CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepiga fataki katika Makao Makuu yake, Edwin Mtei House, Mikocheni jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kumbukizi ya miaka 20 tangu kufanyika kwa mabadiliko makubwa ya chama mwaka 2006.

Shughuli hiyo imefanyika usiku wa leo huku wanachama na viongozi wa chama wakishiriki katika kumbukizi hiyo inayorejea kipindi kinachoelezwa kuwa kilikuwa na umuhimu mkubwa katika historia ya CHADEMA.

Kwa mujibu wa chama hicho, maadhimisho hayo yanalenga kukumbuka hatua za mageuzi zilizofanyika mwaka 2006 na mchango wake katika safari ya kisiasa ya CHADEMA ndani ya Tanzania.

Fataki hizo zimepigwa katika eneo la Makao Makuu ya chama kama ishara ya kuadhimisha miaka 20 ya mabadiliko hayo ya kihistoria.


View: https://www.facebook.com/share/v/1W4drie9e1/
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom