CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

Akaunti ya X (Twitter) ya Chadema iliyokuwa ikijulikana kama ChademaTz. Akaunti hii, ambayo kwa muda mrefu imekuwa chombo muhimu cha mawasiliano na taarifa za Chama, imechukuliwa na kuuzwa kinyume na taratibu na maadili ya Chama.

Taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa aliyekuwa Afisa wa Chadema, Abdulkarim Muro, alihusika kuiuza kwa John Marwa, ambaye sasa anaitumia kupitia chombo chake kingine cha habari cha Royal Television.

Kwa kuzingatia hali hii, tunatoa wito kwa Abdulkarim Muro na John Marwa kurejesha akaunti hiyo kwa Chama ndani ya muda wa siku tatu kuanzia leo.

Iwapo watalazimika kupuuza wito huu, tutatangaza hatua ya pili ya kuchukua.
1774110406799.jpg
 
JOPO LA MAWAKILI WA CHADEMA TAYARI LIMEWASILI DODOMA.

Timu ya mawakili wa CHADEMA imewasili salama mkoani Dodoma, tayari kwa ajili ya kesi za marejeo Mahakama ya Rufaa kuanzia tarehe 24/03/2025.

Timu yetu inaongozwa na Wakili Mwandamizi, Mpale Mpoki Kaba, Dr Rugemeleza Nshala ambaye pia ni mwanasheria Mkuu wa Chama, Gaston Garubindi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Sheria wa Chama, Dickson Matata ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati kuu, Wakili Mwasipu Hekima na wakili Nashon Nkungu.

Mtakumbuka kwamba, Mahakama ya Rufaa itafanya Revision kwenye kesi ya Madai namba 8323/2025 baina ya Said Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya wadhamini wa Chama na Katibu Mkuu wa Chama, pamoja na Maombi madogo yaliyotokana na kesi hiyo ikiwa ni pamoja na Maombi yaliyosababisha Chama kuzuiwa kufanya shughuli za chama, Maombi ya kumtaka Jaji Mwanga kujitoa na kukataa na Maombi ya wadai kupatiwa nyaraka za chama !

Marejeo yote haya, yamepewa namba kama revision No. 1 /2026, civil Revision No 2/ 2026, Civil Revision No. 3/2026 na Civil Revision No. 4 /2026.
1774197216568.jpg
 
Binti aliepoteza mguu wake October 29, 2025.

Imeanzishwa media ya kuwakumbuka ndugu zetu waliouwawa Tarehe 29.10.2025.

Media hii itapost kumbukizi zote za uovu WOTE wa Serikali.

Media inatwa @mo29_tv kila MTU afanye ku Subscribe

LINK MO 29 TV
1774198639297.jpg
 
Ujumbe wa Prof Anna Tibaijuka

MAWAKILI WA CHADEMA WAKIWASILI DODOMA KUTETEA CHAMA CHAO: Ni haki kwa mlalamikaji yeyote kutafuta haki yake mahakamani ila historia inaonesha matumizi ya mifumo ya mahakama kutatua migogoro ya vyama vya siasa hayajaonesha mafanikio ya kudumu barani Afrika. Mfano mashuhuri ni ANC iliyopigwa marufuku mwaka 1960 na Makaburu, ikalazimika kufanya shughuli zake kwa siri, takriban miaka 32 viongozi wake wakifungwa au kukaa uhamishoni.

Matokeo ANC ikajijengea uhalali mkubwa ndani na nje ya nchi na hatimaye, Mfumo wa ubaguzi ulipoanguka, ANC iliibuka ikiwa na nguvu zaidi na kushinda uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia mwaka 1994 chini ya uongozi wa Nelson Mandela. Jaribio la kukiondoa chama hicho kupitia sheria liliishia kukiimarisha.

Pili ni Senegal, chama cha PASTEF kilipigwa marufuku mwaka 2023. Hatua hiyo ilichochea hisia za wananchi dhidi ya kile kilichoonekana kama ukandamizaji wa kisiasa, na mwaka mmoja tu baadaye, 2024, viongozi wanaohusishwa na chama hicho walishinda urais. Tukio hili linaonyesha jinsi hatua za kisheria zinavyoweza kubadili chama cha upinzani kuwa alama ya mapambano ya kisiasa.

