matatizo na kuonesha njia,lkn babu kizee huyu amekua akihamasisha vurugu na kuwataka wananchi kuwakataa hata ndugu zao waliopi ccm wakati yeye ni mwanachama mzuri wa ccm.kweli ccm inambinu nyingi ikiweo hii ya kuwapandikiza mamluki ktk vyama kama walivyo muweka slaa cdm.hata taaluma ya slaa ya theology niya kanisani.
 
Katika hali ya kushangaza Naibu Katibu Mkuu wa CUF Julius Mtatiro amesema CHADEMA kufanya maandamano na Mkutano Temeke Mwisho ni kuingilia ngome yao.

Akizungumzia mwaliko wa CHADEMA kuitaka CUF kushiriki mapokezi ya wabunge wa upinzani kesho na hatimaye kushiriki mkutano wa pamoja Mtatiro amesema kamwe CUF haiwezi kushirikiana na CHADEMA.

Mtatiro amesema mwaliko wa CHADEMA ni wa kisanii na wamegundua Temeke ni ngome kuu ya CUF kwa hiyo CHADEMA haiwezi kupata watu mkutanoni bila kuishirikisha CUF.Mtatiro ameuliza tangu lini Chadema imegundua CUF siyo CCM B? Mtatiro amelalamika CHADEMA inatafuta umaarufu Temeke kupitia mgongo wa CUF.

Kwa upande wake Chama cha NCCR Mageuzi kupitia Katibu Mkuu Sam Ruhuza kimesema kitashiriki kikamilifu mapokezi hayo kwani CHADEMA siyo adui yao bali adui yao ni CCM tu.

Wabunge wa CHADEMA na NCCR waliungana pamoja bungeni kupinga uonevu,ukandamizaji na udhalilishaji wa Spika wa bunge Anne Makinda na Naibu wake Job Ndugai dhidi ya Upinzani bungeni.Hata hivyo mara zote CUF wamekuwa wakiungana na wabunge wa CCM kuwapinga wapinzani wenzao.

Kesho Jumapili CHADEMA imepanga mapokezi makubwa na maandamano kisha mkutano mkubwa wa hadhara Temeke Mwisho kwa lengo la kulaani ukandamizaji wa Spika na Naibu wake.

Source:Tanzania daima/Nipashe.
Kesho Chadema waeleze vizuri watu wa temeke kwani wanajua Mhashamu Kadinal Pengo ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,pamoja na Padri Slaa ambae nae ni Katibu Mkuu Chadema,wanasema Chama cha Kikatoliki,huku temeke ndivyo wanavyo fahamu kesho wasipo sema jambo hilo mkutano utakua hauna maana kabisa na uelewa wa Chadema kuwa ni chama cha Kanisa ume enea sana Temeke yote! Angalizo mhimu sana!
 
Mkuu taja jimbo moja Tanzania bara linalo shikiliwa na mbunge kutoka CUF. Taja jimbo kisha na mbunge wake. Ukiweza kufanya hivi mimi nitaomba radhi kwa post yangu.

Jimbo: Lindi mjini
\Mbunge: Salumu Baruani.
 
Mkuu taja jimbo moja Tanzania bara linalo shikiliwa na mbunge kutoka CUF. Taja jimbo kisha na mbunge wake. Ukiweza kufanya hivi mimi nitaomba radhi kwa post yangu.

yupo baruani wa lindi mjini na mbunge wa kilwa.msijidanganye kaka kwa kujitekenya na kucheka.
 
yupo baruani wa lindi mjini na mbunge wa kilwa.msijidanganye kaka kwa kujitekenya na kucheka.

Majimbo ya CHADEMA 2015 yatapungua, ngoja uone, halafu CUF tunarudi kushikilia kambi ya upinzani 2015.

CHADEMA inategemea nguvu ya wagombea zaidi kuliko chama wakati ni kinyume chake kwa CUF. 2015 lazima wachemshe!
 
Sasa kama cuf kina hazina ya wataalamu waliobobea katika uchumi wa kimataifa na mumo serikalini kwa kushirikiana na mwandani wenu ccm mbona bado nchi yetu iko hoi bin taaban kiuchumi na kijamii?

Na kama kweli cuf ina wataalamu waliobobea, walishindwa nini kutumia taaluma zao na ubobezi wao katika majadiliano hadi Mbowe akawazidi nguvu? Huo usomi wao na ubobezi wao hauna tija yoyote kwa chama chenu.

Mbowe alizidi nguvu katika nini?
 
Ni Mtatiro ndo hataenda lakini wananchi kama kawa pipooooooooooooooøoooooz powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom