CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

u ikiwakamata wengi wao na kuwabambikia kesi za kuwa walikuwa wanaenda kufanya uhalifu! Just imagine kwamba jeshi letu la police limefikia hatua hii
Ombi au pendekezo:

Mambo kama haya yawekewe kumbukumbu kamili kwa kuwataja majina au cheo wahusika. Kama ni mkuu wa Polisi eneo hilo ndiye kachukua jukumu la kutengeneza sheria ya kuwakamata; atajwe tu jina na cheo chake.

Hizi ni kumbukumbu zisizofutika.

Kila tukio, mhusika mkuu wa tukio hilo ikiwezekana atajwe moja kwa moja.

Muda si muda, tutaanza kuona 'pattern' ni watu/viongozi gani hasa wapo mstari wa mbele katika maswala haya.
 
Ombi au pendekezo:

Mambo kama haya yawekewe kumbukumbu kamili kwa kuwataja majina au cheo wahusika. Kama ni mkuu wa Polisi eneo hilo ndiye kachukua jukumu la kutengeneza sheria ya kuwakamata; atajwe tu jina na cheo chake.

Hizi ni kumbukumbu zisizofutika.

Kila tukio, mhusika mkuu wa tukio hilo ikiwezekana atajwe moja kwa moja.

Muda si muda, tutaanza kuona 'pattern' ni watu/viongozi gani hasa wapo mstari wa mbele katika maswala haya.
Hakika hili ni wazo bora na wakulifanya ni sisi! Ngoja niangalie namna bora ya kuweka post kuwahusu ambayo haitaliwa kichwa
 
Hakika hili ni wazo bora na wakulifanya ni sisi! Ngoja niangalie namna bora ya kuweka post kuwahusu ambayo haitaliwa kichwa
Ni sehemu muhimu kabisa ya mapambano, mkuu wangu 'Mshana Jr'..

Hawa ndio nyenzo muhimu inayotumiwa na Samia na Genge lake. Utapambana vipi na uovu bila kujuwa silaha zinazotumiwa kukumaliza?

Ni rahisi tu kuwataja hawa; kwa sababu mkuu wa polisi Pwani ndiye mwenye mamlaka kwenye eneo hilo.
Kwa hiyo, taarifa kama hiyo iliyotolewa kwenye mada, ni kumhusisha tu huyo mkuu na tukio hilo; anakuwa sehemu ya taarifa iliyomo kwenye mada.
 
Ni sehemu muhimu kabisa ya mapambano, mkuu wangu 'Mshana Jr'..

Hawa ndio nyenzo muhimu inayotumiwa na Samia na Genge lake. Utapambana vipi na uovu bila kujuwa silaha zinazotumiwa kukumaliza?

Ni rahisi tu kuwataja hawa; kwa sababu mkuu wa polisi Pwani ndiye mwenye mamlaka kwenye eneo hilo.
Kwa hiyo, taarifa kama hiyo iliyotolewa kwenye mada, ni kumhusisha tu huyo mkuu na tukio hilo; anakuwa sehemu ya taarifa iliyomo kwenye mada.
Nitaweka uzi ndani ya siku hizi mbili
 
Ni sehemu muhimu kabisa ya mapambano, mkuu wangu 'Mshana Jr'..

Hawa ndio nyenzo muhimu inayotumiwa na Samia na Genge lake. Utapambana vipi na uovu bila kujuwa silaha zinazotumiwa kukumaliza?

Ni rahisi tu kuwataja hawa; kwa sababu mkuu wa polisi Pwani ndiye mwenye mamlaka kwenye eneo hilo.
Kwa hiyo, taarifa kama hiyo iliyotolewa kwenye mada, ni kumhusisha tu huyo mkuu na tukio hilo; anakuwa sehemu ya taarifa iliyomo kwenye mada.

View: https://www.facebook.com/share/v/18BAiTf9vs/
 
Katibu Mkuu wa BAWACHA Taifa Mhe.Pamela Maasay akiwa na Viongozi waandamizi pamoja na Wanachama wamefika Mahakama ya Wilaya ya Bunda kufuatilia kesi ya Uhaini inayomkabili aliyekuwa Katibu Mkuu wa Bavicha Taifa Mhe. Kaunya Yohana.
1773075404144.jpg
1773075407600.jpg
1773075410767.jpg
 
Uzi wa matukio mbalimbali ya CHADEMA . Madhila wanayopitia.. Vita wanazopigana.. Mafanikio wanayopa .. Na namna wanavyomgaragaza adui kwenye kila kona.. Kila saa na kila wakati
Karibuni wote! Friends and foes!
I love you. Chadema since
REGIA MTEMA My Sister
 
Wewe ulietafsiri vibaya katuni ya KIPANYA leo kuhusu bendera ya CHADEMA nakuongezea hii ya CCM ambayo imewekwa kama PAZIA LA CHOONI.

Wakati CDM inaendelea kukomaa na harakati za UKOMBOZI wa taifa letu licha ya yote bado ipo imara-huku kuna CCM ambayo haina msaada wowote kwa watanzania zaidi ndio wanaoongoza kundi la WATEKAJI NA KUUWA WATANZANIA.

REPOST 200

#TUTAKUWEPO🫵😎
1773308195513.jpg
1773308192976.jpg
 
VIDEO HII IMEBEBA MAUMIVU MAKUBWA.