Tatu, Gambia, wakati wa utawala wa Yahya Jammeh, vyama vya upinzani vilikumbana na vizuizi vikali, ikiwa ni pamoja na kupigwa marufuku. Hata hivyo, vyama hivyo vilijipanga upya, vikaungana, na hatimaye kushinda uchaguzi wa mwaka 2016. Hivyo basi, ukandamizaji haukuondoa nguvu zao bali uliwafanya wawe na mshikamano zaidi.

Tanzania tunatambuliwa kuvisaidia vyama vya ukombozi wa Afrika hadi uhuru wao, huku vikiwa vimepigwa marufuku na tawala za kikoloni ikiwemo: ZANU-PF ya Zimbabwe, MPLA ya Angola, na FRELIMO ya Msumbiji.

Matumizi ya mahakama katika ushindani wa kisiasa hakulipi. USHAURI WANGU TUJISAHIHISHE NDANI NA NJE YA VYAMA VYETU kushindania uongozi bora hasa wakati huu tunapohitaji MARIDHIANO na MSHIKAMANO ili kulileta taifa letu Pamoja.
1774241129594.jpg
 
Tarehe 29 Mwezi huu ni siku ya kuwaenzi na kuwakumbuka watanganyika wenzetu waliouwawa kwenye maandamano MO 29 TV kuwa sehemu ya maadhimisho haya #share
1774343251048.jpg
 
George Sanga, msaliti wa Watanzania, amezua mjadala mpana katika jamii kufuatia hatua yake ya kubadili msimamo na kuacha njia ya mapambano ya haki na demokrasia. Kitendo chake kinatazamwa na wengi kama usaliti mkubwa dhidi ya jitihada za pamoja zilizojengwa kwa muda mrefu kwa gharama na mchango wa wananchi waliomuamini na kumsimamia katika nyakati ngumu.

Kwa mujibu wa kumbukumbu za matukio yaliyoshuhudiwa na umma, George Sanga aliwahi kukumbwa na kesi nzito ya mauaji iliyokuwa na adhabu kali. Katika kipindi hicho kigumu, Watanzania waliinuka kwa pamoja na kumuunga mkono kwa hali na mali, wakimchangia fedha za chakula akiwa gerezani, kusaidia familia yake kwa mahitaji ya kila siku, pamoja na kugharamia ada ya elimu ya mtoto wake. Baada ya kutoka gerezani, wananchi hao hao walimchangia mtaji ili aweze kurejea katika maisha ya kawaida.

Vilevile, viongozi na wanachama wa CHADEMA walionyesha mshikamano mkubwa kwa kufunga safari kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania kwenda kumtembelea na kumtia moyo alipokuwa kifungoni. Hatua hizi zilidhihirisha wazi imani na matumaini makubwa yaliyowekwa juu yake kama sehemu ya harakati za kuleta mabadiliko ya kweli nchini.

Hata hivyo, katika hali inayozua masikitiko makubwa, George Sanga ameondoka katika chama hicho na kujiunga na CHAUMA, huku akianza kutoa kauli za kejeli na dharau kwa wapigania haki na demokrasia. Aidha, hatua yake ya kuonekana kuwatetea wale waliowahi kumuweka gerezani imeibua hisia kali za kusalitiwa miongoni mwa wananchi waliowahi kusimama naye.

Mabadiliko haya ya ghafla ya msimamo yanaibua maswali makubwa kuhusu uaminifu, uadilifu na dhamira ya kweli ya viongozi ndani ya harakati za kijamii na kisiasa. Jamii inatarajia uwajibikaji na msimamo thabiti kutoka kwa wale wanaopewa dhamana ya kuongoza na kuwakilisha sauti za wananchi.

Wito unatolewa kwa wadau wote wa haki na demokrasia kuendelea kuwa imara, kushikamana na kutetea misingi ya haki na ukweli bila kuyumbishwa na matukio ya mtu mmoja. Mapambano ya haki na demokrasia hayawezi kusimamishwa na mabadiliko ya msimamo ya mtu binafsi, bali yataendelea kwa nguvu ya umma.
1774582330768.jpg
 
Back
Top Bottom