CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

Makamu Mwenyekiti wa Bara, Mhe. John Heche , pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Bara, Mhe. Aman Golugwa, na viongozi wengine, wamewasili katika mortuary ya Hospitali ya Mkoa wa Kigoma, Maweni, muda mfupi kabla ya kuanza kwa uchunguzi wa mwili wa marehemu Suez Dani Maradufu. Uchunguzi huo unalenga kubaini chanzo cha kifo chake.

Live Kesi ya Tundu Lissu inaendelea muda huu kufuatilia Bonyeza link hii TWAHA MWAIPAYA alafu follow channel.
1783134525165.jpg
1783134522075.jpg
1783134518840.jpg
 
Mwigulu ametoa kauli kwamba zuio la mikutano halihusiani na CHADEMA lakini mpaka tunavyoongea sahivi Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ambayo iko chini ya ofisi ya waziri mkuu imezuia kiasi cha tsh million mia tano ya ruzuku na mwigulu analijua

Baadaye wakasema chadema imepeleka barua kukumbushia jambo hili baadaye ofisi ya msajili ikatuma barua kusogeza sogeza siku ili mwaka wa serikali uishe ambao tayari umeshaisha mwezi wa 6 2025
Lengo lao waseme mwaka wa serikali imepita na serikali halihami na deni"

~katibu mkuu wa chadema Mh. John Mnyika See less
1783134680004.jpg
 
Kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Godbless Lema, ameibua mjadala wa kisiasa baada ya kuandika ujumbe kupitia mtandao wa X akitaka kuondolewa kwa uwepo mkubwa wa polisi barabarani na kusisitiza kuwa nguvu ya taifa hupimwa kwa uwezo wa kusikiliza sauti tofauti za wananchi kupitia haki na uwajibikaji. Lema alisema hali ya mashaka na tahadhari iliyopo inaweza kuathiri mazingira ya ubunifu na maendeleo.
Kauli hiyo imekuja wakati kukiwa na maandalizi ya maandamano yaliyopangwa kufanyika Julai 7, 2026, huku baadhi ya makundi ya kisiasa na kijamii yakieleza sababu na malengo ya maandamano hayo. Serikali pamoja na Jeshi la Polisi, kwa upande wao, wameendelea kusisitiza kuwa mikusanyiko ya hadhara inapaswa kufanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa ili kulinda amani na usalama wa nchi.
Mjadala huo umeibua maoni mbalimbali kutoka kwa wadau wa kisiasa na kijamii, huku ukihusisha pia kumbukumbu za maandamano ya Oktoba 29, 2025, yaliyogubikwa na mvutano kati ya waandamanaji na vyombo vya usalama. Baadhi ya wadau wameendelea kutoa wito wa kutafutiwa suluhisho la kudumu kwa masuala yanayochochea migogoro ya kisiasa nchini.
1783153915870.jpg
 
‼️HABARI MBAYA‼️

Huyu kwenye picha anaitwa Pendo Kileo ni Mwanachama wa CHADEMA kutoka Kata ya Chamazi.

Juzi alitoa taarifa Polisi kituo cha Polisi Chamazi kwamba kuna watu walitaka kumteka, akawambia Polisi kwamba maeneo ambako anaishi kuna CCTV so Polisi wanaweza kuanzia Uchunguzi wao hapo.

Leo kapigiwa simu na Polisi wa Chang’ombe wakamwambia kwamba aende ili waweze kumpatia mtaalam ambae ataenda nae kuangalia na kuchukua hiyo CCTV footage.

Sasa badala ya kupewa msaada ambao ameitiwa, Polisi wamemkamata na kumuweka ndani, familia yake imeenda Changan’ombe Polisi kufuatilia wamefukuzwa.

#FreePendoKileo
1783221452803.jpg
 
‼️HABARI MBAYA‼️

Jioni hii, July 4, 2026 watu waliojitambulisha ni Askari wa Jeshi la Police, wamewateka Viongozi Wa CHASO Mkoa wa Mbeya.