Video hii ilichukuliwa nje ya kituo cha Polisi bandari, Mimi nilifika katika kituo hiki kufuatilia dhamana ya Deusdedith Soka, katika video hii niliwambia Polisi wamempokonya mawasiliano Soka ili wamteke kweli baadae yalitokea hayo.

Pili mkono wangu wa kulia kwenye video hii yupo Juma Kaswahili mwenye kapelo na Jacob Mlay amevaa nguo nyeusi hawa wote wametekwa.

Kwa hali hii unawezaje kulala ukapata usingizi? Kwa hali hii unawezaje kunyamaza kimya? Kiukweli kukaa kimya haiwezekani kwani hata Mimi na wewe hatupo salama.

Ameandika Twaha Mwaipaya

View: https://www.facebook.com/share/v/1MmHwnki72/
 
Bendera iliyochanika lakini bado inapepea.

Katika sanaa ya kisiasa, bendera iliyoharibika mara nyingi huashiria kuwa kundi au harakati imepitia mashinikizo, migogoro, au mashambulizi ya kisiasa. Bendera bado ipo juu ya mlingoti na inapepea. Hii ni ishara ya ustahimilivu na kuendelea kuwepo.

Upepo mkali unaopeperusha bendera.

Upepo tunaweza kutafsiri kama nguvu kutoka nje—pressure ya kisiasa, vyombo vya dola, au mazingira magumu ya ushindani wa kisiasa. Kwa mtazamo wa kisiasa, upepo unatafasiriwa kama ishara ya nguvu au shinikizo linalotoka kwa dola au mfumo wa utawala.

Mawingu mazito angani.

Mawingu katika sanaa mara nyingi hutumika kuonyesha hali ya sintofahamu, mgogoro, au kipindi kigumu. Hivyo anga lenye mawingu linaweza kuwakilisha mazingira ya kisiasa yenye mvutano katika Tanzania, hasa wakati wa ushindani mkali uliopo kati ya CHADEMA na DOLA.

Mlingoti mrefu unaoshikilia bendera.

Huu unaweza kuashiria msingi wa harakati—yaani wanachama, wafuasi, au misingi ya chama. Hata kama bendera imechanika, mlingoti bado umesimama na umenyooka wima, ikimaanisha kwamba msingi wa harakati bado haujaanguka. Bado upo imara.

Kwa kuzingatia harakati nyingi za kisiasa barani Afrika, harakati za wananchi zinapofikia hatua fulani, haziwezi tena kusimamishwa na nguvu tu za dola. CHADEMA imepita maumivu mengi — viongozi kufungwa, mikutano kupigwa marufuku, wanachama kunyanyaswa.

Katika historia, harakati zinazozaliwa kutokana na kile wananchi wanachoona kama ukandamizaji mara nyingi huimarika zaidi kadiri shinikizo linapoongezeka. Kila shambulizi kutoka kwa “dola katili” linatafsiriwa kama uthibitisho harakati hiyo ina ukweli unaoogopwa.

CHADEMA sasa ni imani. Itikadi ya CHADEMA imejikita ndani ya mioyo ya watu. Kitalaam, taasisi ikishafikia hatua ya kuwa harakati (movement), inakuwa vigumu kuizima kwa kutumia nguvu za dola pekee, kwa sababu huwezi “kufunga” au “kupiga marufuku” fikra.

CHADEMA imeshambuliwa sana na dola katili la CCM lakini bado inapepea. CHADEMA ni movement siyo tena chama cha siasa. Dola katili ya MaCCM inatakiwa kuelewa kwamba, CHADEMA ni imani ya watanzania. Hakuna idadi ya vitisho ambayo itawaogopesha.

NB; huu ni mtazamo wangu binafsi. Ukweli na usahihi wa kazi hii ya sanaa ni wa mtunzi, Masoud Kipanya
IMG-20260313-WA0027.jpg
 
TUKUTANE MAHAKAMA YA DODOMA

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kupitia kwa mawakili na viongozi wake wakuu kilimwandikia barua Jaji Mkuu, George Masaju kikimlalamikia juu ya jinsi kesi ya mgawanyo wa mali ambayo imesababisha chama kufungiwa/kuzuiliwa kufanya shughuli zake za kisiasa inavyoendeshwa. Baada ya Jaji Mkuu kupokea malalamiko hayo aliamua kuitisha kesi hiyo (file) yeye mwenyewe (suo moto) kwa mamlaka aliyonayo kutoka Mahakama kuu. Sasa hatimaye mahakama ya rufaa imetoa wito (summons) kwa pande zote mbili ili kupitia malalamiko hayo mahakama ya rufaa ifanye marejeo (revision) kwa lengo la kuona kama malalamiko ni ya msingi au la na endapo mahakama ya Rufaa itaona na kujiridhisha kuwa kulikuwa na shida kwenye amri zilizokuwa zinatolewa na jaji wa mahakama kuu basi itazitupilia mbali na pengine sasa chama kitaruhusiwa kuendelea na shughuli zake za kisiasa kama kawaida.

Tukutane Dodoma tarehe 24/3/2026.

Wanachama na wapenda haki wote mnakaribishwa.
1773419124303.jpg
 
Back
Top Bottom