CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

BREAKING NEWS

Mahakama ya rufani Dodoma imeiruhusu Chadema kuendelea na majukumu yake ya kisiasa imetengua amri batili ya mahakama Kuu.
1776264950688.jpg
 
UJUMBE WA DADA WA TAIFA MANGE KIMAMBI, LEO MARA BAADA YA KUICHANGIA CHADEMA DOLA ELFU MOJA

Chadema pokeeni huu mchango wangu ambao umetokana na pesa ambazo Watanzania wananipa kupitia subscription za Mange Kimambi App na subscription za account ya Instagram ambayo imefungwa ( ni maajabu account imefungwa ila bado wananikusanyia mapato kila mwezi na kunitumia).

Hizi pesa mmpewa na Watanzania sio na Mange Kimambi maana bila Watanzania hii pesa nisingekuwa nayo.

Ahsanteni sana Watanzania kwa kuendelea kulipia subscription za Mange Kimambi app, although sijaweka habari zaidi ya miezi 9 sasa. Na pia Ahsanteni ambao hamja cancel subscription za page yangu ya instagram iliyofungwa (@mangekimambi80) nawaomba msicancel.

Watanzania, Chadema hawatoweza kutusaidia kudai haki kama hawana pesa yoyote. Ni lazma sisi wananchi tuwachangie.

Kama jinsi mlivyojiunga kwenye subscribption za Mange Kimambi app naomba mjiunge na subscription za Chadema. Imagine Kama Watanzania laki 2 tu mkijiunga subscription ya elfu 3 tu kwa mwezi, hiyo ni milioni 600 kila mwezi kwa Chadema.

Pia bila pesa hakuna movement ya maana Chadema wataweza kufanya. Wauwaji wanakodi zetu wanazitumia kushikilia nchi bila ridhaa yetu. Ni lazma tuwawezeshe Chadema.
1776356800435.jpg
 
Karibuni Tuchangie Chama Chetu. Tuchangie Mapambano yetu.
1776530081976.jpg
 
Mapema leo, uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ulikutana na ujumbe wa African Women Leaders Network uliokuwa ukiongozwa na aliyekuwa Rais wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf, akiwa ameambatana na aliyekuwa Rais wa Ethiopia, Sahle-Work Zewde.

Ziara ya ujumbe huo nchini Tanzania inalenga kukutana na makundi mbalimbali, ikiwemo vyama vya siasa na asasi za kiraia, kwa lengo la kukusanya na kufuatilia taarifa kuhusu matukio yaliyotokea kabla na baada ya tarehe 29 Oktoba 2025.

Kwa upande wa CHADEMA, ujumbe uliongozwa na Makamu Mwenyekiti Bara, Mhe John Heche, akifuatana na Katibu Mkuu, Mhe John Mnyika; Naibu Katibu Mkuu Bara, Mhe Amani Golugwa; Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Wakili Ali Ibrahimu; pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee, Mama Suzan Lyimo.

Katika kikao hicho, CHADEMA iliwasilisha msimamo wake rasmi kama ulivyoazimiwa na Kamati Kuu ya chama , na kueleza kwa kina matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu na vitendo vya ukatili vinavyodaiwa kutokea kabla, wakati na baada ya tarehe 29 Oktoba 2025.

Chama kinasisitiza umuhimu wa uchunguzi huru na wa haki, uwajibikaji kwa wote waliohusika, pamoja na kulindwa kwa misingi ya demokrasia, haki na utawala wa sheria nchini.
1776701888858.jpg
 
Back
Top Bottom