CHADEMA wanaingilia Ngome ya CUF - Mtatiro

CHADEMA wanaingilia Ngome ya CUF - Mtatiro


Ni katika hali ya kutafuta uungwaji mkono wa vyama vingine, ili siku nyingine nao tuwashitaki kwa wananchi kuwa wanaungana na CCM kuwakandamiza watz kama wanashindwa kuungana nasi kuwatetea.

For what, msimamo wa CUF siunaeleweka jamani?
 
Hili gazeti ni sawa na gazeti la uhuru. Yanaandika habari za upande mmoja hayana maana yeyote.

Kwa sababu hawana sababu ya kuandika za upande mwingine magazeti na tv zote zinaripot..hili gazet kazi yake ni kubalance..ulizia mauzo!
 
Katika hali ya kushangaza Naibu Katibu Mkuu wa CUF Julius Mtatiro amesema CHADEMA kufanya maandamano na Mkutano Temeke Mwisho ni kuingilia ngome yao.

Akizungumzia mwaliko wa CHADEMA kuitaka CUF kushiriki mapokezi ya wabunge wa upinzani kesho na hatimaye kushiriki mkutano wa pamoja Mtatiro amesema kamwe CUF haiwezi kushirikiana na CHADEMA.

Mtatiro amesema mwaliko wa CHADEMA ni wa kisanii na wamegundua Temeke ni ngome kuu ya CUF kwa hiyo CHADEMA haiwezi kupata watu mkutanoni bila kuishirikisha CUF.Mtatiro ameuliza tangu lini Chadema imegundua CUF siyo CCM B? Mtatiro amelalamika CHADEMA inatafuta umaarufu Temeke kupitia mgongo wa CUF.

Kwa upande wake Chama cha NCCR Mageuzi kupitia Katibu Mkuu Sam Ruhuza kimesema kitashiriki kikamilifu mapokezi hayo kwani CHADEMA siyo adui yao bali adui yao ni CCM tu.

Wabunge wa CHADEMA na NCCR waliungana pamoja bungeni kupinga uonevu,ukandamizaji na udhalilishaji wa Spika wa bunge Anne Makinda na Naibu wake Job Ndugai dhidi ya Upinzani bungeni.Hata hivyo mara zote CUF wamekuwa wakiungana na wabunge wa CCM kuwapinga wapinzani wenzao.

Kesho Jumapili CHADEMA imepanga mapokezi makubwa na maandamano kisha mkutano mkubwa wa hadhara Temeke Mwisho kwa lengo la kulaani ukandamizaji wa Spika na Naibu wake.

Source:Tanzania daima/Nipashe.

Huu ni uchanga wa kisiasa na cheap reason ya kutoshiriki kwenye maandamano. Ijulikane tu kuwa TZ ni ya wote na si ngoma ya mtu ama chama kimoja
 

Ni katika hali ya kutafuta uungwaji mkono wa vyama vingine, ili siku nyingine nao tuwashitaki kwa wananchi kuwa wanaungana na CCM kuwakandamiza watz kama wanashindwa kuungana nasi kuwatetea.
Mbona kule bungeni haya mlikuwa hamyaoni uwaziri kivuli shida kwa CUF wakati wao wanaongoza pale bungeni waliwapa unaibu wacheni unafiki
 
For what, msimamo wa CUF siunaeleweka jamani?

Ni kweli mkuu, lakini wananch wa CUF ni watz kama tulivyo sisi, na kumbuka, kilichoungana na ccm zanzibar ni chama na siyo wanachama, kuna wanaCUF hawapendi kabisa kilichotokea Zenji, ndio maana tunajaribu kuwatafuta na kuwarudisha kwenye mstari. Watarudi tu, we utaona kama wanaCUF hawahudhuria huo mkutano.
 
Imenikumbusha kuwa mwanzoni Sir Elton John alikuwa anakana yeye siyo shoga, hadi baadae sana.Hongera Mtatiro kwa kukiri hili...

Tuko unapindisha maana ya maneno ya Mtatiro kwa makusudi. Walichotaka kufanya CDM ni kuitumia CUF kwa maslahi yake. Ni marangapi tumesikia wafuasi wa CDM na viongozi wao wakiita CUF CCM B bila ya justification yoyote?
 

Ni kweli mkuu, lakini wananch wa CUF ni watz kama tulivyo sisi, na kumbuka, kilichoungana na ccm zanzibar ni chama na siyo wanachama, kuna wanaCUF hawapendi kabisa kilichotokea Zenji, ndio maana tunajaribu kuwatafuta na kuwarudisha kwenye mstari. Watarudi tu, we utaona kama wanaCUF hawahudhuria huo mkutano.

Hauwezi kuwarudisha wana cuf kwenye mstari kwa kuongozana na viongozi wao, siasa ni ideological issue, waende wamwage sera, na kama target ni wanachama wa cuf basi waende na maelezo customized kwao, ama sivyo hakuna haja ya kila mtu kuwa mwana CHADEMA, CHADEMA ni lazima ijiandae kupigiwa kura na watu wasio na vyama na watu wenye vyama. wanataka nchi nzima tuwe CHADEMA ili iweje? wanataka kuua upinzani?
 
Tuko unapindisha maana ya maneno ya Mtatiro kwa makusudi. Walichotaka kufanya CDM ni kuitumia CUF kwa maslahi yake. Ni marangapi tumesikia wafuasi wa CDM na viongozi wao wakiita CUF CCM B bila ya justification yoyote?

Justification ipi zaidi ya hii ya kupinga kupingwa kwa CCM?
 
hapa ndio nimegundua Mtatizo yupo kimaslahi zaidi kwa ajili ya CCM
upinzani wapo kuingoa CCM na bila kuungana hawataweza kumtokomeza nduli CCM
heko NCCR unganeni pamoja lenu moja achaneni na huyo kibaraka CCMB
 
Wa matamshi ya Mtatiro...

Mtatiro alikuwa anawasuta CDM ambao wanasema wasichokiamini.

Wanasema maandamano ni ya wapinzani lakini yakiisha wanaiita CUF CCM B. Hicho ndicho ambacho CUF hawakitaki. Ni ujuha kukubali kutumika!
 
Tuko Walichotaka kufanya CDM ni kuitumia CUF kwa maslahi yake. Ni marangapi tumesikia wafuasi wa CDM na viongozi wao wakiita CUF CCM B bila ya justification yoyote?
Chadema waitumie CUF? huijui Chadema nini!!
 
Back
Top Bottom