Mwenyekiti ametekwa akiwa Chuoni, Catholic University Of Mbeya,

Katibu wa CHASO Mkoa ametekwa akiwa Ofisi za CHADEMA Kanda ya Nyasa Kadege,

Mwenyekiti CHASO Tawi la Catholic University of Mbeya ametekwa akiwa Chuoni.

Viongozi hao ni-;

1. NOAH MWALWANGE (Mkiti CHASO Mkoa)
2. GWAMAKA MBOKA (Katibu CHASO Mkoa
3. Ndg WASINYO M/Kiti Tawi la CUOM.

Gari ambayo imetumika kuwateka ni HILUX nyeupe yenye usajili: DPE 8978.

Tunalitaka Jeshi la Police Mkoa Mbeya kueleza Sababu za kuwakamata na mahali wanapowashikilia.
1783272201023.jpg
 
‼️HABARI MBAYA‼️

Huyu kwenye picha anaitwa Abdalah Mnyulu ni Mwanachama wa CHADEMA, anaishi Chamazi Mbagala.

Jana majira ya jioni watu waliokuwa wamevaa kiraia ambao walijitambulisha kuwa ni maofisa wa Jeshi la Polisi wakiwa na silaha za moto na gari mbili aina ya Hilux walivamia dukani kwake na kumkamata kisha wakaondoka nae, mashuhuda wanasema watu hao walisema wanampeleka kituo cha Polisi kilichopo Mbande.

Familia yake ilifika kituo cha Polisi cha Mbande wakaambiwa hayupo, wamezunguka vituo vyote vya Polisi vilivyopo Mbagala lakini hawajafanikiwa kumpata so mpaka sasa haijulikani Polisi wamempeleka wapi.

#FreeAbdalahMnyulu
1783344710779.jpg
 
DADA WA TAIFA MANGE KIMAMBI USIKU HUU: WATANZANIA MSIPOMLINDA John Heche WANAMUUA, HE IS A WALKING DEAD MAN KWA KUKATAA MARIDHIANO FEKI NA KUTAKA WAUAJI WAWAJIBISHWE NDIPO NCHI IPONE!

“Habari niliyopewa usiku huu ni nzito sana.

Watanzania naomba mnisikilize, Heche is a DEAD MAN WALKING….

Huu mpango wa kumuondoa kama kiongozi wa Chadema kupitia kumchafua kuwa kaiba pesa za tone tone ukishindwa kumuondoa CCM watamuua ili waweze kuweka mtu ambae ataipeleka Chadema kwenye maridhiano na kimama.

Yani ni hivi, kimama anataka maridhiano na Chadema at any cost . Yani lazma yafanyike, wamemwaga pesa ndani ya Chadema kama zote ili Heche aondolewe Chadema waweze kuweka mtu wao. Unaambiwa kampeni ya kumchafua Heche ni kubwa na ndo kwanza imeanza, mnaambiwa mpaka kwenye kamati kuu ya chama wanamwaga hela ili aondolewe.

Sasa ikishindikana hiyo plan ya kumuondoa kwa kumchafua kimama yuko tayari kwenda kwenye plan B, to kill him…..

ile ticket and info alioposti Yericko sio Ai au edit it’s real. Kapewa na usalama wa taifa, although Heche hakusafiri. Ila hali ni mbaya kiasi hiko. Mombo anamstalk Heche kila anapoenda anasubiri go head ya kimama then amuue Heche.

Watanzania Heche na Lissu ndio watu wamwisho tulionao wenye msimamo mkali, tumlinde Heche kwa njia yoyote, yani hata ikibidi tupeane zamu kulala nje ya geti lake, au hata tuchange tulipie international security group waje kumlinda other wise HE IS DEAD…”

Kwa sasa John Heche. kama Tundu Lissu atapambaniwa na kila mtanzania! Hizi harakati zina damu za watanzania! Hatuwezi kukubali damu za ndugu zetu zichezewe na wanasiasa wenye tamaa!
1783579775157.jpg
 
‼️HABARI MBAYA‼️

Hawa kwenye picha ni Viongozi wa Bawacha Mkoa wa wa Tanga Katibu na Mwenyekiti.

