Mimi mpenda mabadiliko Tanzania nimefuatilia uchaguzi mdogo wa Ubunge wa Igunga na kuona jinsi kampeni zilivyokuwa.
Kumetokea matukio mbalimbali ya kukashifiana,kumwagiana tindikali,bastola mkutanoni,kufyatua risasi nk ambayo kwa namna moja ama nyingine yalitia dosari kampeni za uchaguzi huo.
Ukiangalia kwa makini utaona kuwa hayo matukio yamehusisha wanachama wa vyama tofauti lakini tukio la kumkamatwa na kushikiliwa kwa DC wa Igunga kipindi kabla ya kampeni ni tukio lililokihusisha Chadema moja kwa moja kama chama.Hili tukio halikuwa la kistaarabu kwa kuwa DC wa Igunga alikuwa kwenye majukumu yake ya kazi na hakupaswa kudhalilishwa kiasi kile.
Tukubali tusikubali ni kwamba kitendo cha kumdhalilisha DC wa Igunga kimewapunguzia KURA Chadema kwa kuwa CCM + magazeti yao walichukua hicho kitendo kama mtaji wao wa kisiasa na wamefanikiwa kwa hilo.
Kwa heshima na taadhima napenda kumuomba Dr.Slaa kwa niaba ya CDM wamuombe radhi DC wa Igunga na wananchi wote wa Igunga na hii itaonesha kuwa CDM imestaarabika na ni chama cha waadilifu na itawezesha CDM kukubalika zaidi jimboni humo.
Kumetokea matukio mbalimbali ya kukashifiana,kumwagiana tindikali,bastola mkutanoni,kufyatua risasi nk ambayo kwa namna moja ama nyingine yalitia dosari kampeni za uchaguzi huo.
Ukiangalia kwa makini utaona kuwa hayo matukio yamehusisha wanachama wa vyama tofauti lakini tukio la kumkamatwa na kushikiliwa kwa DC wa Igunga kipindi kabla ya kampeni ni tukio lililokihusisha Chadema moja kwa moja kama chama.Hili tukio halikuwa la kistaarabu kwa kuwa DC wa Igunga alikuwa kwenye majukumu yake ya kazi na hakupaswa kudhalilishwa kiasi kile.
Tukubali tusikubali ni kwamba kitendo cha kumdhalilisha DC wa Igunga kimewapunguzia KURA Chadema kwa kuwa CCM + magazeti yao walichukua hicho kitendo kama mtaji wao wa kisiasa na wamefanikiwa kwa hilo.
Kwa heshima na taadhima napenda kumuomba Dr.Slaa kwa niaba ya CDM wamuombe radhi DC wa Igunga na wananchi wote wa Igunga na hii itaonesha kuwa CDM imestaarabika na ni chama cha waadilifu na itawezesha CDM kukubalika zaidi jimboni humo.