saronga
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 909
- 218
Dr Slaa amekuwa mbunge wa Karatu 1995 to 2005: ni sawa na miaka 15 na 2010 akagombea urais, vile vile 2015 ndiye mgomea wenu! Inakua miaka mingapi kwenye uongozi? 25 years, is it too much for him? Au CHADEMA haina hazina ya wsomi kushika hizo nafasi kwa vipindi vyote hivyo? Au DR ni mgombea wa kudumu na yeye?
Maalim Seif amekuwa waziri Kiongozi kwa muda gani?? pamoja na kuwa Waziri kiongozi mhaini kwa muda mrefu bado amekuwa ndo mgombea pekee wa urais kupitia CUF tokea 1995 hadi mlipoamua kufunga ndoa na maccm ili tu apate ving'ora vya kumsindikiza kama enzi zile za uwaziri kiongozi Hachokiiii?? ina maana CUF huko Zenji ni Maalim peke yake??? Hivi bado anaamini atakuja kuwa Rais wa zenji, kama bado namshauri afute kabisa mawazo hayo, awaachie na wengine wajaribu, 20 yrs ya ugombea + >15 yrs ya uwaziri kiongozi inamtosha, ameshachuja. Lipumba naye kujiita mlima K'njaro wakati hata urefu wa kichuguu hajaufikia ni pumba tu, yule hata akigombea udiwani kule kwao TB hataambulia kitu, arudi chuo akafundishe, huko ndo kunamfaa, siasa zimeshamuweka kando.