Leo ni siku ya nne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi katika katika vituo tofauti Mkoani Tanga lakin Jeshi la Polisi halitaki kusema kwanini linawashikilia.

Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Tanga Rukia Ally anashikiliwa kituo cha Polisi Muheza.

Na Katibu wa Bawacha Mkoa wa Tanga Nasra Omar Kihiyo anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Korogwe.

#FreeRukiaAlly #FreeNasraKihiyo
1783580949244.jpg
 
KIONGOZI CHADEMA ATEKWA NA KUUAWA KWA KUKATWA NA MAPANGA!

Julius Mbalile Erick (pichani), alikuwa ni Katibu Mwenezi wa CHADEMA Kata ya Murongo Jimbo la Kyerwa mkoani Kagera. Kwa mujibu wa taarifa ya aliyekuwa Mbunge wa CHADEMA, Anatropia Theonest ambayo imetolewa leo, Julius Mbalile Erick alitekwa na kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Baada ya wanafamilia na wanachama wenzake kumtafuta alipatikana siku tatu baadaye akiwa ameuawa kwa kukatwakatwa na mapanga na kisha kutelekezwa.

Mauaji ya Julius Mbalile yanakuja katika kipindi hiki ambapo viongozi wengi na wanachama wa CHADEMA wakiwa wametekwa na wengine kukamatwa na Jeshi la Polisi huku wengine wakinyimwa dhamana katika vituo vya Polisi.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 10 Julai 2026; Saa 6:35 mchana.
1783681167077.jpg
 
MAAZIMIO YA KIKAO CHA KAMATI KUU KILICHOKETI TAREHE 30 JUNI 2026 SUNSET VISTA HOTEL, KIGOMA MJINI.
1783681420111.jpg
1783681423235.jpg
1783681425881.jpg
1783681428661.jpg
 
‼️AMKENI KIMENUKA HUKO JUMUIYA YA MADOLA (COMMONWEALTH)‼️

COMMONWEALTH MINISTERIAL ACTION GROUP

WAMETOA RATIBA YA HATUA ZA UTEKELEZAJI KWA TANZANIA NDANI YA SIKU 30, 60 NA 90

Pamoja na mambo mengine Serikali haram ya Nduli Idd Amin Mama imepewa siku 30 iwe imetatua suala la kuzuiliwa kwa Mhe. @TunduALissu kupitia njia ya kisiasa na kisheria lakini pia kuwaachilia huru watu wengine wote wanaoshikiliwa kwa sababu tu ya kutumia haki zao za msingi kwa njia ya amani.

Ndani ya siku 60 wameambiwa warejeshe upatikanaji kamili wa majukwaa ya kidijitali (digital platforms) kusitisha vitendo vya vitisho na unyanyasaji dhidi ya vyombo vya habari na watetezi wa uhuru wa kujieleza.

Ndani ya siku 90 wahakikishe waitishe jukwaa la kuaminika na shirikishi la mashauriano kati ya vyama vya siasa, likiwa na wawezeshaji wasioegemea upande wowote yani Jukwaa hilo liwe na mamlaka ya kujadili na kukubaliana kuhusu marekebisho ya mfumo wa uchaguzi, ushindani wa kisiasa, suala la watu waliowekwa kizuizini na uwajibikaji.

Lakini pia wametoa Onyo la Septemba 2026 kwamba Tanzania imeamriwa kuwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mambo hayo kabla ya mkutano maalum utakaofanyika Septemba 2026.

Onyo la Novemba 2026 (Hatua Kali): Jumuiya ya Madola imetoa onyo la mwisho kwamba isipoona maendeleo yoyote kufikia Novemba 2026, itachukua hatua kali zaidi dhidi ya Tanzania (ambayo kwa sasa tayari ipo chini ya uangalizi kwenye Agenda Rasmi

Ukisikia maji yalelowana na moto umeungua ndo kama hivi.😂😂😂
1783743260096.jpg
1783743263167.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom